Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 2

Kuwa na Zamiri ya Muzuri Mbele ya Mungu

Kuwa na Zamiri ya Muzuri Mbele ya Mungu

“Muendelee kuwa na zamiri ya muzuri.”​—1 PETRO 3:16.

1, 2. Juu ya nini tuko na lazima ya mutu ao kitu fulani ili kutuongoza wakati tuko kwenye hatujue? Yehova ametupatia nini ili kutuongoza?

WAZIA uko unatembea mu jangwa kubwa. Eneo lenye uko unapitia linaendelea kubadilika kadiri upepo mukubwa unapeleka muchanga huku na huku. Ni mwepesi kupotea. Namna gani utajua kwenye unapaswa kuenda? Uko na lazima ya mutu fulani ao kitu fulani ili kukuongoza. Inaweza kuwa dira (ao, boussole), jua ao nyota, karte, ao hata mutu mwenye anajua jangwa hilo muzuri. Kuwa na mutu ao kitu fulani ili kukuongoza ni jambo la maana, kwa sababu kujua kwenye unaenda kunaweza kuokoa uzima wako.

2 Sisi wote tunakutana na magumu mingi mu maisha, na wakati fulani ni mwepesi kujisikia kuwa tumepotea. Lakini ili kutuongoza, Yehova amepatia kila mumoja wetu zamiri. (Yakobo 1:17) Tuone basi zamiri ni nini na namna inatumika. Kisha tutajifunza namna ya kuzoeza zamiri yetu, juu ya nini tunapaswa kuhangaikia zamiri ya wengine, na namna gani kuwa na zamiri safi kunaweza kufanya maisha yetu ikuwe muzuri zaidi.

ZAMIRI NI NINI NA INATUMIKA NAMNA GANI?

3. Zamiri ni nini?

3 Zamiri yetu ni zawadi ya muzuri kutoka kwa Yehova. Ni uwezo wenye kuwa ndani yetu wenye unatusaidia kujua mambo ya muzuri na mambo ya mubaya. Mu Biblia, neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa na neno “zamiri” linamaanisha “kujijua.” Wakati zamiri yetu inatumika muzuri, inatusaidia kuchunguza ikiwa tuko kabisa watu wa namna gani. Inaweza kutusaidia tuchunguze waziwazi mawazo na hisia zetu za ndani sana. Inaweza kutuongoza kufanya mambo ya muzuri na kutusaidia tuepuke mambo ya mubaya. Na inaweza kufanya tufurahi wakati tunakamata maamuzi ya muzuri ao tujilaumu kisha kukamata maamuzi ya mubaya.​—Ona Mafasirio Ingine ya 5.

4, 5. (a) Ni nini ilitokea wakati Adamu na Eva walikataa kusikiliza zamiri yao? (b) Ni mifano gani ya Biblia yenye kuonyesha namna zamiri inatumika?

4 Kila mumoja wetu anaweza kuchagua ikiwa atasikiliza zamiri yake ao hapana. Adamu na Eva walichagua kukataa kusikiliza zamiri yao, na kwa hiyo walifanya zambi. Kisha, zamiri yao ilianza kuwasumbua, lakini walikuwa wamechelewa sana. Tayari walikuwa wamekosa kumutii Mungu. (Mwanzo 3:7, 8) Hata kama wote walikuwa na zamiri yenye kukamilika na walijua kama ni mubaya kukosa kumutii Mungu, walichagua kukataa kusikiliza zamiri yao.

5 Kwa upande mwingine, wanadamu wengi wenye hawakamilike walisikiliza zamiri yao. Yobu alikuwa mufano muzuri. Kwa kuwa alikamata maamuzi ya muzuri, alisema hivi: “Moyo wangu hautanihukumu wakati wote wenye nitakuwa muzima.” (Yobu 27:6) Wakati Yobu alisema “moyo wangu,” alizungumuzia zamiri yake, ni kusema, uwezo wake wa kujua mema na mabaya. Lakini wakati fulani, Daudi hakusikiliza zamiri yake na alikosa kumutii Yehova. Kisha alijisikia mwenye kosa sana hivi kwamba ilikuwa kama vile moyo wake ulikuwa ‘unamulaumu.’ (1 Samweli 24:5) Ile ni zamiri ya Daudi yenye ilikuwa inamuambia kama amefanya kosa. Kusikiliza zamiri yake, kungemusaidia aepuke kufanya tena ile kosa.

