Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 11

Maisha ya Kisha Siku ya Ndoa

Maisha ya Kisha Siku ya Ndoa

“Upendo haushindwe hata kidogo.”​—1 WAKORINTO 13:8.

1, 2. Kuwa na magumu mu ndoa inamaanisha kama imeshindwa? Fasiria.

NDOA ni zawadi kutoka kwa Yehova. Inaweza kufanya maisha ya mutu ikuwe yenye furaha zaidi. Lakini, kila ndoa inakuwaka na magumu. Inaweza hata kuonekana kama magumu haitaishaka, na bibi na bwana wanaweza kujisikia kama hawana tena uhusiano wa karibu kama zamani.

2 Hatupaswe kushangaa ikiwa ndoa yetu inakuwa na magumu wakati fulani. Lakini, kuwa na magumu mu ndoa hakumaanishe kama imeshindwa. Hata bibi na bwana wenye walikuwa na magumu makubwa sana walipata njia za kutengeneza tena uhusiano wao na kufanya ndoa yao ikuwe yenye nguvu zaidi. Namna gani?

MUMUKARIBIE MUNGU ZAIDI NA MUKUWE NA UHUSIANO WA KARIBU KATI YENU

3, 4. Ni nini inaweza kutokea mu ndoa wakati fulani?

3 Ndoa inaunganisha watu wawili wenye kuwa tofauti, wenye kila mutu iko na mambo yenye anapendaka na yenye anachukiaka, mawazo, na namna tofauti ya kufanya mambo. Pia, bibi na bwana wanaweza kuwa walikomalia mahali tofauti ao kutoka katika desturi tofauti. Inaomba wakati na kujikaza ili bibi na bwana wafikie kujuana na kuelewana muzuri.

4 Kadiri wakati unapita, bibi ao bwana anaweza kuanza kuhangaikia mambo yake mwenyewe na ile inaweza kufanya ajitenge na mwenzake. Inaweza kuonekana kama vile kila mutu iko anaishi maisha yake. Ni nini inaweza kuwasaidia wakuwe na uhusiano wa karibu zaidi?

Mashauri ya Biblia ni ya maana ili ndoa ikuwe muzuri

5. (a) Ni nini inaweza kusaidia Mukristo akuwe na uhusiano wa karibu zaidi pamoja na bibi ao bwana yake? (b) Kulingana na Waebrania 13:4, namna gani tunapaswa kuona ndoa?

5 Yehova anatoa mashauri ya muzuri yenye inaweza kukusaidia wewe na bibi ao bwana yako mumukaribie na mukuwe na uhusiano wa karibu kati yenu. (Zaburi 25:4; Isaya 48:17, 18) Anatuambia hivi: “Ndoa iheshimiwe kati ya watu wote.” (Waebrania 13:4) Kitu fulani chenye unaheshimia unakiona kuwa cha bei na cha maana. Unakilinda na unakikamata kwa uzito. Ni vile Yehova anapenda tuone ndoa.

KUMUPENDA YEHOVA KUNAWEZA KUSAIDIA NDOA YENU

6. Kulingana na Matayo 19:4-6, Yehova anaona ndoa namna gani?

6 Yehova njo mwenye alianzisha ndoa ya kwanza. Mwana wake, Yesu, alisema hivi: “Je, hamukusoma kama ule mwenye aliwaumba tangu mwanzo aliwafanya mwanaume na mwanamuke na alisema: ‘Kwa sababu hiyo mwanaume atamuacha baba yake na mama yake na atashikamana na bibi yake, na hao wawili watakuwa mwili mumoja’? Na hivyo hawako wawili tena, lakini mwili mumoja. Kwa hiyo, kile chenye Mungu ameunganisha, mutu yeyote asikitenganishe.” (Matayo 19:4-6) Kuanzia mwanzo, Yehova alikusudia ndoa ikuwe mupango wenye kuendelea. Alipenda watu wa familia wakuwe na uhusiano wa karibu, wakuwe wenye furaha, na wafurahie maisha pamoja.

