Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 15

Ufurahie Kazi Yako

Ufurahie Kazi Yako

“Kila mutu anapaswa . . . kufurahia kazi yake yote ya nguvu.”​—MUHUBIRI 3:13.

1-3. (a) Namna gani watu wengi wanajisikia kuhusu kazi yao? (b) Tutajibia maulizo gani katika sura hii?

MU DUNIA yote watu wanatumika kwa bidii ili kutimiza mahitaji yao wenyewe na mahitaji ya familia zao. Watu wengi hawafurahie kazi yao, na watu fulani wanaogopa hata kuenda ku kazi kila siku. Ikiwa wewe pia unajisikia vile, unaweza kufanya nini ili kazi yako ikuwe yenye kufurahisha zaidi? Unaweza kufanya nini ili ufurahie kazi yako?

2 Yehova anatuambia hivi: “Kila mutu anapaswa kula na kunywa na kufurahia kazi yake yote ya nguvu. Ni zawadi ya Mungu.” (Muhubiri 3:13) Yehova alituumba na uhitaji na tamaa ya kufanya kazi. Anapenda tufurahie mambo yenye tunafanya.​—Soma Muhubiri 2:24; 5:18.

3 Sasa, ni nini inaweza kutusaidia tufurahie kazi yetu? Ni kazi ya namna gani Wakristo wanapaswa kuepuka? Namna gani tunaweza kuonyesha usawaziko kati ya kazi yetu na ibada yetu kwa Yehova? Na ni kazi gani ya maana zaidi tunaweza kufanya?

WAFANYAKAZI WAWILI WAKUBWA ZAIDI

4, 5. Namna gani Yehova anaona kazi?

4 Yehova mwenyewe anapenda kufanya kazi. Mwanzo 1:1 inasema hivi: “Katika mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.” Kisha Mungu kumaliza kuumba dunia na kila kitu chenye kuwa ndani, alisema kama uumbaji wake ulikuwa ‘muzuri sana.’ (Mwanzo 1:31) Muumbaji wetu alikuwa mwenye furaha kwa sababu ya vitu vyenye aliumba.​—1 Timoteo 1:11.

5 Yehova hajaacha hata kidogo kufanya kazi. Yesu alisema hivi: “Baba yangu anaendelea kufanya kazi mupaka sasa.” (Yohana 5:17) Hata kama hatuna habari zote juu ya mambo yote ya ajabu yenye Yehova amekuwa akifanya, kuko mambo fulani yenye tunajua. Amekuwa akichagua wale wenye watatawala na Mwana wake, Yesu Kristo, ili wakuwe sehemu ya Ufalme. (2 Wakorinto 5:17) Yehova iko pia anatumika kwa bidii ili kuongoza na kuhangaikia wanadamu. Kwa sababu ya kazi yetu ya kuhubiri yenye kufanywa mu dunia yote, mamilioni ya watu wanafikia kumujua Yehova na wako na tumaini la kuishi milele mu dunia paradiso.​—Yohana 6:44; Waroma 6:23.

6, 7. Yesu ni mufanyakazi wa namna gani?

6 Kama vile Baba yake, Yesu anafurahia kufanya kazi. Mbele akuje ku dunia, Yesu alikuwa “fundi wa kazi” wa Mungu, na alisaidia katika kazi ya kuumba vitu vyote mbinguni na duniani. (Mezali 8:22-31; Wakolosai 1:15-17) Wakati alikuwa ku dunia, Yesu aliendelea kufanya kazi kwa bidii. Wakati alikuwa kijana, alijifunza kuwa seremala mwenye ufundi, na inawezekana alijenga nyumba na kutengeneza vitu vya mu nyumba. Yesu alijua muzuri kazi yake hivi kwamba alijulikana kuwa “ule seremala.”​—Marko 6:3.

7 Lakini, kazi ya maana zaidi yenye Yesu alifanya ku dunia ilikuwa kuhubiri habari njema na kufundisha watu juu ya Yehova. Ilimuomba miaka tatu na nusu ili kumaliza utumishi wake, na alitumika kwa bidii tangu asubui sana mupaka usiku. (Luka 21:37, 38; Yohana 3:2) Yesu alitembea mamia ya kilometre kwenye barabara zenye vumbi, akihubiria watu wengi zaidi.​—Luka 8:1.