6. Juu ya nini tunaweza kusema kama zamiri yetu ni zawadi kutoka kwa Mungu?

6 Hata watu wenye hawamujue Yehova mara mingi wanatambua kama kuko mambo yenye kuwa sawa na mambo yenye haiko sawa. Biblia inasema hivi: “Kwa mawazo yao wenyewe wanashitakiwa ao hata wanatetewa.” (Waroma 2:14, 15) Kwa mufano, watu wengi wanajua kama ni mubaya kuua ao kuiba. Hata kama wanaweza kuwa hawatambue jambo hilo, kwa kweli wanasikiliza zamiri yao, ni kusema, uwezo wa kujua mambo ya muzuri na mambo ya mubaya wenye Yehova alitia ndani yao. Wanafuata pia kanuni za Mungu, ao kweli za musingi zenye Yehova aliweka ili zitusaidie kukamata maamuzi ya muzuri mu maisha.

7. Juu ya nini wakati fulani zamiri yetu inaweza kutudanganya?

7 Lakini wakati fulani zamiri yetu inaweza kutudanganya. Kwa mufano, inaweza kuharibishwa na mawazo na hisia zetu zenye hazikamilike na inaweza kutuongoza mu njia ya mubaya. Hatuwezi kupata zamiri ya muzuri bila sisi kufanya jambo lolote. (Mwanzo 39:1, 2, 7-12) Tunapaswa kuizoeza. Ili kutusaidia, Yehova anatupatia roho yake takatifu na kanuni za Biblia. (Waroma 9:1) Acha tuone namna tunaweza kuzoeza zamiri yetu.

NAMNA GANI TUNAWEZA KUZOEZA ZAMIRI YETU?

8. (a) Namna gani mawazo ya moyo wetu inaweza kufanya zamiri yetu ishindwe kutumika muzuri? (b) Tunapaswa kujiuliza ulizo gani mbele ya kukamata uamuzi fulani?

8 Watu fulani wanawaza kama kusikiliza zamiri yao kunamaanisha tu kufuata mawazo ya moyo wao. Wanawaza kama wanaweza kufanya jambo lolote lenye wanapenda kama jambo hilo haliwasumbue. Lakini moyo wetu haukamilike, na unaweza kutudanganya. Tamaa za moyo wetu zinaweza kuwa zenye nguvu na kufanya zamiri yetu ishindwe kutumika muzuri. Biblia inasema hivi: “Moyo ni mudanganyifu kuliko kitu kingine chochote na uko hatari. Ni nani anaweza kuujua?” (Yeremia 17:9) Kwa hiyo tunaweza kuanza kuwaza kama jambo fulani ni la muzuri wakati jambo hilo ni la mubaya. Kwa mufano, mbele Paulo akuwe Mukristo, alitesa mubaya sana watu wa Mungu na aliamini kuwa jambo lenye alikuwa anafanya lilikuwa la muzuri. Kulingana na mawazo yake, alikuwa na zamiri ya muzuri. Lakini alifikia kusema hivi: “Mwenye ananichunguza ni Yehova.” (1 Wakorinto 4:4; Matendo 23:1; 2 Timoteo 1:3) Wakati Paulo alijua namna Yehova alijisikia juu ya mambo yenye alikuwa anafanya, alitambua kama alipaswa kubadilika. Ni wazi kama, mbele tufanye jambo fulani, tunapaswa kujiuliza, ‘Yehova anapenda nifanye nini?’