7. Bibi na bwana wanaweza kufanya nini ili ndoa yao ikuwe yenye nguvu?

7 Lakini leo, watu wenye kuoana wanapambana na mahangaiko na mikazo mingi zaidi kuliko wakati mwingine wowote. Wakati fulani mikazo ni yenye nguvu sana na ile inafanya bibi na bwana wafikiri kama ndoa yao haiwezi kuokoka, na wanavunjika moyo. Lakini kuelewa mawazo ya Yehova juu ya ndoa kunaweza kutusaidia.​—1 Yohana 5:3.

8, 9. (a) Ni wakati gani tunapaswa kufuata muongozo wa Yehova juu ya ndoa? (b) Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaona ndoa yetu kuwa ya maana?

8 Muongozo wa Yehova ni wenye faida kwetu sikuzote. Kama vile tumeona, Yehova anatushauria hivi: “Ndoa iheshimiwe kati ya watu wote.” (Waebrania 13:4; Muhubiri 5:4) Ikiwa tunafuata muongozo wa Yehova hata wakati ni nguvu kufanya vile, tutapata faida kabisa.​—1 Watesalonike 1:3; Waebrania 6:10.

9 Kwa kuwa tunaona ndoa yetu kuwa ya maana, tunaepuka kufanya ao kusema jambo lolote lenye linaweza kuiharibu. Lakini, tunapenda uhusiano wetu pamoja na bwana ao bibi yetu ukuwe wenye nguvu zaidi. Namna gani tunaweza kufanya vile?

HESHIMIA NDOA YAKO KUPITIA MANENO NA MATENDO

10, 11. (a) Ndoa fulani zinakuwaka na matatizo gani makubwa? (b) Juu ya nini tunapaswa kuwa waangalifu wakati tunazungumuza na bibi ao bwana yetu?

10 Mutu anaweza kuumiza bibi ao bwana yake mu njia mingi. Tunajua kama Mukristo hapaswe hata kidogo kumupiga bibi ao bwana yake, ao kufanya jambo lolote ili kumuumiza kimwili. Lakini, tunaweza kuumizana kupitia maneno yetu. Maneno inaweza kuwa silaha. Mwanamuke mumoja alisema hivi: “Bwana yangu ananipigaka kupitia maneno yake. Pengine siwezi kuwa na vidonda vyenye kuonekana, lakini kusema kila mara maneno yenye kuumiza, kama vile ‘Unanichokesha!’ na ‘Uko wa bure!’ kumefanya moyo wangu ukuwe na vidonda.” Mwanaume mumoja alisema kama bibi yake anamushushiaka heshima na kumupanga majina. Alisema hivi: “Siwezi kurudilia mbele ya watu wenye kujiheshimia mambo yenye ananiambiaka. Njo maana sizungumuzake naye na njo maana sitokake haraka ku kazi. Ni muzuri zaidi kubakia ku kazi kuliko kurudia ku nyumba.” Leo, watu wengi wanaona kutumia matusi, maneno makali na ya mubaya yenye kuumiza moyo kuwa jambo la kawaida.

11 Wakati bibi na bwana wanazungumuza pamoja kwa ukali, ile inafanya moyo ukuwe na vidonda vyenye havipone haraka. Kusema kweli, Yehova hapendi bibi na bwana watendeane vile. Lakini inawezekana kuumiza bibi ao bwana yako bila hata kujua. Unaweza kuwaza kama uko mutu muzuri mbele ya bwana ao bibi yako, lakini yeye anakuona namna gani? Kama jambo fulani lenye ulisema liliumiza bwana ao bibi yako, utakuwa tayari kubadilika?​—Wagalatia 5:15; soma Waefeso 4:31.

12. Ni nini inaweza kufanya uhusiano wa bibi ao bwana pamoja na Yehova uharibike?

12 Namna unazungumuza na bibi ao bwana yako, ikuwe muko peke yenu ao mbele ya watu, ni jambo la maana mbele ya Yehova. (Soma 1 Petro 3:7.) Yakobo 1:26 inatukumbusha hivi: “Kama mutu yeyote anawaza yeye ni muabudu wa Mungu lakini hazuie kabisa ulimi wake, anadanganya moyo wake mwenyewe, na ibada yake ni ya bure.”