8, 9. Juu ya nini Yesu alifurahia kazi yake?

8 Yesu aliona kufanya kazi ya Mungu kama vile chakula. Ile kazi ilimupatia nguvu. Kuko siku zenye Yesu alitumika sana hivi kwamba hakuchukua hata wakati wa kula chakula. (Yohana 4:31-38) Alitumia kila nafasi ili kusaidia wengine wajifunze juu ya Baba yake. Ndiyo sababu angeweza kusema hivi: “Nimekutukuza katika dunia, kwa kuwa nimemaliza kazi yenye ulinipatia nifanye.”​—Yohana 17:4.

9 Ni wazi kuwa, Yehova na Yesu wanatumika kwa bidii sana na kazi yao inawafanya watosheke na kuwaletea furaha. Tunapenda ‘kuwa waigaji wa Mungu,’ na tunapenda ‘kufuata hatua [za Yesu] kwa ukaribu.’ (Waefeso 5:1; 1 Petro 2:21) Ndiyo sababu tunajaribu kutumika kwa bidii na kujikaza sana katika mambo yote yenye tunafanya.

TUNAPASWA KUONA KAZI YETU NAMNA GANI?

10, 11. Ni nini inaweza kutusaidia tukuwe na mawazo ya muzuri kuhusu kazi yetu?

10 Tukiwa watu wa Yehova, tunatumika kwa bidii ili kutimiza mahitaji yetu wenyewe na ya familia zetu. Tunapenda tufurahie kazi yetu, lakini ile inaweza kuwa nguvu. Sasa, tunaweza kufanya nini ikiwa hatufurahie kazi yetu?

Kuwa na mawazo ya muzuri kunaweza kufanya kazi yoyote ikuwe yenye kufurahisha

11 Ukuwe na mawazo ya muzuri. Pengine hatuwezi kubadilisha mahali kwenye tunatumikia ao kazi yenye tunafanya, lakini tunaweza kubadilisha mawazo yetu. Kuelewa mambo yenye Yehova anapenda tufanye kunaweza kutusaidia. Kwa mufano: Yehova anapenda kichwa cha familia afanye nguvu yake yote ili kutimiza mahitaji ya familia yake. Kwa kweli, Biblia inasema kama mutu mwenye hatimize mahitaji ya familia yake “ni mubaya kuliko mutu mwenye hana imani.” (1 Timoteo 5:8) Ikiwa uko kichwa cha familia, unatumika kwa bidii ili kutimiza mahitaji ya familia yako. Ikuwe unapenda kazi yako ao hapana, unajua kama kwa kutimiza mahitaji ya familia yako, unamufurahisha pia Yehova.

12. Kuwa mufanyakazi mwenye bidii na muaminifu kunatuletea faida gani?

12 Ukuwe mufanyakazi mwenye bidii na munyoofu. Ile inaweza kufanya ikuwe mwepesi zaidi ufurahie kazi yako. (Mezali 12:24; 22:29) Zaidi ya ile, mukubwa wako wa kazi atakutumainia. Wakubwa wa kazi wanapendaka wafanyakazi waaminifu kwa sababu wanajua kama hawatawaiba feza, vitu, ao wakati. (Waefeso 4:28) Na jambo la maana zaidi, Yehova anaona wakati unafanya kazi kwa bidii na kwa uaminifu. Unaweza kuwa na “zamiri nyoofu” kwa sababu unajua kama uko unamufurahisha Mungu mwenye unapenda.​—Waebrania 13:18; Wakolosai 3:22-24.

13. Ni faida gani ingine yenye tunapata wakati tunakuwa na mwenendo muzuri ku kazi?

13 Ujue kama mwenendo wako ku kazi unaweza kumuletea Yehova sifa. Ile inatupatia sababu ingine ya kufurahia kazi yetu. (Tito 2:9, 10) Mufano wako wa muzuri unaweza hata kuchochea mumoja kati ya wafanyakazi wenzako ajifunze Biblia.​—Soma Mezali 27:11; 1 Petro 2:12.

