Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 5

Mambo ya Kufanya ili Kuendelea Kujitenga na Ulimwengu

Mambo ya Kufanya ili Kuendelea Kujitenga na Ulimwengu

“Hamuko sehemu ya ulimwengu.”​—YOHANA 15:19.

1. Yesu alihangaikia nini usiku wenye ulitangulia kifo chake?

NI USIKU wenye kutangulia kifo cha Yesu. Anajua kama iko karibu kuacha wanafunzi wake, na anahangaikia wakati wenye kuja wa wanafunzi wake. Anawaambia hivi: “Hamuko sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 15:19) Muda fulani kisha, anasali kwa Baba yake kwa ajili yao. Anasema hivi: “Wao hawako sehemu ya ulimwengu, kama vile mimi siko sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 17:15, 16) Yesu alipenda kusema nini?

2. “Ulimwengu” wenye Yesu alizungumuzia ni nini?

2 “Ulimwengu” wenye kuzungumuziwa hapa ni watu wenye hawamujue Mungu na wenye kuwa chini ya utawala wa Shetani. (Yohana 14:30; Waefeso 2:2; Yakobo 4:4; 1 Yohana 5:19) Tunaweza kufanya nini ili tusikuwe “sehemu ya ulimwengu”? Katika sura hii, tutazungumuzia njia mbalimbali: Tunaendelea kuwa washikamanifu ku Ufalme wa Mungu na hatuunge mukono upande wowote, ni kusema, hatuunge mukono upande fulani mu mambo ya politike. Tunapinga roho ya ulimwengu. Tunaonyesha kiasi mu mambo ya kuvaa na kujipamba, na tuko na mawazo yenye kufaa juu ya feza. Tunavaa pia silaha zenye Mungu anatutolea.​—Ona Mafasirio Ingine ya 16.

UKUWE MUSHIKAMANIFU KU UFALME WA MUNGU

3. Yesu alikuwa na mawazo gani juu ya politike?

3 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, aliona kama watu walikuwa na magumu mingi na kama maisha yao ilikuwa nguvu. Aliwahangaikia sana na alipenda kuwasaidia. Je, aliamua kuwa kiongozi wa politike? Hapana. Alijua kama kile chenye watu walikuwa nacho lazima kabisa ni Ufalme wa Mungu, ao serikali. Yesu angekuwa Mufalme wa ile Ufalme, na Ufalme njo ulikuwa kichwa kikubwa cha mahubiri yake. (Danieli 7:13, 14; Luka 4:43; 17:20, 21) Yesu hakujiingiza mu mambo ya politike, na sikuzote hakuunga mukono upande wowote. Wakati alikuwa mbele ya Gavana Muroma Pontio Pilato, alisema hivi: “Ufalme wangu hauko sehemu ya ulimwengu huu.” (Yohana 18:36) Wanafunzi wake pia hawakuunga mukono upande wowote. Kitabu Sur le chemin de la civilisation kilisema kuwa Wakristo wa kwanza-kwanza “hawakukubali vyeo mu mambo ya politike.” Leo, Wakristo wa kweli wako pia na ile mawazo. Tunategemeza kwa ushikamanifu Ufalme wa Mungu na hatuunge mukono upande wowote mu mambo ya politike ya ulimwengu.​—Matayo 24:14.

Unaweza kufasiria sababu yenye inafanya uunge mukono Ufalme wa Mungu?

