Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 16

Umupinge Ibilisi

Umupinge Ibilisi

“Mumupinge Ibilisi, naye atawakimbia ninyi.”​—YAKOBO 4:7.

1, 2. Tunapaswa kuelewa nini juu ya Shetani na pepo wachafu?

MAISHA mu ulimwengu mupya wa Yehova itakuwa ya muzuri sana. Mwishowe, tutaishi kama vile Mungu alipenda tuishi. Lakini leo tunaishi mu ulimwengu wenye kutawaliwa na Shetani pamoja na pepo wake wachafu. (2 Wakorinto 4:4) Hata kama hatuwezi kuwaona, wanaishi na ni wenye nguvu sana.

2 Katika sura hii, tutaona namna tunaweza kubakia karibu na Yehova na kujilinda na Shetani. Yehova anaahidi kuwa atatusaidia. Lakini tunapaswa kuelewa njia zenye Shetani na pepo wachafu wanatumia ili kutudanganya na kutushambulia.

“KAMA SIMBA MWENYE KUNGURUMA”

3. Ibilisi iko na kusudi gani juu ya uhusiano wetu pamoja na Yehova?

3 Shetani anasema kama wanadamu wanamuabudu Yehova kwa sababu ya faida fulani na kama tutaacha kumutumikia Yehova ikiwa mambo inakuwa nguvu sana. (Soma Yobu 2:4, 5.) Wakati mutu fulani anaonyesha kama anapenda kujifunza kumuhusu Yehova, Shetani na pepo wachafu wanaona ile jambo, na wanajaribu kumuzuia. Wanakasirika wakati mutu fulani anajitoa kwa Yehova na kubatizwa. Biblia inalinganisha Ibilisi na “simba mwenye kunguruma, akitafuta kumumeza mutu.” (1 Petro 5:8) Shetani anapenda kuharibu uhusiano wetu pamoja na Yehova.​—Zaburi 7:1, 2; 2 Timoteo 3:12.

Shetani anakasirika wakati tunajitoa kwa Yehova

4, 5. (a) Shetani hana uwezo wa kufanya nini? (b) ‘Kumupinga Ibilisi’ maana yake nini?

4 Lakini hatupaswe kumuogopa Shetani na pepo wake wachafu. Yehova amewawekea mipaka kuhusu mambo yenye wanaweza kututendea. Yehova anaahidi kama “kundi kubwa” la Wakristo wa kweli wataokoka “taabu kubwa.” (Ufunuo 7:9, 14) Hakuna jambo lenye Ibilisi anaweza kufanya ili kuzuia hilo litimie, kwa sababu Yehova iko analinda watu Wake.

5 Kama tunabakia karibu na Yehova, Shetani hawezi kuvunja uhusiano wetu pamoja na Yehova. Neno la Mungu linatuhakikishia hivi: “Yehova iko pamoja na ninyi wakati wote wenye munaendelea kuwa pamoja naye.” (2 Mambo ya Nyakati 15:2; soma 1 Wakorinto 10:13.) Wanaume na wanamuke wengi waaminifu wa zamani, kama vile Abeli, Enoko, Noa, Sara, na Musa, walimupinga Ibilisi kwa kubakia karibu na Yehova. (Waebrania 11:4-40) Sisi pia tunaweza kufanya vile. Neno la Mungu linatupatia ahadi hii: “Mumupinge Ibilisi, naye atawakimbia ninyi.”​—Yakobo 4:7.

TUKO KATIKA ‘MAPAMBANO’

6. Shetani anatushambulia namna gani?

6 Hata kama Shetani anajua kama Yehova amemuwekea mipaka kuhusu mambo yenye anaweza kututendea, ataendelea kujaribu kutumia kila njia ili kuregeza uhusiano wetu pamoja na Mungu. Leo, Ibilisi anatushambulia mu njia mingi mbalimbali, na anatumia njia zenye amekuwa akitumia kwa maelfu ya miaka. Ni njia gani fulani kati ya njia zenye anatumia?

