Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 10

Ndoa Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu

Ndoa Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu

“Kamba ya nyuzi tatu (3) haiwezi kukatika haraka.”​—MUHUBIRI 4:12.

1, 2. (a) Wale wenye wametoka tu kuoana wanatumainia nini? (b) Tutazungumuzia nini katika sura hii?

WAZIA namna bwana arusi na bibi-arusi wanakuwaka wenye furaha siku ya ndoa yao. Wanakuwaka na furaha kwa ajili ya maisha yao ya wakati wenye kuja na wanakuwaka na matumaini na mipango mingi. Wanatumainia kuwa ndoa yao itaendelea na itakuwa yenye furaha.

2 Lakini, ndoa mingi zenye zinaanzaka muzuri, haziendeleake kuwa vile. Ili bibi na bwana waendelee kuishi pamoja mu ndoa na waendelee kuwa wenye furaha, wako na lazima ya muongozo kutoka kwa Mungu. Kwa hiyo, acha tuzungumuzie jibu la Biblia kuhusu hii maulizo: Ndoa inaleta faida gani fulani? Kama unataka kuoa ao kuolewa, namna gani unaweza kuchagua muzuri mutu wa kuoana naye? Unaweza kufanya nini ili ukuwe bwana muzuri ao bibi muzuri? Na ni nini inaweza kusaidia ndoa iendelee?​—Soma Mezali 3:5, 6.

NINAPASWA KUOA AO KUOLEWA?

3. Mutu anapaswa kuoa ao kuolewa ili akuwe na furaha? Fasiria.

3 Watu fulani wanaamini kama mutu anaweza tu kuwa na furaha ikiwa iko mwenye kuoa ao kuolewa. Lakini ile haiko kweli. Yesu alisema kama kubakia bila kuoa ao kuolewa inaweza kuwa zawadi. (Matayo 19:11, 12) Na mutume Paulo alisema kama kuko faida za kubakia bila kuoa ao kuolewa. (1 Wakorinto 7:32-38) Ni wewe wa kuamua ikiwa utaoa ao kuolewa. Haupaswe kuacha marafiki wako, watu wa familia, ao desturi yenu ikukaze kuoa ao kuolewa.

4. Taja faida fulani za ndoa ya muzuri.

4 Biblia inasema kama ndoa pia ni zawadi kutoka kwa Mungu na kama iko na faida fulani. Yehova alisema hivi juu ya mwanaume wa kwanza, Adamu: “Haiko muzuri mwanaume huyu aendelee kuwa peke yake. Nitamufanyia musaidizi, akuwe kikamilisho chake.” (Mwanzo 2:18) Yehova aliumba Eva ili akuwe bibi ya Adamu, na wakakuwa familia ya kwanza ya wanadamu. Kama bibi na bwana wako na watoto, ndoa yao inapaswa kuleta hali ya usalama yenye inaweza kuwasaidia kuchunga watoto wao. Lakini kuzaa watoto haiko tu njo kusudi ya kufunga ndoa.​—Zaburi 127:3; Waefeso 6:1-4.

5, 6. Namna gani ndoa inaweza kuwa kama “kamba ya nyuzi tatu”?

5 Mufalme Sulemani aliandika hivi: “Wawili ni muzuri zaidi kuliko mumoja kwa sababu wako na zawabu ya muzuri kwa ajili ya kazi yao ya nguvu. Kwa maana kama mumoja wao anaanguka, ule mwingine anaweza kusimamisha mwenzake. Lakini itakuwa namna gani kwa ule mwenye kuwa peke yake kama anaanguka bila mutu wa kumusimamisha? . . . Na kamba ya nyuzi tatu (3) haiwezi kukatika haraka.”​—Muhubiri 4:9-12.