NI KAZI YA NAMNA GANI NINAPASWA KUCHAGUA?

14-16. Tunapaswa kufikiria nini wakati tunachagua kazi?

14 Biblia haina oroza ao liste ya kazi zenye Mukristo anapaswa kukubali ao zenye anapaswa kukataa. Lakini iko na kanuni zenye zinaweza kutusaidia tukamate maamuzi ya muzuri kuhusu kazi. (Mezali 2:6) Kwa kutumia kanuni za Biblia, tunaweza kujiuliza maulizo yenye kufuata.

Utafute kazi yenye haitapingana na kanuni za Yehova

15 Hii kazi itaniomba kufanya jambo fulani lenye Yehova anasema kuwa ni la mubaya? Tumejifunza kuhusu tabia zenye Yehova anachukia, kama vile kuiba na kusema uongo. (Kutoka 20:4; Matendo 15:29; Waefeso 4:28; Ufunuo 21:8) Kwa hiyo, tunakuwa waangalifu ili kuepuka kazi yoyote yenye inapingana na kanuni za Yehova.​—Soma 1 Yohana 5:3.

16 Hii kazi inaunga mukono ao inachochea tabia fulani yenye Yehova anakataza? Kwa mufano, utafanya nini ikiwa unapewa kazi ya kukaribisha watu ku hospitali yenye inasaidiaka watu kutosha mimba? Hakuna ubaya wowote wa kufanya kazi ya kukaribisha watu. Lakini unajua namna Yehova anajisikia wakati mutu anatosha mimba. Kwa hiyo, hata kama hautasaidia watu kutosha mimba moja kwa moja, je, hautajisikia kuwa mwenye kosa mbele ya Yehova?​—Kutoka 21:22-24.

17. Ni nini inaweza kutusaidia tukamate maamuzi yenye itamufurahisha Mungu?

17 Kwa kutumia kanuni zenye Mungu anatutolea, tunaweza kuwa kama watu wenye kuzungumuziwa mu Waebrania 5:14, “wale wenye kwa kutumia nguvu zao za utambuzi wamezizoeza kufanya tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa.” Ujiulize hivi: ‘Ikiwa ninakubali kufanya kazi hii, je, wengine watakwazika? Kazi hii itaniomba niache bibi na watoto wangu na kuenda mu inchi ingine? Ile itakuwa na matokeo gani juu yao?’

“MUHAKIKISHE MAMBO YA MAANA ZAIDI”

18. Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kutia ibada yetu pa nafasi ya kwanza?

18 Inaweza kuwa nguvu kutia ibada yetu kwa Yehova pa nafasi ya kwanza katika hizi “nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia.” (2 Timoteo 3:1) Kupata kazi na kuichunga inaweza kuwa nguvu kabisa. Tunapaswa kuhangaikia familia yetu, lakini tunajua kama ni ibada yetu njo inapaswa kutiwa pa nafasi ya kwanza. Hatuwezi kuruhusu vitu vya kimwili vikuwe vya maana sana mu maisha yetu. (1 Timoteo 6:9, 10) Sasa, namna gani tunaweza ‘kuhakikisha mambo ya maana zaidi’ na wakati uleule tutimize mahitaji ya familia yetu?​—Wafilipi 1:10.

19. Namna gani kumutegemea Yehova kunaweza kutusaidia tukuwe na usawaziko kuhusu kazi yetu?

19 Umutegemee Yehova kwa moyo wako wote. (Soma Mezali 3:5, 6.) Tunajua kama Mungu anajua kabisa mambo yenye tuko nayo lazima na kama anatuhangaikia sana. (Zaburi 37:25; 1 Petro 5:7) Neno lake linatuambia hivi: “Njia yenu ya maisha ikuwe bila upendo wa feza, wakati munatosheka na vitu vya sasa. Kwa maana [Mungu] amesema: ‘Sitakuacha hata kidogo, na sitakutupa hata kidogo.’” (Waebrania 13:5) Yehova hapendi tuhangaike sana juu ya kutimiza mahitaji ya familia yetu. Mara kwa mara, ameonyesha kama anaweza kutimiza mahitaji ya watu wake. (Matayo 6:25-32) Hata kama tunafanya kazi gani, tunajifunza neno la Mungu kwa ukawaida, tunahubiri habari njema, na tunaenda ku mikutano yetu ya Kikristo.​—Matayo 24:14; Waebrania 10:24, 25.