13. Ni mu njia gani ingine mutu anaweza kuumiza bibi ao bwana yake?

13 Kuko njia zingine zenye bibi ao bwana anapaswa kuonyesha kama anahangaikia mwingine. Kwa mufano, bibi ao bwana yako anaweza kujisikia namna gani kama unaanza kupitisha wakati mingi na mutu mwingine? Unaweza kuwa na sababu ya muzuri ya kufanya vile, kama vile kuhubiri ao kusaidia mutu fulani kupambana na magumu, lakini, ile inaweza kufanya bibi ao bwana yako aumie? Bibi mumoja Mukristo alisema hivi: “Kuona kama bwana yangu anapitisha wakati mingi pamoja na dada mwingine mu kutaniko na kumuhangaikia sana kunaniumizaka. Inafanya nijione kuwa mutu wa bure.”

14. (a) Andiko la Mwanzo 2:24 linatufundisha ukweli gani wa musingi? (b) Tunapaswa kujiuliza maulizo gani?

14 Sisi Wakristo, tuko na madaraka ya kuhangaikia wazazi wetu na ndugu na dada mu kutaniko letu. Lakini, wakati tunaoa ao kuolewa, daraka letu kubwa ni kuhangaikia bibi ao bwana yetu. Yehova alisema kama bwana “atashikamana na bibi yake.” (Mwanzo 2:24) Namna bibi ao bwana yetu anajisikia inapaswa kuwa jambo la maana sana kwetu. Ujiulize hivi: ‘Je, ninapitisha wakati pamoja na bibi ao bwana yangu kama vile inapaswa? Ninamuhangaikia na kumuonyesha upendo wenye iko nao lazima na wenye anastahili?’

15. Juu ya nini Wakristo wenye kuoa ao kuolewa wanapaswa kuepuka kuwa na uhusiano wa karibu sana pamoja na mutu mwenye haiko bibi ao bwana yao?

15 Kama tunakuwa na uhusiano wa karibu sana pamoja na mutu mwenye haiko bibi ao bwana yetu, ile inaweza kuleta fujo mu ndoa yetu. Tunaweza kufikia kumupenda sana ule mutu na kuanza kumutamani. (Matayo 5:28) Ile tamaa inaweza kukomaa na kutuchochea kufanya jambo fulani lenye linaweza kushushia heshima ndoa yetu.

“KITANDA CHA NDOA KIKUWE BILA UCHAFU”

16. Biblia inatoa amri gani kuhusu ndoa?

16 Kisha kusema: “Ndoa iheshimiwe kati ya watu wote,” Biblia inasema hivi: “Kitanda cha ndoa kikuwe bila uchafu, kwa maana Mungu atahukumu waasherati na wazinifu.” (Waebrania 13:4) Katika andiko hili, “kitanda cha ndoa” kinamaanisha kitendo cha ndoa kati ya bwana na bibi. (Mezali 5:18) Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia “kitanda cha ndoa” na kama hatukichafue?

17. (a) Leo, watu wengi wanaona uzinifu namna gani? (b) Namna gani Wakristo wanapaswa kuona uzinifu?

17 Leo, watu fulani wanawaza kama hakuna ubaya wowote kukosa uaminifu kwa bibi ao bwana yao. Hatupaswe hata kidogo kuambukizwa na ile tabia. Yehova anaonyesha wazi kabisa kama anachukia uasherati na uzinifu. (Soma Waroma 12:9; Waebrania 10:31; 12:29) Kama tunafanya ngono na mutu mwenye haiko bibi ao bwana yetu, tutachafua ndoa yetu. Tutaonyesha kama hatuheshimie kanuni za Yehova, na tutaharibu uhusiano wetu pamoja naye. Kwa hiyo, tunapaswa kuepuka hata kukamata hatua ya kwanza yenye inaweza kutuongoza ku uzinifu. Ile inatia ndani kuepuka kuwa na mawazo machafu kuelekea mutu mwingine.​—Yobu 31:1.

