Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mafasirio Ingine

Mafasirio Ingine

 1 KANUNI

Sheria za Mungu zinategemea kanuni zake. Kanuni hizo ni kweli za musingi zenye kupatikana mu Biblia. Zinatusaidia kuelewa namna Mungu anawaza na namna anaona mambo. Kanuni zinatusaidia kukamata maamuzi ya muzuri mu maisha na kufanya mambo yenye kuwa sawa. Ni za maana zaidi sana mu hali zenye hakuna kabisa sheria za Mungu zenye kuwa wazi.

Sura ya 1, fungu la 8

 2 KUTII

Kumutii Yehova kunamaanisha kuwa tayari kufanya mambo yenye anatuambia tufanye. Yehova anapenda tumutii kwa sababu tunamupenda. (1 Yohana 5:3) Kama tunamupenda na kumutumainia Mungu, tutafuata mashauri yenye anatutolea mu hali zote. Tutamutii hata wakati ni nguvu kwetu kufanya vile. Ni jambo la muzuri kwetu kumutii Yehova, juu anatufundisha namna ya kuwa na maisha ya muzuri leo na anatuahidi kama tutapata baraka mingi wakati wenye kuja.​—Isaya 48:17.

Sura ya 1, fungu la 10

 3 UHURU WA KUCHAGUA

Yehova amemupatia kila mutu uhuru wa kuchagua, ao uwezo wa kukamata maamuzi. Hakutuumba ili tukuwe kama mashine. (Kumbukumbu la Torati 30:19; Yoshua 24:15) Tunaweza kutumia uhuru wetu ili kukamata maamuzi ya muzuri. Lakini kama hatuko waangalifu, tunaweza kukamata maamuzi yenye haiko ya hekima. Kuwa na uhuru wa kuchagua kunamaanisha kama tunapaswa kuamua kipekee ikiwa tutakuwa washikamanifu kwa Yehova na kuonyesha kama tunamupenda kabisa.

Sura ya 1, fungu la 12

 4 KANUNI ZA MWENENDO

Yehova anaweka kanuni za mwenendo, ao miongozo kwa ajili ya mwenendo na matendo yetu. Katika Biblia, tunaweza kujifunza kanuni hizo na namna zinaweza kutusaidia kuishi maisha ya muzuri. (Mezali 6:16-19; 1 Wakorinto 6:9-11) Ile miongozo inatusaidia kujua ni mambo gani yenye Mungu anaona kuwa ya muzuri na yenye anaona kuwa ya mubaya. Inatusaidia pia kujua namna ya kuonyesha upendo, namna ya kukamata maamuzi ya muzuri, na namna ya kutendea wengine mu njia ya muzuri. Hata kama kanuni za ulimwengu zinaendelea kushuka, kanuni za Yehova hazibadilike. (Kumbukumbu la Torati 32:4-6; Malaki 3:6) Kuzifuata kunatulinda ili tusipatwe na hatari kubwa, ya kimwili na ya moyoni.

Sura ya 1, fungu la 17

 5 ZAMIRI

Zamiri ni uwezo wenye kuwa ndani yetu wenye unatusaidia kujua mambo ya muzuri na mambo ya mubaya. Yehova amemupatia kila mumoja wetu zamiri. (Waroma 2:14, 15) Ili zamiri yetu itumike muzuri, tunapaswa kuizoeza kulingana na kanuni za Yehova za mwenendo. Kisha zamiri yetu inaweza kutusaidia kukamata maamuzi yenye kumufurahisha Mungu. (1 Petro 3:16) Zamiri yetu inaweza kutuonya wakati tunakuwa karibu kukamata uamuzi wa kipumbavu, ao inaweza kufanya tuumie sana kisha kufanya jambo fulani la mubaya. Zamiri yetu inaweza kuwa zaifu, lakini kupitia musaada wa Yehova, tunaweza kuifanya ikuwe tena nguvu. Zamiri ya muzuri inatupatia amani ya akili na inafanya tujiheshimie.

Sura ya 2, fungu la 3

 6 KUMUOGOPA MUNGU

Kumuogopa Mungu kunamaanisha kumupenda na kumuheshimia sana hivi kwamba tunaepuka kufanya jambo lolote lenye linaweza kumuchukiza. Kumuogopa Mungu kunatusaidia kufanya mambo ya muzuri na kuepuka kufanya mambo ya mubaya. (Zaburi 111:10) Kunatuchochea kusikiliza kwa uangalifu kila jambo lenye Yehova anasema. Kunatusaidia pia kutimiza ahadi zetu kwake juu tunamuheshimia kabisa. Kumuogopa Mungu kuko na matokeo juu ya namna yetu ya kufikiri, ya kutendea wengine, na juu ya maamuzi yenye tunakamata kila siku.

Sura ya 2, fungu la 9

 7 KUTUBU

Kutubu kunatia ndani huzuni kubwa yenye mutu anasikia kwa sababu alifanya jambo fulani la mubaya. Wale wenye kumupenda Mungu wanahuzunika sana wakati wanatambua kama walifanya jambo fulani lenye linapingana na kanuni zake. Kama tunafanya jambo fulani la mubaya, tunapaswa kumuomba Yehova atusamehe kwa musingi wa bei ya ukombozi ya Yesu. (Matayo 26:28; 1 Yohana 2:1, 2) Wakati tunatubu kikweli na tunaacha kufanya jambo la mubaya, tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatusamehe. Hatuna tena sababu ya kujihukumu juu ya mambo yenye tulifanya zamani. (Zaburi 103:10-14; 1 Yohana 1:9; 3:19-22) Tunapaswa kujikaza sana ili kujifunza kutokana na makosa yetu, kubadilisha mawazo yoyote ya mubaya, na kuishi kulingana na kanuni za Yehova.