20. Tunaweza kufanya nini ili maisha yetu iendelee kuwa mwepesi?

20 Fanya jicho lako liendelee kukazia jambo moja. (Soma Matayo 6:22, 23.) Ile inamaanisha kufanya maisha yako iendelee kuwa mwepesi ili uweze kutia pa nafasi ya kwanza utumishi wako kwa Yehova. Tunajua kama ni kukosa akili kuruhusu feza, kuwa na maisha ya muzuri, ao vyombo vyenye vimetengenezwa hivi karibuni vikuwe vya maana sana kwetu kuliko urafiki wetu pamoja na Mungu. Sasa, ni nini itatusaidia kutanguliza mambo yenye inapaswa kutangulizwa? Tunapaswa kujikaza sana ili tusikuwe na madeni. Kama uko tayari na deni, ukamate mipango ili kuipunguza ao kuilipa yote. Ikiwa hatuko waangalifu, vitu vya kimwili vinaweza kukamata wakati na nguvu yetu mingi, na tunaweza kukosa wakati wa kusali, kujifunza, ao wa kuhubiri. Kuliko kuacha vitu vya kimwili vifanye maisha yetu ikuwe nguvu, tunataka kujifunza namna ya kutosheka na vitu vya musingi kama vile “chakula na nguo.” (1 Timoteo 6:8) Na hata kama tuko mu hali gani, ni jambo la maana tujichunguze kila wakati ili kuona kama tunaweza kumutumikia Yehova zaidi.

21. Juu ya nini tunapaswa kuamua mambo ya kutia pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu?

21 Tia mambo yenye kufaa pa nafasi ya kwanza. Tunapaswa kutumia kwa hekima wakati wetu, nguvu, na vitu vyetu vya kimwili. Kama hatuko waangalifu, vitu vyenye haviko vya maana sana, kama vile masomo ao feza, vitakamata wakati wetu wa maana. Yesu alisema hivi: “Muendelee kutafuta kwanza Ufalme.” (Matayo 6:33) Maamuzi yetu, tabia, mambo yenye tunafanya kila siku, na miradi yetu, ile yote inaonyesha ni mambo gani tunatia pa nafasi ya kwanza katika mioyo yetu.

KAZI YA MAANA SANA YENYE TUNAWEZA KUFANYA

22, 23. (a) Ni kazi gani ya maana sana yenye sisi Wakristo tunaweza kufanya? (b) Ni nini itatusaidia tufurahie kazi yetu?

22 Kazi ya maana sana yenye tuko nayo ni kumutumikia Yehova na kuhubiria wengine habari njema. (Matayo 24:14; 28:19, 20) Kama Yesu, tunapenda kutumia nguvu yetu yote katika ile kazi. Watu fulani wamehamia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri. Wengine wanajifunza luga ingine ili waweze kuhubiria watu wenye wanazungumuza ile luga. Uzungumuze na wale wenye wamefanya vile, na uwaulize juu ya ile jambo. Watakuambia kama maisha yao imefikia kuwa yenye furaha zaidi na yenye maana zaidi.​—Soma Mezali 10:22.

Kumutumikia Yehova njo kazi ya maana sana yenye tunaweza kufanya

23 Leo, watu wengi kati yetu wanapaswa kupitisha saa mingi zaidi ku kazi ao hata kwa kufanya kazi mbalimbali ili tu kutimiza mahitaji ya musingi ya familia yao. Yehova anajua ile, na anapendezwa na kila jambo lenye tunafanya ili kuhangaikia familia yetu. Kwa hiyo, sisi wote tuendelee kumuiga Yehova na Yesu kwa kutumika kwa bidii, hata kama tunafanya kazi ya namna gani. Na tukumbuke kama kazi yetu ya maana sana ni kumutumikia Yehova na kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu. Ile itatuletea furaha ya kweli.