6 Ndoa ya muzuri inaweza kufanya watu wawili wakuwe na urafiki wa karibu sana. Inaweza kufanya wasaidiane, watiane moyo, na kila mutu alinde mwenzake. Upendo unaweza kufanya ndoa ikuwe yenye nguvu, lakini ndoa itakuwa yenye nguvu zaidi ikiwa bibi na bwana wanamuabudu Yehova. Ndoa yao inaweza kuwa kama “kamba ya nyuzi tatu,” kamba ya nyuzi tatu yenye kufungwa sana pamoja. Kamba ya namna ile iko nguvu zaidi kuliko kamba ya nyuzi mbili. Ndoa itakuwa yenye nguvu ikiwa bibi na bwana wanamufanya Yehova kuwa sehemu ya ndoa yao.

7, 8. Ni shauri gani mutume Paulo alitoa juu ya ndoa?

7 Kisha kuoana, bibi na bwana wanaweza kufurahia kutimiziana tamaa za kufanya ngono. (Mezali 5:18) Lakini, kama mutu anaoa ao kuolewa juu tu ya kutimiza zile tamaa, anaweza kukosa kuchagua kwa hekima mutu wa kuoana naye. Njo maana Biblia inasema kama mutu anapaswa kufunga ndoa kisha kupita “mwanzo wa kipindi cha ujana,” ni kusema, kipindi cha maisha chenye tamaa za kufanya ngono ni zenye nguvu sana. (1 Wakorinto 7:36) Ni muzuri zaidi kuoa ao kuolewa kisha zile tamaa kutulia. Kisha ule wakati mutu anaweza kufikiri muzuri na kukamata uamuzi wa muzuri.​—1 Wakorinto 7:9; Yakobo 1:15.

8 Kama uko unafikiria kuoa ao kuolewa, ni muzuri kuwa na mawazo yenye kufaa na kukumbuka kama kila ndoa inakuwaka na magumu. Paulo alisema kama wale wenye kuoa ao kuolewa “watakuwa na taabu katika mwili wao.” (1 Wakorinto 7:28) Hata ndoa yenye kuwa muzuri zaidi inakuwaka na magumu. Kwa hiyo kama unapenda kuoa ao kuolewa, uhakikishe kama unachagua kwa hekima mutu wa kuoana naye.

NINAPASWA KUOANA NA NANI?

9, 10. Ni nini inaweza kutokea kama tunaoana na mutu mwenye hamuabudu Yehova?

9 Kuko kanuni ya Biblia ya maana yenye mutu anapaswa kukumbuka wakati anachagua bwana ao bibi. Ile kanuni ni hii: “Musifungwe nira yenye haiko sawa pamoja na watu wenye hawako waamini.” (2 Wakorinto 6:14) Ule mufano unategemea jambo lenye lilikuwa linafanywa wakati wa kulima. Kama wanyama wawili hawana urefu moja ao nguvu ileile, mulimaji hawezi kuwafunga pamoja ili kulima shamba. Kuwafunga pamoja haiwezi kuwa muzuri juu wote wawili wanaweza kuteseka. Vilevile, ndoa kati ya mutu mwenye kumuabudu Yehova na mutu mwenye hamuabudu, bila shaka itakuwa na magumu mingi. Njo maana Biblia inatupatia shauri lenye hekima la kuoa ao kuolewa “katika Bwana tu.”​—1 Wakorinto 7:39.

10 Wakati fulani, kuko Wakristo wenye waliona kama ni muzuri kuoa ao kuolewa na mutu mwenye hamuabudu Yehova kuliko kubakia peke yao. Lakini kama tunazarau shauri la Biblia, mara mingi ile inaleta maumivu na inafanya mutu akose furaha. Tukiwa waabudu wa Yehova, kumutumikia njo jambo la maana zaidi mu maisha yetu. Unaweza kujisikia namna gani ikiwa hauwezi kutimiza ile sehemu ya maana sana mu maisha yako pamoja na bibi ao bwana yako? Watu wengi waliamua kubakia peke yao kuliko kuoana na mutu mwenye hamupendi Yehova na kumutumikia.​—Soma Zaburi 32:8.