7. Juu ya nini Shetani anashambulia watu wa Yehova?

7 Mutume Yohana aliandika hivi: “Ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za ule muovu.” (1 Yohana 5:19) Ulimwengu huu muovu unatawaliwa na Shetani na angependa pia kutawala watu wa Yehova. (Mika 4:1; Yohana 15:19; Ufunuo 12:12, 17) Ibilisi anajua kama anabakia na wakati kidogo sana, kwa hiyo anaendelea kuchochea sana kila mumoja wetu ili asikuwe mushikamanifu kwa Yehova. Wakati fulani Shetani anatushambulia moja kwa moja, lakini wakati mwingine anatushambulia kwa kutumia njia zenye hazionekane waziwazi.

8. Ni jambo gani lenye kila Mukristo anapaswa kujua?

8 Tunasoma hivi katika andiko la Waefeso 6:12: “Tunapambana [“tunapigana mieleka,” maelezo ya chini] . . . na majeshi ya pepo wachafu katika mahali pa kimbingu.” Kila Mukristo anafanya vita kipekee na Shetani na pepo wachafu. Tunapaswa kujua kama wale wote wenye wanajitoa kwa Yehova wako pia mu ile vita. Mu barua yake kwa Wakristo wa Efeso, mutume Paulo alitia moyo mara tatu Wakristo ‘wasimame imara.’​—Waefeso 6:11, 13, 14.

9. Shetani na pepo wachafu wanajaribu kututendea namna gani?

9 Shetani na pepo wachafu wanajaribu kutudanganya kwa kutumia njia mingi mbalimbali. Kupata ushindi juu ya Shetani katika njia fulani, hakumaanishe kama Shetani hawezi kupata ushindi juu yetu katika njia ingine. Ibilisi anajaribu kupata uzaifu wetu ili achague mitego yenye atatumia ili kutunasa. Lakini hatupaswe kunaswa, kwa sababu Biblia inatufundisha juu ya mitego yenye Ibilisi anatumia. (2 Wakorinto 2:11; ona Mafasirio Ingine ya 31.) Mutego moja kati ya mitego yenye anatumia ni kufanya watu wapashane habari na pepo wachafu.

UJITENGE KABISA NA PEPO WACHAFU

10. (a) Kupashana habari na pepo wachafu kunatia ndani nini? (b) Namna gani Yehova anaona tabia ya kupashana habari na pepo wachafu?

10 Kupashana habari na pepo wachafu kunatia ndani mambo yenye haiko ya kawaida yenye inafanya mutu akuwe na uhusiano na pepo wachafu, mambo kama vile kutabiri matukio, uchawi, ulozi, ao kujaribu kuzungumuza na wafu. Biblia inatuambia kama kupashana habari na pepo wachafu ni “chukizo” na kama hatuwezi kufanya vile na wakati uleule tumuabudu Yehova. (Kumbukumbu la Torati 18:10-12; Ufunuo 21:8) Wakristo wanapaswa kuepuka kabisa njia yoyote ya kupashana habari na pepo wachafu.​—Waroma 12:9.

11. Kupendezwa na mambo yenye haiko ya kawaida kunaweza kutuletea hatari gani?

11 Shetani anajua kama ikiwa tunapendezwa na mambo yenye haiko ya kawaida, itakuwa mwepesi kwake kutuingiza mu mambo ya kupashana habari na pepo wachafu. Njia yoyote ya kupashana habari na pepo wachafu inaweza kuharibu uhusiano wetu pamoja na Yehova.

SHETANI ANAJARIBU KUTUDANGANYA

12. Namna gani Shetani anajaribu kuchochea mawazo yetu?

12 Shetani anajaribu kuvuruga mawazo ya watu. Hatua kwa hatua anatia mashaka mu akili za watu, mupaka wanafikia kufikiri kuwa “wema ni ubaya na ubaya ni wema.” (Isaya 5:20) Ibilisi anachochea wazo la kuwa kufuata mashauri ya Biblia hakulete faida na kama tunaweza kuwa wenye furaha zaidi ikiwa hatufuate kanuni za Mungu.

13. Namna gani Shetani amejaribu kuleta mashaka?

13 Njia moja kati ya njia zenye matokeo zaidi yenye Shetani anatumia, ni kueneza mashaka. Amekuwa akitumia ile njia kwa muda murefu. Mu bustani ya Edeni, alijaribu kuleta mashaka wakati alimuuliza Eva hivi: “Je, ni kweli kwamba Mungu alisema hamupaswe kula matunda ya kila muti wa bustani?” (Mwanzo 3:1) Kisha, katika siku za Yobu, Shetani alimuuliza Yehova mbele za malaika: “Je, Yobu anamuogopa Mungu bure?” (Yobu 1:9) Kisha Yesu kubatizwa, Shetani alimujaribu kwa kusema hivi: “Kama wewe uko mwana wa Mungu, ambia majiwe haya yakuwe mikate.”​—Matayo 4:3.