9. Kumuogopa Mungu maana yake nini?

9 Wakati unapenda mutu fulani, unaepuka kumuchukiza. Kwa kuwa tunamupenda Yehova, tunaepuka kufanya jambo lolote lenye litamuchukiza ao kumukasirisha. Tunapaswa kuogopa kumuchukiza Yehova, na woga huo unapaswa kuwa wenye nguvu sana. Hilo linaonyeshwa wazi kupitia mufano wa Nehemia. Akiwa gavana, alikataa kutumia mamlaka yake ili akuwe tajiri. Juu ya nini? Alifasiria kama ilikuwa “kwa sababu ya kumuogopa Mungu.” (Nehemia 5:15) Nehemia hakupenda kufanya jambo lolote lenye lingemuchukiza Yehova. Kama Nehemia, sisi pia tunaogopa kumuchukiza Yehova. Kwa hiyo, tunaepuka kufanya jambo fulani la mubaya. Tunaweza kujua mambo yenye kumufurahisha Yehova kwa kusoma Biblia.​—Ona Mafasirio Ingine ya 6.

10, 11. Ni kanuni gani za Biblia zinaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri kuhusu pombe?

10 Kwa mufano, Mukristo anaweza kuwa na lazima ya kuamua ikiwa atakunywa pombe ao hapana. Ni kanuni gani zitamusaidia kukamata uamuzi wa muzuri? Kanuni zenye kufuata zinaweza kumusaidia: Biblia haikataze kunywa pombe. Kwa kweli, inatuambia kama divai ni zawadi kutoka kwa Mungu. (Zaburi 104:14, 15) Lakini, Yesu aliambia wanafunzi wake waepuke ‘kunywa sana.’ (Luka 21:34) Na Paulo aliambia Wakristo waepuke “karamu za kupitisha mipaka na ulevi.” (Waroma 13:13) Alisema kama walevi “hawatariti Ufalme wa Mungu.”​—1 Wakorinto 6:9, 10.

11 Mukristo anaweza kujiuliza: ‘Ni kwa kiasi gani ninaona pombe kuwa ya maana? Niko na lazima ya pombe ili nijifurahishe? Ninakunywa pombe ili inisaidie nijiaminie zaidi? Ninaweza kuzuia kiasi cha pombe na mara yenye ninakunywa? * Ninaweza kupitisha wakati muzuri pamoja na marafiki hata kama hakuna pombe?’ Tunaweza kumuomba Yehova atusaidie kukamata maamuzi yenye hekima. (Soma Zaburi 139:23, 24.) Mu njia hiyo, tunazoeza zamiri yetu ikuwe tayari kufuata kanuni za Biblia. Lakini inaomba mambo mingi zaidi, kama vile tutaona.

JUU YA NINI TUHANGAIKIE ZAMIRI ZA WENGINE?

12, 13. Juu ya nini zamiri yetu inaweza kuwa tofauti na zamiri za watu wengine? Tunaweza kutenda namna gani mu hali hiyo?

12 Zamiri zinatofautiana. Zamiri yako inaweza kukuruhusu kufanya jambo fulani lenye zamiri ya mutu mwingine haimuruhusu kufanya. Kwa mufano, unaweza kuamua kunywa pombe, lakini mutu mwingine anaona kama hapaswe kunywa pombe. Sababu gani watu wawili wanaweza kuwa na mawazo tofauti kuhusu jambo hilo?

Zamiri yenye kuzoezwa inaweza kukusaidia kuamua ikiwa utakunywa pombe ao hapana

13 Mawazo ya mutu juu ya jambo fulani inaweza kuchochewa na fasi kwenye alikomalia, namna familia yake iliona jambo hilo, mambo yenye ilimupata mu maisha, na mambo ingine. Kuhusu pombe, mutu mwenye pengine zamani alikuwa na magumu ya kujizuia mbele ya pombe anaamua kukataa kunywa pombe kabisa. (1 Wafalme 8:38, 39) Kwa hiyo, ikiwa unapatia mutu fulani pombe naye anakataa, utatenda namna gani? Utakasirika? Utaendelea kumukaza ao kumulazimisha akunywe tu? Utamukaza akuambie juu ya nini amekataa? Hapana, juu unaheshimia zamiri yake.