Sura ya 2, fungu la 18

 8 KUTENGWA NA KUTANIKO

Wakati mutu fulani mwenye alifanya zambi nzito hatubu na anakataa kufuata kanuni za Yehova, hawezi tena kuwa mushiriki wa kutaniko. Anapaswa kutengwa na kutaniko. Wakati mutu fulani anatengwa na kutaniko, tunaacha kupitisha wakati pamoja naye na tunaacha kuongea naye. (1 Wakorinto 5:11; 2 Yohana 9-11) Mupango wa kutengwa na kutaniko unafanya jina la Yehova na kutaniko visichafuliwe. (1 Wakorinto 5:6) Pia, kutengwa na kutaniko ni nizamu yenye inaweza kusaidia mutu atubu ili amurudilie Yehova.​—Luka 15:17.

Sura ya 3, fungu la 19

 9 MUONGOZO, MAAGIZO, NA MASHAURI

Yehova anatupenda na anapenda kutusaidia. Njo maana anatupatia muongozo, maagizo, na mashauri kupitia Biblia na kupitia watu wenye kumupenda. Kwa kuwa tuko wanadamu wenye hawakamilike, tuko na lazima kabisa ya musaada huo. (Yeremia 17:9) Wakati tunasikiliza kwa heshima wale wenye Yehova anatumia ili kutuongoza, tunaonyesha kama tunamuheshimia na kama tunapenda kumutii.​—Waebrania 13:7.

Sura ya 4, fungu la 2

 10 KIBURI NA UNYENYEKEVU

Kwa kuwa hatukamilike, ni mwepesi kwetu kujipenda sisi wenyewe na kuwa wenye kiburi. Lakini Yehova anapenda tukuwe wanyenyekevu. Mara mingi, tunajifunza unyenyekevu wakati tunajilinganisha na Yehova na kutambua kuwa tuko wa hali ya chini sana. (Yobu 38:1-4) Njia ingine ya maana ya kuwa wanyenyekevu ni kujifunza kufikiria zaidi watu wengine na kufikiria zaidi faida zao kuliko faida zetu sisi wenyewe. Mara mingi kiburi kinafanya mutu aamini kuwa ni wa muzuri zaidi kuliko wengine. Mutu munyenyekevu anajichunguza kikweli na anatambua sifa zake za muzuri na pia uzaifu wake. Haogope kukubali makosa yake, kuomba musamaha, na kukubali mawazo na mashauri ya wengine. Mutu munyenyekevu anamutegemea Yehova na anafuata muongozo wake.​—1 Petro 5:5.

Sura ya 4, fungu la 4

 11 MAMLAKA

Mamlaka ni haki ya kutoa amri na kukamata maamuzi. Ni Yehova peke yake njo iko na mamlaka ya juu zaidi mbinguni na duniani. Kwa kuwa aliumba vitu vyote, yeye njo Mutu mwenye kuwa na nguvu zaidi mu ulimwengu wote. Sikuzote anatumia mamlaka yake kwa faida ya wengine. Yehova amepatia wanadamu fulani daraka la kutuhangaikia. Kwa mufano, wazazi, wazee wa kutaniko, na wakubwa wa serikali wako na mamlaka fulani, na Yehova anapenda tuwatii. (Waroma 13:1-5; 1 Timoteo 5:17) Lakini wakati sheria za mwanadamu zinapingana na sheria za Mungu, tunamutii Mungu kuliko wanadamu. (Matendo 5:29) Wakati tunakubali mamlaka ya watu wenye Yehova anatumia, tunaonyesha kuwa tunaheshimia maamuzi ya Yehova.

Sura ya 4, fungu la 7

 12 WAZEE

Yehova anatumia wazee, ni kusema, ndugu wenye kuwa na uzoefu, ili kuhangaikia kutaniko. (Kumbukumbu la Torati 1:13; Matendo 20:28) Wanaume hao wanatusaidia ili tuendelee kuwa na uhusiano wenye nguvu pamoja na Yehova na kumuabudu mu njia ya amani na yenye kupangwa muzuri. (1 Wakorinto 14:33, 40) Ili wazee wawekwe na roho takatifu, wanapaswa kutimiza sifa zenye kuombwa zenye kupatikana mu Biblia. (1 Timoteo 3:1-7; Tito 1:5-9; 1 Petro 5:2, 3) Tunatumainia na kuunga mukono tengenezo la Mungu, kwa hiyo, tunawatii wazee kwa furaha.​—Zaburi 138:6; Waebrania 13:17.