4. Namna gani Wakristo wa kweli wanaonyesha kama wanategemeza Ufalme wa Mungu?

4 Mabalozi wanawakilisha serikali yao mu inchi ingine, kwa hiyo, hawajiingize mu mambo ya politike ya ile inchi. Ni vile pia kuhusu Wakristo watiwa-mafuta, wenye kuwa na tumaini la kutawala pamoja na Kristo mbinguni. Paulo aliandikia Wakristo watiwa-mafuta hivi: “Sisi ni mabalozi pa nafasi ya Kristo.” (2 Wakorinto 5:20) Wakristo watiwa-mafuta wanawakilisha serikali ya Mungu. Hawajiingize mu mambo ya politike na mabishano kuhusu serikali za ulimwengu huu. (Wafilipi 3:20) Lakini, watiwa-mafuta wamesaidia mamilioni ya watu wajifunze juu ya serikali ya Mungu. “Kondoo wengine,” wenye kuwa na tumaini la kuishi milele mu ulimwengu mupya wa Mungu, wanategemeza watiwa-mafuta. Wao pia hawaunge mukono upande wowote. (Yohana 10:16; Matayo 25:31-40) Ni wazi kuwa, hakuna Mukristo mwenye anapaswa kujiingiza mu mambo ya politike ya ulimwengu huu.​—Soma Isaya 2:2-4.

5. Ni sababu gani moja yenye kufanya Wakristo waepuke kupigana vita?

5 Wakristo wa kweli wanaona waamini wenzao kama familia yao na ni wenye umoja hata kama wanatoka mu inchi gani na hata kama wako na hali gani ya maisha. (1 Wakorinto 1:10) Kama tungekuwa tunaenda ku vita, tungepigana na familia yetu wenyewe, ni kusema, waamini wenzetu, wenye Yesu alituambia tupende. (Yohana 13:34, 35; 1 Yohana 3:10-12) Zaidi ya ile, Yesu aliwaambia wanafunzi wake wapende hata maadui wao.​—Matayo 5:44; 26:52.

6. Watumishi washikamanifu wa Yehova wanaona serikali namna gani?

6 Hata kama sisi Wakristo hatuunge mukono upande wowote, tunajikaza sana ili kuwa raia wazuri. Kwa mufano, tunaheshimia serikali kwa kutii sheria zake na kwa kulipa kodi. Lakini sikuzote tunahakikisha kama tunapatia “Mungu vitu vya Mungu.” (Marko 12:17; Waroma 13:1-7; 1 Wakorinto 6:19, 20) “Vitu vya Mungu” vinatia ndani upendo wetu kwake, utii wetu, na ibada yetu. Tuko tayari kufa kuliko kukosa kumutii Yehova.​—Luka 4:8; 10:27; soma Matendo 5:29; Waroma 14:8.

PINGA “ROHO YA ULIMWENGU”

7, 8. “Roho ya ulimwengu” ni nini, na inafanya watu wakuwe namna gani?

7 Tunaonyesha kama tunajitenga na ulimwengu wa Shetani wakati tunakataa kuongozwa na “roho ya ulimwengu.” Ile roho ni namna ya kufikiri na kutenda yenye inatoka kwa Shetani, na inaongoza wale wenye hawamutumikie Yehova. Lakini Wakristo wanapinga ule mutazamo. Kama vile Paulo alisema, “sisi tulipokea, hapana roho ya ulimwengu, lakini roho yenye inatoka kwa Mungu.”​—1 Wakorinto 2:12; Waefeso 2:2, 3; ona Mafasirio Ingine ya 17.

8 Roho ya ulimwengu inafanya watu wakuwe wachoyo, wenye kiburi, na waasi. Inawafanya wafikiri kama haiko lazima wamutii Mungu. Shetani anapenda watu wafanye kile wanapenda bila kufikiria matokeo. Anapenda watu waamini kama “tamaa ya mwili na tamaa ya macho” njo mambo ya maana zaidi mu maisha. (1 Yohana 2:16; 1 Timoteo 6:9, 10) Ibilisi anajikaza zaidi sana kudanganya watumishi wa Yehova na kutuchochea kwa ujanja tufikiri kama yeye.​—Yohana 8:44; Matendo 13:10; 1 Yohana 3:8.

9. Roho ya ulimwengu inaweza kuwa na matokeo gani juu yetu?

9 Kama vile tu hewa yenye tunapumua, roho ya ulimwengu iko kila fasi. Kama hatufanye nguvu ili kupinga ile roho, inaweza kutuchochea mubaya. (Soma Mezali 4:23.) Ile inaweza kuanza mu njia zenye kuonekana kuwa haziko za mubaya, kama vile kujiacha tuchochewe na mawazo na mitazamo ya watu wenye hawamuabudu Yehova. (Mezali 13:20; 1 Wakorinto 15:33) Ao tunaweza kuchochewa na mambo kama vile pornografia, uasi-imani, ao michezo yenye kuchochea roho ya mashindano.​—Ona Mafasirio Ingine ya 18.