14, 15. Ni hali gani ilitokea katika siku za Paulo? Ni shauri gani la muzuri Paulo alitoa?

14 Katika siku za mutume Paulo, kulitokea hali fulani yenye kuonyesha namna zamiri zinaweza kutofautiana. Nyama fulani zenye ziliuzishwa mu soko zilikuwa zimetumiwa mu ibada ya uongo na kutolewa kwa sanamu. (1 Wakorinto 10:25) Paulo hakuwaza kama ilikuwa mubaya kuuza na kula nyama hizo. Kwake, chakula chote kilitoka kwa Yehova. Lakini ndugu fulani wenye zamani walikuwa wanaabudu sanamu waliona mambo kwa njia tofauti. Waliona kama ilikuwa mubaya kula nyama hizo. Je, Paulo alifikiri: ‘Hilo halisumbue zamiri yangu. Niko na haki ya kula chochote chenye ninapenda?’

15 Paulo hakufikiri vile. Namna ndugu zake walijisikia ilikuwa jambo la maana sana hivi kwamba alikuwa tayari kuacha haki zake fulani. Paulo alisema kama hatupaswe ‘kujipendeza wenyewe.’ Aliongeza hivi: “Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe.” (Waroma 15:1, 3) Kama Yesu, Paulo alihangaikia sana watu wengine kuliko kujihangaikia yeye mwenyewe.​—Soma 1 Wakorinto 8:13; 10:23, 24, 31-33.

16. Juu ya nini hatupaswe kuhukumu ndugu yetu juu ya jambo lenye zamiri yake inamuruhusu kufanya?

16 Lakini namna gani ikiwa zamiri ya mutu mwingine inamuruhusu kufanya jambo fulani lenye sisi tunaona kuwa la mubaya? Tunapaswa kuwa waangalifu ili tusimulaumu na kuendelea kusema kuwa tuko na haki na kuwa yeye njo iko na makosa. (Soma Waroma 14:10.) Yehova alitupatia zamiri ili tujihukumu, hapana ili tuhukumu watu wengine. (Matayo 7:1) Tusiache hata kidogo maamuzi yetu ilete migawanyiko mu kutaniko. Lakini, tutafute njia mbalimbali za kuendeleza upendo na umoja.​—Waroma 14:19.

KUWA NA ZAMIRI YA MUZURI KUNAWEZA KUTULETEA FAIDA

17. Zamiri ya watu fulani imefikia kuwa namna gani?

17 Mutume Petro aliandika hivi: “Muendelee kuwa na zamiri ya muzuri.” (1 Petro 3:16) Jambo la kuhuzunisha ni kuwa, wakati watu wanaendelea kuzarau kanuni za Yehova, mwishowe zamiri yao haiwaonye tena ao kuwaonyesha hatari. Paulo alisema kama zamiri kama hiyo imekuwa kama “kovu lenye lilifanywa kwa chuma cha moto cha kutilia alama.” (1 Timoteo 4:2) Umekwisha kuunguzwa mubaya sana na moto? Wakati jambo hilo linatokea, ngozi yako inakuwa yenye kovu sana hivi kwamba hauwezi kusikia kitu chochote ku ile kovu. Ikiwa mutu anaendelea kufanya mambo ya mubaya, zamiri yake inaweza kuwa kama “kovu” na inaweza kufikia kuacha kutumika.

Zamiri ya muzuri inaweza kutuongoza mu maisha na kutuletea furaha na amani ya akili

18, 19. (a) Kujilaumu na kusikia haya kunaweza kutuletea faida gani? (b) Tunaweza kufanya nini ikiwa tunajilaumu juu ya zambi zenye tumekwisha kutubu?