11. Namna gani unaweza kuchagua muzuri mutu wa kuoana naye?

11 Ile haimaanishe kama mutu yeyote mwenye kumutumikia Yehova atakuwa bwana ao bibi muzuri kwako. Kama uko unawaza kuoa ao kuolewa, tafuta mutu mwenye unapenda kabisa na mwenye munaweza kupatana naye muzuri. Uchunge mupaka wakati utapata mutu mwenye anapenda kufanya mambo yenye wewe pia unapenda kufanya mu maisha na mwenye anatia utumishi wake kwa Mungu pa nafasi ya kwanza. Kamata wakati wa kusoma na kufikiri sana juu ya mashauri ya muzuri kuhusu ndoa, mashauri yenye kupatikana mu vichapo vya mutumwa muaminifu.​—Soma Zaburi 119:105.

12. Tunaweza kujifunza nini kutokana na ndoa zenye zilipangwa na wazazi zenye kuzungumuziwa mu Biblia?

12 Katika desturi fulani, ni jambo la kawaida kwa wazazi kuchagulia mutoto wao mwanaume ao mwanamuke mutu wa kuoana naye. Inajulikana kama wazazi njo wanajua muzuri mutu mwenye kufaa kabisa kuoana na mutoto wao. Zamani, watu walikuwa pia na ile desturi. Kwa hiyo, kama familia yenu inaamua kufuata ile desturi, Biblia inaweza kusaidia wazazi kujua sifa za kuangalia. Kwa mufano, wakati Abrahamu alichagulia mutoto wake Isaka bibi, jambo la kwanza lenye alikazia haikuwa feza ao hali ya maisha; alimuchagulia mwanamuke mwenye kumupenda Yehova.​—Mwanzo 24:3, 67; ona Mafasirio Ingine ya 25.

NAMNA GANI NINAWEZA KUJITAYARISHA KWA AJILI YA NDOA?

13-15. (a) Namna gani mwanaume anaweza kujitayarisha ili akuwe bwana muzuri? (b) Namna gani mwanamuke anaweza kujitayarisha ili akuwe bibi muzuri?

13 Kama uko unafikiria kuoa ao kuolewa, hakikisha kama uko tayari. Pengine unawaza kama uko tayari, lakini acha tuone ikiwa kujitayarisha kwa ajili ya ndoa inamaanisha nini. Jibu linaweza kukushangaza.

Chukua wakati wa kusoma na kufikiri sana juu ya mashauri ya Neno la Mungu kuhusu ndoa

14 Biblia inaonyesha kama mu familia, bibi na bwana wako kila mutu na madaraka yake. Kwa hiyo inaeleweka kama kuwa tayari kwa ajili ya ndoa itaomba jambo fulani tofauti, ukuwe mwanaume ao mwanamuke. Kama mwanaume iko anafikiria kuoa, anapaswa kujiuliza ikiwa iko tayari kuwa kichwa cha familia. Yehova anatazamia bwana atimizie bibi na watoto wake mahitaji ya kimwili na ya moyoni. Jambo la maana zaidi, bwana anapaswa kuongoza mambo ya kiroho ya familia yake. Biblia inasema kama mwanaume mwenye hahangaikie familia yake iko “mubaya kuliko mutu mwenye hana imani.” (1 Timoteo 5:8) Kwa hiyo, kama uko mwanaume mwenye anafikiria kuoa, ona namna hii kanuni ya Biblia inaweza kukusaidia: “Tayarisha kazi yako ya inje, na utayarishe kila kitu katika shamba; kisha ujenge nyumba yako.” Mu maneno ingine, mbele ya kuoa, hakikisha kama uko ule bwana mwenye Yehova anapenda ukuwe.​—Mezali 24:27.

15 Mwanamuke mwenye kufikiria kuolewa anapaswa kujiuliza ikiwa iko tayari kwa ajili ya madaraka yenye bibi anapaswa kutimiza ao pengine ile yenye mama anapaswa kutimiza. Biblia inazungumuzia njia fulani kati ya njia mingi zenye kuonyesha kuwa bibi muzuri anahangaikia bwana yake na watoto wake. (Mezali 31:10-31) Leo, wanaume wengi na wanamuke wengi wanafikiria tu mambo yenye mutu mwenye wataoana naye anaweza kuwafanyia. Lakini Yehova anapenda tufikirie mambo yenye tunaweza kufanyia mutu mwenye tutaoana naye.