14. Namna gani Shetani anaweza kufanya watu wafikiri kama kupashana habari na pepo wachafu hakuna hatari?

14 Leo, Ibilisi anaendelea kutia mashaka mu akili za watu. Anajaribu kufanya watu wajiulize ikiwa ni mubaya kabisa kupashana habari na pepo wachafu kwa kufanya njia fulani za kupashana habari na pepo hao zionekane kuwa za muzuri. Hata Wakristo fulani wamefikia kufanywa vipofu ili wasione hatari. (2 Wakorinto 11:3) Sasa, tunaweza kufanya nini ili kujilinda? Namna gani tunaweza kuwa hakika kama hatudanganywe na Shetani? Tuzungumuzie njia mbili zenye anaweza kutumia ili kutudanganya: mambo ya kujifurahisha na matunzo.

SHETANI ANATUMIA TAMAA ZETU ZA ASILI ILI KUTUJARIBU

15. Namna gani tunaweza kujiingiza mu mambo ya pepo wachafu kupitia mambo yenye tunajifurahisha nayo?

15 Leo, filme mingi, video, programu za televizyo, michezo ya ordinatere, na site za Enternete vinaonyesha mambo ya pepo wachafu, uchawi, na nguvu zenye haziko za kawaida. Watu wengi hawaone hatari ya kujifurahisha na ile mambo na hawatambue hatari ya kuacha pepo wachafu mu maisha yao. Mutu anaweza pia kujiingiza mu mambo ya kupashana habari na pepo wachafu kupitia mambo kama vile kutabiri matukio kwa kuangalia nyota, karte, kitu fulani chenye kuwa kama kioo, na kwa kusoma alama za mikono. Ibilisi anaficha hatari na anajaribu kufanya ile mambo ionekane kuwa yenye haieleweke, yenye kuvutia, na yenye kufurahisha. Mutu anaweza hata kuwaza kuwa hakuna hatari yoyote ya kuangalia jambo fulani lenye linahusu pepo wachafu ao lenye haliko la kawaida ikiwa kwa kweli hapashane habari na pepo wachafu. Juu ya nini ile mawazo ni yenye hatari?​—1 Wakorinto 10:12.

16. Juu ya nini tunapaswa kuepuka kujifurahisha na mambo yenye inahusu pepo wachafu?

16 Shetani na pepo wachafu hawawezi kujua mawazo yetu. Lakini wanaweza kujua mambo yenye tunatamani na namna yetu ya kufikiri kwa kuangalia maamuzi yenye tunakamata kwa ajili yetu wenyewe na familia yetu, kutia ndani maamuzi yetu juu ya mambo ya kujifurahisha. Ikiwa tunachagua filme, muziki, ao vitabu vyenye kuhusu mambo ya kupashana habari na pepo wachafu, ulozi, kuingiwa na pepo wachafu, uchawi, mizimu, ao mambo yenye kufanana na ile, Shetani na pepo wachafu wataona kama tunapendezwa na ile mambo. Wanaweza kujaribu kutuingiza ndani zaidi mu mambo ya kupashana habari na pepo wachafu.​—Soma Wagalatia 6:7.

17. Namna gani Shetani anaweza kutumia tamaa yetu ya kupenda kuwa na afya ya muzuri?

17 Pia, Shetani anaweza kutumia tamaa yetu ya kupenda kuwa na afya ya muzuri. Leo, watu wengi wanateseka kwa sababu ya kuwa na afya ya mubaya. Mutu anaweza kuwa amejaribu njia mbalimbali za matunzo, lakini bila kupata matokeo ya muzuri. (Marko 5:25, 26) Anaweza hata kufikia kupoteza tumaini na kuwa tayari kukubali matunzo yoyote. Lakini kwa kuwa tuko Wakristo, tunapaswa kuwa waangalifu ili tusichague matunzo yenye kutia ndani kutumia “nguvu za uchawi.”​—Isaya 1:13.