10. Tunaweza kufanya nini ili kupinga roho ya ulimwengu?

10 Sasa, namna gani tunaweza kuepuka kuongozwa na roho ya ulimwengu? Tunapaswa kubakia karibu na Yehova na kuacha hekima yake ituongoze. Tunapaswa kuendelea kusali ili atupatie roho yake takatifu na kuendelea kuwa na mengi ya kufanya katika utumishi wetu kwake. Yehova njo Mutu mwenye nguvu zaidi mu ulimwengu wote. Tuko hakika kuwa anaweza kutusaidia tupinge roho ya ulimwengu.​—1 Yohana 4:4.

UVAE KWA NJIA YENYE INAMULETEA MUNGU HESHIMA

11. Roho ya ulimwengu imefanya watu wavae na kujipamba namna gani?

11 Tunaonyesha pia kuwa hatuko sehemu ya ulimwengu kupitia namna yetu ya kuvaa na kujipamba. Watu wengi katika ulimwengu wanavaa ili kufanya wengine wawaangalie sana, ili kuamusha ndani ya wengine mawazo machafu, ili kuonyesha kama ni waasi, ao ili kuonyesha kama wako na feza mingi. Wengine hawahangaikie namna yao ya kuonekana. Wanaweza kuchagua kuwa ovyoovyo ao kuwa wachafu. Hatuwezi kuruhusu hali yoyote kati ya hali za ile namna ichochee uamuzi wetu juu ya kuvaa na kujipamba.

Namna yangu ya kuvaa inamuletea Yehova heshima?

12, 13. Ni kanuni gani zenye zinapaswa kutusaidia kuchagua nguo za kuvaa?

12 Kwa kuwa tuko watumishi wa Yehova, tunapenda sikuzote kuvaa muzuri, katika namna yenye kuwa safi, yenye kupendeza, na yenye kupatana na hali. Tunavaa kwa “kiasi na akili ya muzuri,” ili kuonyesha kuwa ‘tunashikamana na Mungu.’​—1 Timoteo 2:9, 10; Yuda 21.

13 Namna yetu ya kuvaa inaweza kubadilisha mawazo yenye watu wako nayo juu ya Yehova na watu wake. Tunapenda kufanya “mambo yote kwa utukufu wa Mungu.” (1 Wakorinto 10:31) Sifa ya kiasi inatia ndani kuheshimia hisia na mawazo ya wengine. Kwa hiyo, wakati tunachagua nguo za kuvaa ao kuamua namna tunapenda kuonekana, tukumbuke kuwa maamuzi yetu inaweza kuwa na matokeo juu ya wengine.​—1 Wakorinto 4:9; 2 Wakorinto 6:3, 4; 7:1.

14. Tunapaswa kufikiria nini wakati tunachagua nguo za kuvaa ku mikutano ao mu mahubiri?

14 Tunavaa namna gani wakati tuko ku mikutano yetu ao mu mahubiri? Je, tunavaa mu njia yenye kufanya wengine watuangalie sana? Nguo zetu zinafanya wengine wajisikie mubaya? Je, tunawaza kuwa namna yetu ya kuvaa haiangalie watu wengine lakini inatuangalia tu sisi wenyewe? (Wafilipi 4:5; 1 Petro 5:6) Ni kweli kwamba, tunapendaka kuonekana muzuri, lakini mambo yenye inaweza kufanya tupendeze kabisa ni sifa zetu za Kikristo. Zile sifa njo Yehova anaona wakati anatuangalia. Sifa hizo zinaonyesha vile tuko kwa ndani, ni kusema, ‘ule mutu wa siri wa ndani ya moyo, mwenye samani kubwa mbele ya macho ya Mungu.’​—1 Petro 3:3, 4.