16, 17. Kama uko unafikiria kuoa ao kuolewa, unapaswa kufikiria nini?

16 Mbele ya kuoa ao kuolewa, fikiri sana juu ya mambo yenye Yehova anasema kuhusu bwana na bibi. Kuwa kichwa cha familia hakumaanishe kama mwanaume anaweza kumutendea mwenzake kwa ukali, ikuwe kimwili ao kumutesa moyoni. Kichwa muzuri wa familia anafuata mufano wa Yesu, mwenye sikuzote iko mwenye upendo na mwema kwa wale wenye kuwa chini ya uongozi wake. (Waefeso 5:23) Kwa upande wake, mwanamuke anapaswa kuelewa ikiwa kutegemeza maamuzi ya bwana yake na kumuunga mukono kutamaanisha nini. (Waroma 7:2) Anapaswa kujiuliza ikiwa atafurahia kujitiisha kwa mwanaume mwenye hakamilike. Ikiwa anaona kama hataweza kufanya vile, pengine ataona kama ni muzuri zaidi abakie peke yake kwa sasa.

17 Bibi ao bwana anapaswa kuhangaikia zaidi kufurahisha mwenzake kuliko kujifurahisha yeye mwenyewe. (Soma Wafilipi 2:4.) Paulo aliandika hivi: “Kila mumoja wenu anapaswa kumupenda bibi yake kama vile anajipenda mwenyewe; kwa upande mwingine, bibi anapaswa kumuheshimia sana bwana yake.” (Waefeso 5:21-33) Bibi na bwana wako na lazima ya kujisikia kama wanapendwa na kuheshimiwa. Lakini ili ndoa ikuwe muzuri, mwanaume iko zaidi sana na lazima ya kujua kama bibi yake anamuheshimia, na mwanamuke iko zaidi sana na lazima ya kujua kama bwana yake anamupenda.

18. Juu ya nini mwanaume na mwanamuke wanapaswa kuwa waangalifu wakati wa uchumba?

18 Uchumba unapaswa kuwa wakati wa muzuri wa kusaidia mwanaume na mwanamuke wajuane muzuri. Pia, ni wakati wa kuona mambo mu njia yenye kufaa na kusema mambo waziwazi ili waweze kuamua ikiwa wanaweza kabisa kuishi pamoja. Wakati wa uchumba, mwanaume na mwanamuke wanajifunza kuzungumuza pamoja na kujaribu kujua mambo yenye kuwa kabisa katika moyo wa mwingine. Wakati uhusiano wao unakuwa nguvu, ni jambo la kawaida kila mumoja avutie mwingine kimwili. Lakini wanapaswa kuwa waangalifu kuhusu namna wanaonyeshana upendo mbele waoane juu wasifikie kufanya jambo fulani la mubaya. Upendo wa kweli utawasaidia wajizuie na utawaepusha kufanya jambo fulani lenye linaweza kuharibisha uhusiano kati yao wenyewe na uhusiano wao pamoja na Yehova.​—1 Watesalonike 4:6.

Wakati wa uchumba, mwanaume na mwanamuke wanaweza kujifunza kuzungumuza pamoja

NINAWEZA KUFANYA NINI ILI NDOA YETU IENDELEE?

19, 20. Namna gani Wakristo wanaona ndoa?

19 Vitabu mingi na filme vinamalizia kwa kuonyesha ndoa kubwa na yenye furaha. Mu maisha ya kawaida, siku ya ndoa ni mwanzo tu. Yehova alikusudia ndoa ikuwe uhusiano wenye kuendelea.​—Mwanzo 2:24.