Umutegemee Yehova wakati unagonjwa

18. Ni matunzo ya namna gani Wakristo wanapaswa kuepuka?

18 Katika Israeli ya zamani, watu fulani walitumia “nguvu za uchawi.” Yehova aliwaambia hivi: “Wakati munanyoosha mikono yenu, Ninawaficha macho yangu. Hata kama munatoa sala nyingi, Sisikilize.” (Isaya 1:15) Waza juu ya jambo hili: Yehova hangesikiliza hata sala zao! Hatupendi kufanya jambo lolote lenye linaweza kuharibu uhusiano wetu pamoja na Yehova na kufanya akatae kutusaidia, zaidi sana wakati tuko wagonjwa. (Zaburi 41:3) Kwa hiyo, tunapaswa kuchunguza ikiwa matunzo yenye tunataka kufuata haina uhusiano wowote na mambo ya kupashana habari na pepo wachafu ao nguvu zenye haziko za kawaida. (Matayo 6:13) Tukiona kama inawezekana ile matunzo ikuwe na uhusiano na pepo wachafu, tunapaswa kuiepuka!​—Ona Mafasirio Ingine ya 32.

HADISI KUHUSU PEPO WACHAFU

19. Namna gani Ibilisi amefanya watu wengi waogope?

19 Hata kama watu fulani wanawaza kuwa Ibilisi na pepo wachafu ni watu wa kuwazia tu, wengine wanajua kama ni watu wenye kuishi kwa sababu ya mambo yenye wamekwisha kujionea. Watu wengi wanaogopa sana roho waovu na ni watumwa wa desturi zenye kutegemea mambo ya uchawi. Wengine wanafanya watu waogope pepo wachafu kwa kueneza hadisi zenye kuonyesha kama wanatendea mubaya wanadamu. Mara mingi, watu wanafurahia zile hadisi na wanakuwa na hamu ya kuzielezea wengine. Na mara mingi, zile hadisi zote zinafanya watu wamuogope Ibilisi.

20. Namna gani tunaweza kueneza uongo wa Shetani?

20 Fikiria jambo hili: Shetani anapenda watu wamuogope. (2 Watesalonike 2:9, 10) Yeye ni muongo mwenye anajua namna ya kuchochea akili za wale wenye kuvutiwa na mambo ya kupashana habari na pepo wachafu na anafanya waamini mambo yenye haiko kabisa ya kweli. Wale watu wanaweza kueleza mambo yenye wanafikiri kuwa waliona na kusikia. Kadiri watu wanarudilia zile hadisi, ni vile zinatiwa chumvi. Hatupendi kumusaidia Shetani kueneza woga kwa kurudilia zile hadisi.​—Yohana 8:44; 2 Timoteo 2:16.

21. Kuliko kuzungumuzia hadisi zenye zinahusu pepo wachafu, tunaweza kuzungumuzia nini?

21 Ikiwa mutu wa Yehova alikuwa na uhusiano na pepo wachafu zamani, hapaswe kuzungumuzia ile mambo ili kufurahisha wengine. Watu wa Yehova hawapaswe kuogopeshwa na jambo lolote lenye Ibilisi na pepo wake wachafu wanaweza kufanya. Lakini, tunapaswa kukaza akili juu ya Yesu na juu ya nguvu zenye Yehova amemupatia. (Waebrania 12:2) Yesu hakufurahisha wanafunzi wake kwa kuwaelezea hadisi zenye zinahusu pepo wachafu. Alikazia ujumbe wa Ufalme na “mambo makubwa ya Mungu.”​—Matendo 2:11; Luka 8:1; Waroma 1:11, 12.

22. Umeazimia kufanya nini?

22 Tusisahau hata kidogo kama kusudi la Shetani ni kuharibu uhusiano wetu pamoja na Yehova. Atajaribu kufanya jambo lolote ili kutimiza kusudi lake. Lakini tunajua njia zenye Ibilisi anatumia na tumeazimia kupinga njia zote za kupashana habari na pepo wachafu. ‘Hatutamupatia Ibilisi nafasi’ ya kuregeza azimio letu. (Soma Waefeso 4:27.) Ndiyo, ikiwa tunamupinga Ibilisi, hatutanaswa na mitego yake na tutakuwa salama katika ulinzi wa Yehova.​—Waefeso 6:11.