Sura ya 4, fungu la 8

 13 KICHWA CHA FAMILIA

Yehova amepatia wazazi daraka la kuhangaikia watoto wao na watu wa nyumba yao. Lakini, Biblia inafasiria kama bwana njo kichwa cha familia. Kama baba haiko ku nyumba, mama njo anakuwa kichwa cha familia. Daraka mbalimbali za kichwa cha familia zinatia ndani kutolea familia chakula, nguo, na mahali pa kuishi. Ni jambo la maana sana kichwa cha familia akuwe wa kwanza kusaidia watu wa familia yake kumuabudu Yehova. Kwa mufano, anahakikisha kama wanaenda ku mikutano, wanahubiri, na wanajifunza Biblia pamoja kwa ukawaida. Pia, kichwa cha familia anakamata uamuzi wa mwisho. Sikuzote anajikaza kumuiga Yesu kwa kuwa mupole na mwenye usawaziko, hatende hata kidogo kwa ukali ao kwa jeuri. Ile inafanya mu familia mukuwe hali yenye upendo na inasaidia watu wote mu familia wajisikie salama na wafanye maendeleo katika uhusiano wao pamoja na Yehova.

Sura ya 4, fungu la 12

 14 BARAZA LENYE KUONGOZA

Baraza Lenye Kuongoza ni kikundi cha wanaume wenye kuwa na tumaini la kuenda mbinguni wenye wanatumiwa na Mungu ili kuongoza kazi ya watu wake. Mu karne ya kwanza, Yehova alitumia baraza lenye kuongoza ili kuongoza kutaniko la kwanza-kwanza katika ibada yao na kazi yao ya kuhubiri. (Matendo 15:2) Leo, kikundi cha ndugu wenye kutumika kama Baraza Lenye Kuongoza njo wenye kutoa maagizo, kuongoza, na kulinda watu wa Mungu. Wakati ndugu hao wanakamata maamuzi, wanategemea muongozo wa Neno la Mungu na wa roho yake takatifu. Yesu alizungumuzia kikundi hicho cha wanaume watiwa-mafuta kuwa “mutumwa muaminifu na mwenye busara.”​—Matayo 24:45-47.

Sura ya 4, fungu la 15

 15 KUFUNIKA KICHWA

Wakati fulani dada anaweza kuombwa afanye kazi fulani mu kutaniko yenye kwa kawaida inafanywa na ndugu. Wakati anafanya ile kazi, anaonyesha kama anaheshimia mupango wa Mungu kwa kuvaa kitu fulani ili kufunika kichwa. Lakini iko tu na lazima ya kufunika kichwa chake katika hali fulani. Kwa mufano, dada anaweza kuvaa kitu fulani ili kufunika kichwa chake ikiwa anaongoza funzo la Biblia wakati bwana yake ao ndugu mwenye kubatizwa iko pale.​—1 Wakorinto 11:11-15.

Sura ya 4, fungu la 17

 16 KUEPUKA KUUNGA MUKONO UPANDE WOWOTE

Tunaepuka kuunga mukono upande wowote wakati tunakataa kuwa upande fulani mu mambo ya politike. (Yohana 17:16) Watu wa Yehova wanaunga mukono Ufalme wake. Tunaepuka kuunga mukono upande wowote mu mambo ya ulimwengu, kama vile Yesu alifanya.

Yehova anatuomba ‘tutii serikali na mamlaka.’ (Tito 3:1, 2; Waroma 13:1-7) Lakini sheria ya Mungu inasema pia kama hatupaswe kuua. Kwa hiyo, zamiri ya Mukristo haiwezi kumuruhusu aende ku vita. Ikiwa Mukristo anapewa nafasi ya kufanya kazi ya kiraia pa nafasi ya kazi ya kijeshi, anapaswa kufikiria kama zamiri yake inamuruhusu kufanya vile.

Tunamuabudu tu Yehova, juu yeye njo Muumbaji wetu. Hata kama tunaheshimia alama za taifa, hatuwezi kusalimia bendera (drapeau) ao kuimba wimbo wa taifa. (Isaya 43:11; Danieli 3:1-30; 1 Wakorinto 10:14) Pia, watu wa Mungu wanaamua kipekee kukataa kuchagua chama ao mutu yeyote wa politike. Ile ni juu tayari tumekwisha kuchagua kuwa upande wa serikali ya Mungu.​—Matayo 22:21; Yohana 15:19; 18:36.

Sura ya 5, fungu la 2

 17 ROHO YA ULIMWENGU

Ulimwengu unachochea namna ya Shetani ya kufikiri. Ile namna ya kufikiri inaenea sana kati ya watu wenye hawamupendi Yehova na hawapendi kumuiga na wenye wanazarau kanuni zake. (1 Yohana 5:19) Mawazo ya vile na matendo yenye kuchochewa nayo inaitwa roho ya ulimwengu. (Waefeso 2:2) Watu wa Yehova wanahakikisha kuwa wanakataa kuruhusu ile roho iwatawale. (Waefeso 6:10-18) Kwa upande mwingine, tunapenda njia za Yehova na tunajikaza sana kushikamana na namna yake ya kufikiri.