15. Juu ya nini Yehova hatuambie nguo zenye tunapaswa kuvaa kabisa na namna tunapaswa kuonekana?

15 Yehova hakutupatia liste ya sheria zenye kuhusu nguo zenye tunaweza kuvaa na zile zenye hatuwezi kuvaa. Lakini, ametupatia kanuni za Biblia, zenye zinaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri. (Waebrania 5:14) Anapenda maamuzi yetu, ikuwe makubwa ao madogo, itegemee upendo wetu kwake na kwa watu wengine. (Soma Marko 12:30, 31.) Mu dunia yote, watu wa Yehova hawavae kwa namna ileile. Namna yao ya kuvaa inategemea desturi yao na mambo yenye wanapenda kipekee. Tofauti hizo zinapendeza na zinafurahisha.

MAWAZO YENYE KUFAA JUU YA FEZA

16. Ni nini inaonyesha kama mawazo ya ulimwengu juu ya feza inapingana na mafundisho ya Yesu? Tunapaswa kujiuliza maulizo gani?

16 Shetani anapenda watu wafikiri kama kuwa na feza na vitu vya kimwili njo kunawaletea furaha, lakini watumishi wa Yehova wanajua kama ile haiko kweli. Tunaamini maneno ya Yesu. Alisema hivi: “Hata wakati mutu iko na vitu vingi, uzima wake hautokane na vitu vyenye iko navyo.” (Luka 12:15) Feza haziwezi kutuletea furaha ya kweli. Haziwezi kutupatia marafiki wa kweli, amani ya kweli ya akili, ao uzima wa milele. Ni kweli kwamba, tuko na lazima ya vitu fulani vya kimwili, na tunapenda kufurahia maisha. Lakini Yesu alitufundisha kama tutakuwa na furaha ikiwa tuko na uhusiano wa muzuri pamoja na Mungu na ikiwa tunaona ibada yetu kuwa jambo la maana zaidi mu maisha yetu. (Matayo 5:3; 6:22, maelezo ya chini) Ujiulize hivi: ‘Nimeambukizwa na mawazo ya ulimwengu juu ya feza? Feza njo jambo lenye nafikiria na kuzungumuzia sana?’​—Luka 6:45; 21:34-36; 2 Yohana 6.

17. Kukataa mawazo ya ulimwengu juu ya feza kunaweza kukuletea faida gani?

17 Kama tunakaza akili juu ya utumishi wetu kwa Yehova na kukataa mawazo ya ulimwengu juu ya feza, maisha yetu itakuwa yenye maana. (Matayo 11:29, 30) Tutatosheka na tutakuwa na amani ya akili na ya moyoni. (Matayo 6:31, 32; Waroma 15:13) Mahangaiko yetu juu ya vitu vya kimwili itakuwa kidogo. (Soma 1 Timoteo 6:9, 10.) Tutakuwa na furaha yenye mutu anapata wakati anatoa. (Matendo 20:35) Na namna yetu ya kuishi itafanya tupate wakati mingi zaidi wa kuwa pamoja na watu wenye tunapenda. Tunaweza hata kulala muzuri zaidi.​—Muhubiri 5:12.

TUVAE “SILAHA ZOTE”

18. Shetani anajaribu kufanya nini?

18 Shetani anajaribu kuharibu uhusiano wetu pamoja na Yehova, kwa hiyo tunapaswa kufanya nguvu yetu yote ili kuulinda. Tunapambana na “majeshi ya pepo wachafu.” (Waefeso 6:12) Shetani na pepo wake wachafu hawapendi tukuwe na furaha na kuishi milele. (1 Petro 5:8) Hao maadui wenye nguvu wanapigana na sisi, lakini kwa musaada wa Yehova, tunaweza kupata ushindi juu yao!

