Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 1

Upendo wa Mungu Hauna Mwisho

Upendo wa Mungu Hauna Mwisho

“Kumupenda Mungu kunamaanisha hivi, kwamba tushike amri zake; na bado amri zake haziko muzigo muzito.”​—1 YOHANA 5:3.

1, 2. Juu ya nini unamupenda Yehova Mungu?

UNAMUPENDA Mungu? Pengine kumupenda sana kulifanya ujitoe kwake katika sala. Pengine unajisikia kuwa yeye ni Rafiki yako wa muzuri zaidi. Lakini mbele hata umupende Yehova, yeye alikupenda. Biblia inasema hivi: “Sisi tunapenda, kwa sababu alitupenda kwanza.”​—1 Yohana 4:19.

2 Waza juu ya mambo yote yenye Yehova amefanya ili kuonyesha kama anatupenda. Ametupatia dunia ili ikuwe fasi ya muzuri ya kuishi na kila kitu chenye tuko nacho lazima ili tufurahie maisha. (Matayo 5:43-48; Ufunuo 4:11) Anapenda tukuwe na uhusiano wa muzuri pamoja naye, na amefanya iwezekane kwetu kujifunza juu yake. Wakati tunasoma Biblia, tunamusikiliza Yehova. Na wakati tunasali, anatusikiliza. (Zaburi 65:2) Anatuongoza na kututia nguvu kupitia roho yake takatifu yenye nguvu. (Luka 11:13) Alituma hata Mwana wake mupendwa ku dunia ili kutuokoa kutoka mu zambi na kifo.​—Soma Yohana 3:16; Waroma 5:8.

3. Namna gani tunaweza kuendelea kuwa na uhusiano wa muzuri pamoja na Yehova?

3 Waza kidogo juu ya mumoja kati ya marafiki wako wa karibu, mutu mwenye amekuwa pamoja na wewe wakati wa furaha na wakati wa magumu. Inaomba kujikaza ili kufanya urafiki wa karibu kama huo uendelee kuwa wenye nguvu. Ni vile pia kuhusu urafiki wetu pamoja na Yehova, Rafiki wa karibu zaidi mwenye tunaweza kuwa naye. Urafiki wetu pamoja naye unaweza kuendelea milele. Kwa hiyo Biblia inatuambia hivi: “Mubakie katika upendo wa Mungu.” (Yuda 21) Namna gani tunaweza kufanya vile? Biblia inajibia hivi: “Kumupenda Mungu kunamaanisha hivi, kwamba tushike amri zake; na bado amri zake haziko muzigo muzito.”​—1 Yohana 5:3.

“KUMUPENDA MUNGU KUNAMAANISHA HIVI”

4, 5. Namna gani upendo wako kwa Mungu ulianza kukomaa?

4 Mutume Yohana aliandika kuhusu “kumupenda Mungu.” Unakumbuka wakati kwa mara ya kwanza ulianza kumupenda Yehova?

Wakati unajitoa kwa Yehova na kubatizwa, unaonyesha kama unamupenda na kama unapenda kumutii milele

5 Kumbuka namna ulijisikia wakati ulijifunza kwa mara ya kwanza kuwa Yehova anapenda uishi milele mu ulimwengu mupya. Ulijifunza kuhusu mambo yote yenye alifanya ili jambo hilo liwezekane, na ulitambua kama zawadi yenye Yehova alitupatia kwa kutuma Mwana wake ku dunia ni ya bei sana. (Matayo 20:28; Yohana 8:29; Waroma 5:12, 18) Wakati ulijua kama Yehova anakupenda sana, moyo wako uliguswa sana, na wewe pia ulianza kumupenda.​—Soma 1 Yohana 4:9, 10.