Sura ya 5, fungu la 7

 18 UASI-IMANI

Uasi-imani ni kupinga kweli ya Biblia. Waasi-imani wanamupinga Yehova na pia Yesu, Mufalme mwenye alichaguliwa wa Ufalme wa Mungu, na wanajaribu kuchochea wengine wajiunge pamoja nao. (Waroma 1:25) Wanapenda kutia mashaka mu akili ya wale wenye kumuabudu Yehova. Watu fulani mu kutaniko la Kikristo la kwanza-kwanza waligeuka kuwa waasi-imani, na ni vile pia wamoja leo. (2 Watesalonike 2:3) Wale wenye kuwa washikamanifu kwa Yehova wanakataa kabisa kuunga mukono waasi-imani. Hatupaswe hata kidogo kuruhusu tamaa ya kujua vile mambo iko ao mikazo ya watu wengine ituchochee tusome, ao kusikiliza mawazo ya waasi-imani. Tuko washikamanifu kwa Yehova na ni yeye tu njo tunaabudu.

Sura ya 5, fungu la 9

 19 KUFUNIKA ZAMBI

Chini ya Sheria ya Musa, watu wa taifa la Israeli, walimuomba Yehova asamehe zambi zao. Walipeleka zabihu za kufunika zambi ku hekalu; zabihu za nafaka, mafuta, na za wanyama. Kwa kufanya vile, walikumbushwa kama Yehova alikuwa tayari kusamehe zambi zao wakiwa taifa ao mutu mumoja-mumoja. Mwishowe, kisha Yesu kutoa uzima wake ili kufunika zambi zetu, zile zabihu za kufunika zambi hazikukuwa tena za lazima. Yesu alitoa zabihu yenye kuwa kamilifu “mara moja kwa wakati wote.”​—Waebrania 10:1, 4, 10.

Sura ya 7, fungu la 6

 20 KUHESHIMIA UZIMA WA WANYAMA

Chini ya Sheria ya Musa, watu waliruhusiwa kutumia wanyama kwa ajili ya chakula. Waliambiwa pia watoe zabihu za wanyama. (Mambo ya Walawi 1:5, 6) Lakini Yehova hakuruhusu hata kidogo watu wake watendee wanyama kwa ukali. (Mezali 12:10) Kwa kweli, Sheria ilikuwa na maagizo yenye ililinda wanyama wasitendewe kwa ukali. Waisraeli waliombwa wahangaikie muzuri wanyama wao.​—Kumbukumbu la Torati 22:6, 7.

Sura ya 7, fungu la 6

 21 VISEHEMU VYA DAMU NA UFUNDI MBALIMBALI WA KUTUNZA

Visehemu vya damu. Damu inafanyizwa na sehemu ine kubwa​—chembe nyekundu (globules rouges), chembe nyeupe (globules blancs), vigandisha-damu (plaquettes), na plasma. Zile sehemu ine kubwa za damu zinaweza kugawanywa katika sehemu kidogo-kidogo sana, zenye kuitwa visehemu vya damu. *

Wakristo wanakataa kutiwa mu mishipa damu yote nzima ao sehemu moja kati ya sehemu ine kubwa za damu. Lakini, wanapaswa kukubali visehemu vya damu? Biblia haizungumuzie waziwazi jambo hilo. Kwa hiyo, kila Mukristo anapaswa kukamata uamuzi wake mwenyewe wenye kutegemea zamiri yake yenye kuzoezwa na Biblia.

Wakristo fulani wanachagua kukataa visehemu vyote vya damu. Wanaweza kuwaza kama Sheria ya Mungu kwa Waisraeli iliomba damu yoyote yenye ilitoshwa mu munyama imwangwe “kwenye udongo.”​—Kumbukumbu la Torati 12:22-24.

Wengine wanaamua kwa njia tofauti. Zamiri yao inawaruhusu wakubali visehemu fulani vya damu. Wanaweza kuwaza kama visehemu vidogo vya damu havimaanishe tena uzima wa kiumbe mwenye damu ilitoka.

Wakati unakamata maamuzi kuhusu visehemu vya damu, ufikirie maulizo yenye kufuata:

  • Ninajua kama kukataa visehemu vyote vya damu kunamaanisha kama sitakubali dawa fulani zenye zinapiganisha magonjwa ao zenye zinaweza kuzuia damu kuvuja?

  • Namna gani ninaweza kufasiria munganga sababu yenye inanifanya nikatae ao kukubali kisehemu kimoja cha damu ao zaidi?

Ufundi mbalimbali wa kutunza. Sisi Wakristo, hatutolee watu damu, ao kuweka damu yetu wenyewe majuma fulani mbele ya kufanyiwa upasuaji. Lakini, kuko ufundi mwingine wa kutunza wenye unatumia damu ya mugonjwa. Kila Mukristo anapaswa kuamua yeye mwenyewe namna damu yake itatumiwa wakati wa upasuaji, wakati wa kupimwa damu, ao wakati wa matunzo yenye kutumiwa wakati huo. Wakati wa ufundi kama huo, damu ya mugonjwa inaweza kutenganishwa kabisa na mugonjwa kwa muda fulani.​—Ili kupata maelezo zaidi, ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 10, 2000, ukurasa wa 30-31.

Kwa mufano, kuko ufundi fulani wenye kuitwa hémodilution, wenye mbele tu ya upasuaji, sehemu fulani ya damu ya mugonjwa inatoshwa mu mwili wake na umajimaji fulani unaingizwa ndani ya mwili ili kukamata nafasi ya damu yenye ilitoshwa. Kisha, wakati wa upasuaji ao muda mufupi kisha upasuaji, ile damu inarudishwa tena ndani ya mwili wa mugonjwa.