19. Andiko la Waefeso 6:14-18 linafasiria namna gani “silaha” za Kikristo?

19 Wakati wa zamani, maaskari walivaa silaha ili kujilinda wakati wako mu uwanja wa mapigano. Vilevile, tunapaswa kuvaa “silaha” zenye Yehova ametupatia. (Waefeso 6:13) Zitatulinda. Tunasoma kuhusu ile jambo mu andiko la Waefeso 6:14-18: “Kwa hiyo, musimame imara, mukiwa mumejifunga kwenye kiuno mukaba wa ile kweli, mukiwa mumevaa bamba la kifua la haki, na mukiwa mumevaa kwenye miguu yenu viatu ambavyo ni utayari wa kutangaza habari njema ya amani. Zaidi ya mambo yote hayo, muchukue ngao kubwa ya imani, yenye kwa kuitumia mutaweza kuzimisha mishale yote yenye kuwaka moto ya ule muovu. Pia, mupokee kofia ya chuma ya wokovu, na upanga wa roho, ni kusema, neno la Mungu, na kwa kila namna ya sala na sala ya kumulilia Mungu mukiendelea kusali kila wakati katika roho.”

20. Tunapaswa kufanya nini ili “silaha” zetu zitusaidie?

20 Ikiwa askari anasahau kuvaa silaha moja kati ya silaha zake na kuacha sehemu fulani ya mwili wake bila ulinzi, ni ku ile sehemu njo kwenye adui atapiga. Kama tunapenda “silaha” zetu zitulinde, hatupaswe kusahau kuvaa hata silaha moja kati ya zile silaha. Tunapaswa kuvaa zile silaha wakati wote na kuzilinda mu hali ya muzuri. Vita yetu itaendelea mupaka wakati ulimwengu wa Shetani utaharibiwa na mupaka wakati Shetani na pepo wake wachafu hawatakuwa tena ku dunia. (Ufunuo 12:17; 20:1-3) Kwa hiyo, kama tuko tunapiganisha tamaa za mubaya ao tuko tunapambana na uzaifu fulani, hatupaswe kuchoka!​—1 Wakorinto 9:27.

21. Ni nini inaweza kutusaidia kupata ushindi juu ya Ibilisi?

21 Sisi peke yetu hatuwezi kupata ushindi juu ya Ibilisi. Lakini kwa musaada wa Yehova, tunaweza! Ili kuendelea kuwa waaminifu, tunapaswa kusali kwa Yehova, kujifunza Neno lake, na kuendelea kujiunga na ndugu na dada zetu. (Waebrania 10:24, 25) Kufanya vile kutatusaidia tubakie washikamanifu kwa Mungu na tutakuwa tayari kutetea imani yetu.

UKUWE TAYARI KUTETEA IMANI YAKO

22, 23. (a) Ni nini inaweza kutusaidia tukuwe tayari sikuzote kutetea imani yetu? (b) Tutazungumuzia nini mu sura yenye kufuata?

22 Tunapaswa kuwa tayari kutetea imani yetu kila wakati. (Yohana 15:19) Kuhusu mambo fulani, Mashahidi wa Yehova wanatenda kwa njia tofauti kabisa na watu wengi. Ujiulize hivi: ‘Ninaelewa kabisa ni juu ya nini tunatenda kwa njia tofauti? Je, niko hakika kuwa mambo yenye Biblia inasema na yenye mutumwa muaminifu na mwenye busara anasema ni ya kweli? Je ninajivunia kuwa Shahidi wa Yehova? (Zaburi 34:2; Matayo 10:32, 33) Ninaweza kufasiria wengine mambo yenye ninaamini?’​—Matayo 24:45; Yohana 17:17; soma 1 Petro 3:15.

23 Mu hali za mingi, ni mwepesi kujua mambo yenye tunapaswa kufanya ili kuendelea kujitenga na ulimwengu. Lakini wakati ingine, haiko mwepesi kujua. Shetani anajaribu kutukamata kupitia mitego mbalimbali. Moja kati ya mitego yenye anatumia ni mambo ya kujifurahisha. Namna gani tunaweza kuchagua kwa hekima mambo ya kujifurahisha nayo? Tutazungumuzia ile jambo mu sura yenye kufuata.