20 Leo, watu wengi wanaona ndoa kuwa mupango wenye unapaswa kufanya wakati kidogo tu. Ni mwepesi kufunga ndoa na ni mwepesi kuivunja. Watu fulani wanaona kama wakati magumu inaanza, ile njo wakati wa kuachana na kuvunja ndoa. Lakini kumbuka ule mufano wenye tulizungumuzia wa kamba yenye nyuzi tatu zenye kufungana sana pamoja. Kamba yenye iko vile haitakatika hata kama inakokotwa sana. Wakati tunatafuta musaada wa Yehova, ndoa yetu itaendelea. Yesu alisema hivi: “Kile chenye Mungu ameunganisha, mutu yeyote asikitenganishe.”​—Matayo 19:6.

21. Ni nini itasaidia bibi na bwana wapendane?

21 Sisi wote tuko na uwezo na uzaifu mbalimbali. Ni mwepesi sana kukazia uzaifu wa wengine, zaidi sana uzaifu wa bibi ao bwana yetu. Lakini kama tunafanya vile, hatutakuwa na furaha. Kwa upande mwingine, kama tunakaza akili juu ya sifa za muzuri za bwana ao bibi yetu, tunaweza kuwa na ndoa yenye furaha. Je, inawezekana kuwa na ile maoni juu ya mwenzetu mwenye hakamilike? Ndiyo! Yehova anajua kama hatukamilike, lakini anaona zaidi sana sifa zetu za muzuri. Waza kama hangekuwa anafanya vile! Muandikaji mumoja wa zaburi alisema hivi: “Kama ungekuwa unaangalia makosa, Ee Yah, basi ni nani, Ee Yehova, angeweza kusimama?” (Zaburi 130:3) Bibi na bwana wanaweza kumuiga Yehova kwa kuangalia mambo ya muzuri yenye bwana ao bibi yao anafanya na kuwa tayari kusamehe.​—Soma Wakolosai 3:13.

22, 23. Namna gani Abrahamu na Sara ni mufano muzuri kwa watu wenye kuoana?

22 Kadiri miaka inapita, ndoa inaweza kuwa yenye nguvu zaidi. Abrahamu na Sara walikuwa na ndoa yenye furaha na yenye ilifanya muda murefu. Wakati Yehova aliambia Abrahamu waache nyumba yao katika muji wa Uru, inawezekana Sara alikuwa na zaidi ya miaka 60. Wazia namna ilikuwa nguvu kwake kuacha nyumba ya muzuri na kuishi mu mahema. Lakini Sara alikuwa rafiki na bibi wa muzuri kwa bwana yake, na alimuheshimia kabisa. Kwa hiyo, aliunga mukono maamuzi ya Abrahamu na alimusaidia kuitimiza.​—Mwanzo 18:12; 1 Petro 3:6.

23 Kusema kweli, kuwa na ndoa ya muzuri haimaanishe kama bibi na bwana watakuwa wanapatana sikuzote mu kila jambo. Siku fulani, wakati Abrahamu na Sara hawakupatana juu ya jambo fulani, Yehova aliambia Abrahamu hivi: “Umusikilize.” Abrahamu alifanya vile, na matokeo ilikuwa muzuri. (Mwanzo 21:9-13) Kama wakati fulani haupatane na bibi ao bwana yako, usivunjike moyo. Jambo la maana ni kuendelea kutendeana kwa upendo na heshima hata kama hamupatane juu ya jambo fulani.

Kuanzia mwanzo, fanya Neno la Mungu likuwe sehemu ya ndoa yenu

24. Tunaweza kufanya nini ili ndoa yetu imuletee Yehova heshima?

24 Mu kutaniko la Kikristo, muko maelfu ya ndoa zenye kuwa na furaha. Kama unapenda kuoa ao kuolewa, ukumbuke kama kuchagua mutu wa kuoana naye ni moja kati ya maamuzi ya maana zaidi yenye unaweza kukamata mu maisha. Itakuwa na matokeo juu ya maisha yako yote, kwa hiyo utafute muongozo wa Yehova. Ukifanya vile, utachagua kwa hekima mutu wa kuoana naye, utajitayarisha muzuri kwa ajili ya ndoa, utafanya ndoa yenu ikuwe yenye nguvu na yenye upendo yenye itamuletea Yehova heshima.