Ufundi mwingine unaitwa récupération du sang épanché ao kuokoa chembe za damu. Wakati wa ufundi huo, damu ya mugonjwa yenye inavuja wakati wa upasuaji, inakusanywa, inasafishwa na kisha inarudishwa mu mwili wa mugonjwa wakati wa upasuaji ao muda mufupi kisha upasuaji.

Kila munganga anaweza kutumia ule ufundi kwa njia yenye kuwa tofauti kidogo. Kwa hiyo, mbele ya kukubali ufundi wowote wa upasuaji, kukubali kupimwa damu, ao matunzo yenye kutumiwa wakati huo, Mukristo anapaswa kujua kabisa namna damu yake itatumiwa.

Wakati unakamata maamuzi kuhusu ufundi wenye unaomba kutumia damu yako mwenyewe, ufikirie maulizo yenye kufuata:

  • Ikiwa damu yangu inatoshwa ndani ya mwili wangu na pengine iache hata kutembea kwa muda fulani, zamiri yangu itaniruhusu kuona ile damu kuwa ingali sehemu ya mwili wangu, na kwa hiyo kuiona kuwa haipaswe ‘kumwangwa kwenye udongo’?​—Kumbukumbu la Torati 12:23, 24.

  • Zamiri yangu yenye kuzoezwa na Biblia itasumbuliwa ikiwa wakati wa matunzo, sehemu ya damu yangu inatoshwa, inarekebishwa, na kurudishwa tena ndani ya mwili wangu?

  • Ninajua kama kukataa ufundi wote wa kutunza wenye kuomba kutumia damu yangu mwenyewe kunamaanisha kama sitakubali ufundi wenye kuitwa hémodialyse, kupimwa damu, ao kama sitakubali mashini yenye kufanya kazi pa nafasi ya moyo na mapafu?

Mbele ya kukamata maamuzi kuhusu visehemu vya damu na ufundi mbalimbali wa kutunza wenye kutumia damu yetu wenyewe, tunapaswa kusali ili kupata muongozo wa Yehova na kisha tunapaswa kufanya utafiti. (Yakobo 1:5, 6) Kisha kufanya vile, tunapaswa kutumia zamiri yetu yenye kuzoezwa na Biblia ili kukamata uamuzi. Hatupaswe kuuliza wengine kama wangefanya nini ikiwa wangekuwa mu hali yetu, wala hatupaswe kuruhusu wengine wachochee uamuzi wetu.​—Waroma 14:12; Wagalatia 6:5.

Sura ya 7, fungu la 11

 22 KUWA SAFI KATIKA MWENENDO

Kuwa safi katika mwenendo kunamaanisha kuwa na mwenendo na matendo yenye kuwa safi mbele ya Mungu. Kunatia ndani mambo yenye tunawaza, tunasema, na yenye tunafanya. Yehova anatuambia tuepuke aina yoyote ya uchafu wa ngono ao uasherati. (Mezali 1:10; 3:1) Tunapaswa kuamua kuwa tutafuata kanuni safi za Yehova hata mbele tukuwe mu hali yenye inaweza kutujaribu tufanye jambo fulani la mubaya. Tunapaswa kuendelea kumuomba Mungu atusaidie ili akili yetu iendelee kuwa safi, na tunapaswa kuazimia kukataa mambo yote yenye inaweza kutujaribu kufanya uasherati.​—1 Wakorinto 6:9, 10, 18; Waefeso 5:5.

Sura ya 8, fungu la 11

 23 MWENENDO MUPOTOVU WA BILA HAYA NA UCHAFU

Mwenendo mupotovu wa bila haya unatia ndani kusema na kutenda mu njia yenye kupingana kabisa na kanuni za Mungu na kuonyesha mutazamo wa bila haya. Mutu mwenye kutenda vile anaonyesha kuwa haheshimie sheria za Mungu. Wakati mutu anajiingiza mu mwenendo mupotovu wa bila haya, halmashauri ya hukumu itashugulikia jambo hilo. Uchafu unatia ndani aina mbalimbali za matendo ya mubaya. Ikitegemea uzito wa hali, matendo fulani ya uchafu inaweza kushugulikiwa na halmashauri ya hukumu katika kutaniko.​—Wagalatia 5:19-21; Waefeso 4:19; ili kupata habari zaidi, ona “Maswali kutoka kwa Wasomaji” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 7, 2006.

Sura ya 9, fungu la 7; Sura ya 12, fungu la 10

 24 KUPIGA PUNYETO

Yehova alikusudia ngono ikuwe alama ya kuonyeshana upendo kati ya bibi na bwana. Lakini wakati mutu fulani anapiga punyeto, ao anatumia mubaya viungo vyake vya uzazi ili kupata raha ya ngono, anavitumia mu njia chafu. Ile tabia inaweza kuharibisha uhusiano wa mutu pamoja na Yehova. Inaweza kufanya mutu akuwe na tamaa chafu sana na kumufanya aone ngono mu njia yenye haiko safi. (Wakolosai 3:5) Mutu mwenye iko na ile tabia chafu na anaona kama ni nguvu kuiacha hapaswe kuvunjika moyo. (Zaburi 86:5; 1 Yohana 3:20) Kama uko na ile tabia, sali kwa Yehova kwa moyo wako wote na umuombe akusaidie. Epuka mambo yenye inaweza kukufanya ukuwe na mawazo machafu, mambo kama vile pornografia. Zungumuza na mumoja wa wazazi wako Wakristo ao na rafiki yako mukomavu mwenye anaheshimia sheria za Yehova. (Mezali 1:8, 9; 1 Watesalonike 5:14; Tito 2:3-5) Unaweza kuwa hakika kama Yehova anaona na kupendezwa sana na bidii yenye unaonyesha ili kubakia safi katika mwenendo.​—Zaburi 51:17; Isaya 1:18.