18. (a) Juu ya nini kufanya uzinifu ilikuwa sawa na kuabudu miungu ya uongo? (b) Yehova anaona uzinifu namna gani?

18 Katika Israeli ya zamani yenye ilikuwa chini ya Sheria ya Musa, kufanya uzinifu ilikuwa zambi nzito sana, sawa tu na kuabudu miungu ya uongo. Malipizi ya zile zambi ilikuwa kifo. (Mambo ya Walawi 20:2, 10) Ni mu njia gani kufanya uzinifu ilikuwa sawasawa na kuabudu miungu ya uongo? Kama Muisraeli aliabudu miungu ya uongo, alivunja ahadi yake ya kubakia muaminifu kwa Yehova. Kwa kufanya uzinifu, alivunja ahadi yake ya kuwa muaminifu kwa bibi ao bwana yake. (Kutoka 19:5, 6; Kumbukumbu la Torati 5:9; soma Malaki 2:14.) Ni wazi kuwa, zamani, Yehova aliona uzinifu kuwa zambi nzito sana.

19. Ni nini inaweza kutusaidia tuazimie kuepuka uzinifu?

19 Tuseme nini leo? Hata kama hatuko tena chini ya Sheria ya Musa, mawazo ya Yehova juu ya uzinifu haijabadilika. Kama vile tu hatuwezi hata kidogo kuabudu mungu wa uongo, hatupaswe hata kidogo kukosa uaminifu kwa bibi ao bwana yetu. (Zaburi 51:1, 4; Wakolosai 3:5) Kama tunakosa uaminifu, tutashushia heshima ndoa yetu, na tutamushushia heshima Mungu wetu, Yehova.​—Ona Mafasirio Ingine ya 26.

NAMNA YA KUFANYA NDOA YAKO IKUWE YENYE NGUVU ZAIDI

20. Hekima inaweza kuwa na faida gani mu ndoa?

20 Namna gani unaweza kufanya ndoa yako ikuwe yenye nguvu zaidi? Neno la Mungu linasema hivi: “Nyumba inajengwa kwa hekima, na kwa utambuzi inafanywa kuwa salama.” (Mezali 24:3) Nyumba inaweza kuwa yenye baridi na bila kitu ndani ao yenye joto, ya muzuri na yenye kuwa salama. Ni vile pia kuhusu ndoa. Mutu mwenye hekima atahakikisha kama ndoa yake iko salama, ni ya muzuri na yenye kufurahisha.

21. Namna gani ujuzi unaweza kusaidia ndoa ikuwe yenye nguvu zaidi?

21 Kuhusu ile nyumba, Biblia inaendelea kusema hivi: “Kwa ujuzi vyumba vyake vinajazwa kila namna ya hazina za samani na zenye kupendeza.” (Mezali 24:4) Mambo yenye unajifunza katika Neno la Mungu inaweza kufanya ndoa yenu ikuwe muzuri zaidi. (Waroma 12:2; Wafilipi 1:9) Wakati wewe na bibi ao bwana yako munasoma pamoja Biblia na vichapo vyetu, muzungumuzie namna munaweza kutumikisha mambo yenye munajifunza. Mutafute njia za kuonyeshana upendo na heshima, na pia njia za kuonyeshana wema na kuhangaikiana. Omba Yehova akusaidie kukomalisha sifa zenye zitakusaidia kutia nguvu ndoa yenu na zenye zitafanya bibi ao bwana yako akupende zaidi.​—Mezali 15:16, 17; 1 Petro 1:7.

Tegemea muongozo wa Yehova wakati wa ibada ya familia

22. Juu ya nini tunapaswa kutendea bibi ao bwana yetu kwa upendo na heshima?

22 Tunapaswa kufanya nguvu yetu yote ili kutendea bibi ao bwana yetu kwa upendo na heshima. Ile itafanya ndoa yetu ikuwe ya muzuri na yenye nguvu zaidi. Na jambo la maana zaidi, tutamufurahisha Yehova.​—Zaburi 147:11; Waroma 12:10.