18 Wakati tunajilaumu, zamiri yetu inaweza kuwa iko inatuambia kama tumefanya jambo fulani la mubaya. Ile inaweza kutusaidia kujua mambo yenye tulifanya na kuacha kuifanya tena. Tunapenda kujifunza kutokana na makosa yetu ili tusiirudilie tena. Kwa mufano, hata kama Mufalme Daudi alifanya zambi, zamiri yake ilimuchochea atubu. Alichukia mambo yenye alikuwa amefanya na aliazimia kumutii Yehova wakati wenye ungekuja. Kupitia mambo yenye alijionea yeye mwenyewe, Daudi angeweza kusema kama Yehova ni ‘mwema na iko tayari kusamehe.’​—Zaburi 51:1-19; 86:5; ona Mafasirio Ingine ya 7.

19 Lakini muda murefu kisha mutu kutubu zambi yake, moyo wake unaweza kuendelea kumulaumu juu ya mambo yenye alifanya. Kujilaumu kunaweza kuumiza na kunaweza kufanya mutu ajione kuwa wa bure. Ikiwa unajisikia vile wakati fulani, kumbuka kama hauwezi kubadilisha mambo yenye ilitokea zamani. Ikuwe wakati huo ulijua ao hapana mambo yenye ulipaswa kufanya na mambo yenye haukupaswa kufanya, Yehova alikusamehe kabisa, na zambi hizo zilifutwa. Uko safi mbele ya Yehova na ujue kama kwa sasa unafanya mambo yenye kuwa sawa. Moyo wako unaweza kuwa ungali unakuhukumu, lakini Biblia inasema hivi: “Mungu ni mukubwa kuliko mioyo yetu.” (Soma 1 Yohana 3:19, 20.) Ni kusema, upendo na musamaha wake ni vyenye nguvu zaidi kuliko hisia za kujihukumu ao haya yenye mutu anaweza kuwa nayo. Unaweza kuwa hakika kama Yehova amekusamehe. Wakati mutu anakubali kuwa Yehova amemusamehe, zamiri yake itakuwa na amani na anaweza kumutumikia Mungu kwa furaha.​—1 Wakorinto 6:11; Waebrania 10:22.

20, 21. (a) Kitabu hiki kimetayarishwa ili kukusaidia ufanye nini? (b) Ni uhuru gani Yehova ametupatia? Tunapaswa kuutumia namna gani?

20 Kitabu hiki kimetayarishwa ili kukusaidia kuzoeza zamiri yako ili ikuonye na kukulinda mu siku hizi zenye kuwa ngumu. Kitakusaidia pia kutumikisha kanuni za Biblia mu hali mbalimbali za maisha yako. Ni kweli kwamba, kitabu hiki hakitatupatia oroza ao liste ya sheria kuhusu mambo yenye tunapaswa kufanya mu kila hali. Tunaishi kulingana na “sheria ya Kristo,” yenye inategemea kanuni za Mungu. (Wagalatia 6:2) Kujua kama hakuna sheria yenye kuwa wazi juu ya jambo fulani hakutupatie haki ya kufanya mambo ya mubaya. (2 Wakorinto 4:1, 2; Waebrania 4:13; 1 Petro 2:16) Lakini, tunatumia uhuru wetu ili kuonyesha kama tunamupenda Yehova.

21 Wakati tunafikiri sana juu ya kanuni za Biblia na kuzitumikisha, tunajifunza kutumia ‘nguvu zetu za utambuzi’ na tutafikiri kama vile Yehova anafikiri. (Waebrania 5:14) Matokeo ni kwamba tutakuwa na zamiri yenye kuzoezwa yenye itatuongoza mu maisha na kutusaidia tubakie katika upendo wa Mungu.

^ fu. 11 Wanganga wengi wanasema kama, kunywa kwa kiasi ni nguvu zaidi kwa wale wenye wanazoea kulewa. Wanganga wanasema kama watu kama hao hawapaswe kunywa pombe hata kidogo.