Sura ya 9, fungu la 9

 25 KUWA NA BIBI WENGI

Yehova alikusudia ndoa ikuwe kati ya mwanaume mumoja na mwanamuke mumoja. Katika Israeli ya zamani, Mungu aliruhusu wanaume wakuwe na zaidi ya bibi mumoja, lakini hakukusudia vile ku mwanzo. Leo, Yehova haruhusu watu wake wakuwe na bibi ao bwana wengi. Bwana anapaswa kuwa tu na bibi mumoja na bibi anapaswa kuwa tu na bwana mumoja.​—Matayo 19:9; 1 Timoteo 3:2.

Sura ya 10, fungu la 12

 26 KUVUNJA NDOA NA KUTENGANA

Yehova alikusudia bibi na bwana wabakie pamoja maisha yao yote. (Mwanzo 2:24; Malaki 2:15, 16; Matayo 19:3-6; 1 Wakorinto 7:39) Anaruhusu kuvunja ndoa wakati bibi ao bwana anafanya uzinifu. Mu hali ya vile, Yehova anapatia bibi ao bwana mwenye hana kosa haki ya kuamua ikiwa ataomba kuvunja ndoa ao hapana.​—Matayo 19:9.

Wakati fulani, Wakristo fulani waliamua kutengana na bibi ao bwana yao hata kama hakukuwa uasherati. (1 Wakorinto 7:11) Katika hali zenye kuonyeshwa hapa chini, Mukristo anaweza kuamua kutengana na bibi ao bwana yake.

  • Kukataa kimakusudi kutegemeza familia: Bwana anakataa kuhangaikia familia kimwili, mupaka familia inabakia bila feza ao chakula.​—1 Timoteo 5:8.

  • Kutendewa mubaya sana kimwili: Bibi ao bwana anaweza kutendewa mubaya kimwili mupaka anaona kama afya ao uzima wake unakuwa mu hatari.​—Wagalatia 5:19-21.

  • Kutia kabisa mu hatari uhusiano wa mutu pamoja na Yehova: Bibi ao bwana anazuia mwenzake kumutumikia Yehova.​—Matendo 5:29.

Sura ya 11, fungu la 19

 27 KUPONGEZA NA KUTIA MOYO

Sisi wote tuko na lazima ya kupongezwa na kutiwa moyo. (Mezali 12:25; 16:24) Tunaweza kutiana nguvu na kufarijiana kupitia maneno yenye upendo na yenye neema. Maneno ya vile inaweza kusaidia ndugu na dada zetu wavumilie na waendelee kumutumikia Yehova hata kama wanapatwa na matatizo makubwa. (Mezali 12:18; Wafilipi 2:1-4) Kama mutu fulani anajisikia kuwa mwenye kuvunjika moyo sana, tunapaswa kumusikiliza kwa heshima na kujikaza kuelewa namna anajisikia. Ile inaweza kutusaidia tujue kile tunaweza kusema na kile tunaweza kufanya ili kumusaidia. (Yakobo 1:19) Ujiwekee muradi wa kujua ndugu na dada zako muzuri ili uelewe kabisa mambo yenye wako nayo lazima. Kwa kufanya vile unaweza kuwasaidia wamuendee ule mwenye kuwa Chanzo cha faraja yote na kitia-moyo, mwenye anaweza kuwapatia kitulizo cha kweli.​—2 Wakorinto 1:3, 4; 1 Watesalonike 5:11.

Sura ya 12, fungu la 16

 28 SIKU YA NDOA

Biblia haitoe sheria zenye kuwa wazi kuhusu ndoa. Desturi na mambo yenye kuombwa na sheria inatofautiana kulingana na nafasi kwenye watu wanaishi. (Mwanzo 24:67; Matayo 1:24; 25:10; Luka 14:8) Sehemu ya maana zaidi ya siku ya ndoa ni naziri yenye watu wenye wanaoana wanafanya mbele ya Yehova. Watu wengi wenye wanaoana wanapendaka kuwa na watu wa familia yao na marafiki wakati wanafanya naziri na wanapendaka muzee wa kutaniko awatolee hotuba yenye kutegemea Biblia. Ikiwa walipanga vile, ni wale wenye wanaoana njo wanaweza kuamua aina ya karamu yenye watafanya kisha kufunga ndoa. (Luka 14:28; Yohana 2:1-11) Ikuwe watakamata uamuzi gani juu ya mipango ya ndoa yao, wale wenye wanaoana wanapaswa kuhakikisha kama siku yao ya ndoa inamuletea Yehova heshima. (Mwanzo 2:18-24; Matayo 19:5, 6) Kanuni za Biblia zinaweza kuwasaidia kukamata maamuzi ya muzuri. (1 Yohana 2:16, 17) Kama wanachagua matumizi ya pombe wakati wa karamu, wanapaswa kuhakikisha kama karamu itasimamiwa mu njia yenye kufaa. (Mezali 20:1; Waefeso 5:18) Kama wanaamua muziki wowote upigwe ao kukuwe mambo ya kujifurahisha, wanapaswa kuhakikisha kama ile mambo itamuletea Yehova heshima. Wakristo wenye wanaoana wanapaswa kukaza akili juu ya uhusiano wao pamoja na Mungu na uhusiano kati yao wawili kuliko kukazia tu siku yao ya ndoa.​—Mezali 18:22; ili kupata mashauri zaidi, ona Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 10, 2006, ukurasa wa 18-31.

Sura ya 13, fungu la 18

 29 KUKAMATA MAAMUZI YENYE HEKIMA

Tunapenda kukamata maamuzi ya muzuri yenye kutegemea kanuni za Neno la Mungu. Kwa mufano, Mukristo anaweza kualikwa na bibi ao bwana yake mwenye haiko Shahidi wa Yehova wakule chakula pamoja na watu wa jamaa yake wakati wa sikukuu ya watu wa ulimwengu. Kama ungekuwa mu ile hali, ungefanya nini? Ikiwa zamiri yako inakuruhusu kuenda, unaweza kuelezea mwenzako kama ikiwa desturi za kipagani zitafanywa wakati wa kutumia chakula, hautazifanya. Unapaswa pia kufikiria ikiwa wengine watakwazika kama unaenda.​—1 Wakorinto 8:9; 10:23, 24.

Ao, inawezekana mukubwa wako wa kazi akupatie zawadi mu kipindi cha sikukuu. Je, utakataa ile zawadi? Haiko lazima uikatae. Uamuzi wako wa kukubali ao kukataa unaweza kutegemea kwa njia fulani mawazo yenye mukubwa wako wa kazi iko nayo kuhusu ile zawadi. Je, anaiona kuwa sehemu ya ile sikukuu? Ao anaiona tu kuwa njia ya kukushukuru juu ya kazi yako? Kisha kufikiria ile maulizo na mambo ingine, utakuwa na lazima ya kuamua ikiwa utakubali ile zawadi.

Katika hali ingine, mutu fulani anaweza kukupatia zawadi wakati wa kipindi cha sikukuu fulani na kusema: “Najua kama haufanyake hii sikukuu, lakini napenda ukamate hii zawadi.” Pengine ule mutu anapenda tu kukuonyesha wema. Ao, kuko sababu yenye inaweza kukufanya ufikiri kama ule mutu iko anapenda kujaribu imani yako ao kukuingiza mu ile sikukuu? Kisha kufikiria jambo hilo, ni weye njo utaamua ikiwa utakubali ao kukataa ile zawadi. Katika maamuzi yote yenye tunakamata, tunapenda kuwa na zamiri safi na kuwa waaminifu kwa Yehova.​—Matendo 23:1.

Sura ya 13, fungu la 22

 30 BIASHARA NA MAMBO YA KISHERIA

Katika hali mingi, kumaliza matatizo ya kukosa kuelewana haraka na mu njia ya amani, kunafanya matatizo kidogo isikuwe makubwa. (Matayo 5:23-26) Jambo lenye Wakristo wote wanapaswa kuhangaikia ni kumuletea Yehova utukufu na kufanya kutaniko liendelee kuwa na umoja.​—Yohana 13:34, 35; 1 Wakorinto 13:4, 5.

Kama Wakristo wanashindwa kuelewana mu mambo ya biashara, wanapaswa kujikaza kumaliza hali yao bila kupelekana ku tribinali. Andiko la 1 Wakorinto 6:1-8 linaonyesha mashauri yenye mutume Paulo aliwapatia Wakristo juu ya mashitaka ya kisheria. Kushitaki ndugu yetu ku tribinali kunaweza kuharibisha sifa ya Yehova na ya kutaniko. Andiko la Matayo 18:15-17, linaonyesha hatua tatu zenye Wakristo wanapaswa kufuata ili kumaliza matatizo makubwa kama vile kusingizia mutu ao kumuiba kwa kutumia udanganyifu. (1) Wanapaswa kwanza kujaribu kumaliza tatizo kati yao wawili. (2) Kama wanashindwa kupatana, wanaweza kuomba ndugu ao dada mumoja ao wawili wakomavu mu kutaniko ili wawasaidie. (3) Kisha, ikiwa ni lazima, wanaweza kupeleka tatizo hilo ku baraza la wazee ili walishugulikie. Kama hali inafikia kuwa vile, wazee watatumia kanuni za Biblia ili kujaribu kusaidia wote wenye kuwa mu ile hali wafikie kupatana kwa amani. Kama watu fulani kati yao wanakataa kufuata kanuni za Biblia, inaweza kuwa lazima kwa wazee wa kutaniko kufanya halmashauri ya hukumu.

Kuko hali zingine mwenye mashitaka ya kisheria inaweza kuwa ya lazima, pengine ile inaweza kutia ndani kuvunja ndoa, kuomba haki ya kuchunga watoto kisha ndoa kuvunjika, kulipwa na mwenye alivunja ndoa, kurudishiwa feza kisha benki kuhomba (ao, kuchomba), kupata malipo ya asiranse, ao kuomba testama ikubaliwe kisheria. Kama Mukristo anatumia ile njia ya kisheria ili kumaliza matatizo mu njia ya amani kadiri anaweza, hapinge mashauri ya Paulo.

Kama kukosana kunatokea kwa sababu ya hali nzito, kama vile kulalwa kinguvu, kutendea mutoto mubaya kingono, kushambuliwa, kuibiwa kitu cha bei sana, ao kuua, Mukristo mwenye anajulisha ile tendo ku mamlaka ya kisheria hapinge mashauri ya Paulo.

Sura ya 14, fungu la 14

 31 NJIA ZA SHETANI ZA KUDANGANYA

Kuanzia mu bustani ya Edeni, Shetani amekuwa akijaribu kudanganya wanadamu. (Mwanzo 3:1-6; Ufunuo 12:9) Anajua kama ikiwa anafikia kuharibisha mawazo yetu, anaweza kutuchochea tufanye mambo ya mubaya. (2 Wakorinto 4:4; Yakobo 1:14, 15) Anatumia politike, dini, biashara, mambo ya kujifurahisha, elimu, na mambo ingine ili kuendeleza njia yake ya kufikiri na anafanya ionekane kuwa ni ya muzuri.​—Yohana 14:30; 1 Yohana 5:19.

Shetani anajua kama anabakia na wakati mufupi tu wa kudanganya watu. Kwa hiyo, anafanya nguvu yake yote ili kudanganya watu wengi zaidi kadiri inawezekana. Anapenda zaidi sana kudanganya wale wenye kumutumikia Yehova. (Ufunuo 12:12) Kama hatuko waangalifu, Ibilisi anaweza kuharibu akili yetu pole kwa pole. (1 Wakorinto 10:12) Kwa mufano, Yehova anapenda ndoa idumu. (Matayo 19:5, 6, 9) Lakini leo, watu wengi wanaona ndoa kuwa mapatano fulani tu yenye ni mwepesi kuvunja. Filme mingi na programu za televizyo zinachochea pia ile mawazo. Tunapaswa kuhakikisha kuwa tunakataa kuruhusu mawazo ya ulimwengu kuhusu ndoa ituchochee.

Njia ingine yenye Shetani anatumia ili kutudanganya ni kuchochea roho ya kupenda kujitegemea. (2 Timoteo 3:4) Kama hatuko waangalifu, tunaweza kukosa kuheshimia mamlaka ya watu wenye Yehova amechagua. Kwa mufano, ndugu fulani anaweza kuanza kupinga muongozo wa wazee wa kutaniko. (Waebrania 12:5) Ao dada anaweza kuanza kupinga mupango wenye Yehova ameweka mu familia kuhusu ukichwa.​—1 Wakorinto 11:3.

Tunapaswa kuazimia kukataa kuruhusu Shetani achochee mawazo yetu. Kwa upande mwingine, tunapenda kuiga namna ya Yehova ya kufikiri na kuendelea “kukaza akili [zetu] juu ya mambo yenye kuwa juu.”​—Wakolosai 3:2; 2 Wakorinto 2:11.

Sura ya 16, fungu la 9

 32 MATUNZO

Sisi wote tunapenda kuwa na afya ya muzuri na kupata matunzo ya muzuri zaidi wakati tunagonjwa. (Isaya 38:21; Marko 5:25, 26; Luka 10:34) Leo, kuko ufundi mwingi wa kutunza na dawa mbalimbali zenye wanganga na watu wengine wanatumia. Wakati tunaamua ni matunzo gani yenye tutakubali, ni jambo la maana tufuate kanuni za Biblia. Tunakumbuka kama ni Ufalme wa Mungu tu njo utaponyesha magonjwa yetu milele. Hatupendi kukaza sana akili juu ya afya yetu mupaka tufikie kuzarau ibada yetu kwa Yehova.​—Isaya 33:24; 1 Timoteo 4:16.

Tunapaswa kuepuka kwa uangalifu matunzo yoyote yenye inaonekana kuwa inatumia nguvu za pepo wachafu. (Kumbukumbu la Torati 18:10-12; Isaya 1:13) Kwa hiyo, mbele tukubali dawa fulani ao matunzo yoyote, tunapaswa kufanya nguvu yetu yote ili kujua ile matunzo inatokana na nini na inaendeleza mawazo gani. (Mezali 14:15) Hatupaswe kusahau kama Shetani anapenda kutudanganya ili tuingie mu mambo yenye kuwa na uhusiano na pepo wachafu. Ikiwa tunakuwa hata na mashaka kama matunzo fulani iko na uhusiano na pepo wachafu, ni muzuri zaidi kuikataa.​—1 Petro 5:8.

Sura ya 16, fungu la 18

^ fu. 98 Wanganga fulani wanaweza kuona zile sehemu ine kubwa za damu kuwa visehemu vya damu. Kwa hiyo, unaweza kuwa na lazima ya kufasiria uamuzi wako wa kipekee wa kukataa kutiwa mu mishipa damu yote nzima ao sehemu zake ine kubwa, ni kusema, chembe nyekundu, chembe nyeupe, vigandisha-damu, na plasma.