6. Kumupenda mutu fulani kunatia ndani nini? Upendo wako kwa Mungu ulikuchochea kufanya nini?

6 Lakini kujisikia vile ilikuwa njo mwanzo wa kumupenda Mungu. Kwa mufano, wakati tunapenda mutu fulani, tunafanya zaidi ya kusema tu neno “ninakupenda.” Upendo unatusukuma kufanya mambo yenye itafurahisha mutu huyo. Vilevile, upendo wako kwa Yehova ulikuchochea ao kukusukuma uishi kwa njia yenye ingemufurahisha. Wakati upendo huo ulikomaa, bila shaka ulijitoa kwake na kubatizwa. Kwa kufanya vile, ulimupatia Yehova ahadi (ao, malako) ya kumutumikia milele. (Soma Waroma 14:7, 8.) Namna gani unaweza kutimiza ahadi hiyo?

“TUSHIKE AMRI ZAKE”

7. Kama tunamupenda Yehova, tutafanya nini? Amri fulani za Mungu ni gani?

7 Kwa sababu tunamupenda Yehova, ‘tunashika amri zake.’ Namna gani tunafanya vile? Tunamutii. Mu Biblia tunajifunza namna Yehova anapenda tuishi. Kwa mufano, anatuambia kama ni mubaya kulewa, kuiba ao kusema uongo, kufanya ngono na mutu mwenye haiko bibi ao bwana yetu, ao kuabudu mutu ao kitu chochote kuliko yeye.​—1 Wakorinto 5:11; 6:18; 10:14; Waefeso 4:28; Wakolosai 3:9.

8, 9. Namna gani tunaweza kujua mambo yenye Yehova anapenda tufanye mu hali zenye hakuna sheria yenye kuwa wazi katika Biblia? Toa mufano.

8 Lakini ili kumufurahisha Yehova, tunapaswa kufanya zaidi ya kutii tu amri zake. Hakutupatia oroza ao liste ya murefu ya sheria zenye zinahusu kila hali ya maisha yetu. Kwa hiyo, tunaweza kujikuta mu hali zenye hakuna sheria yenye kuwa wazi katika Biblia yenye inatuonyesha jambo la kufanya. Namna gani tunaweza kukamata maamuzi ya muzuri? (Waefeso 5:17) Mu Biblia tunapata kanuni, ni kusema, kweli za musingi zenye zinatufundisha namna Yehova anaona mambo. Na kadiri tunasoma Biblia, tunafikia kujua Yehova ni Mutu wa namna gani. Tunajua mawazo yake, kutia ndani mambo yenye anapenda na mambo yenye anachukia.​—Soma Zaburi 97:10; Mezali 6:16-19; ona Mafasirio Ingine ya 1.

9 Kwa mufano, namna gani tunachagua mambo ya kuangalia ku televizyo ao ku Enternete? Yehova hatuambie waziwazi kile tunapaswa kufanya. Lakini kanuni zenye anatupatia zitatusaidia kukamata maamuzi ya muzuri. Leo, mambo mingi ya kujifurahisha inajaa jeuri na uasherati. Mu Biblia, Yehova anatuambia kuwa “anachukia mutu yeyote mwenye kupenda jeuri” na kuwa “atahukumu waasherati na wazinifu.” (Zaburi 11:5; Waebrania 13:4) Namna gani kanuni hizo zinaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri? Wakati tu tunajua kama Yehova anachukia jambo fulani ao anaona jambo hilo kuwa chafu, tunapaswa kuliepuka.

10, 11. Juu ya nini tunamutii Yehova?

10 Juu ya nini tunamutii Yehova? Haiko juu tunataka tu kuepuka malipizi ao matatizo yenye mutu anapata kwa sababu ya kukamata maamuzi ya mubaya. (Wagalatia 6:7) Lakini, tunamutii Yehova kwa sababu tunamupenda. Kama vile watoto wenye wanapenda kufurahisha baba yao, tunapenda kumufurahisha Baba yetu wa mbinguni. Hakuna jambo lenye linaweza kuwa la muzuri zaidi kuliko kujua kama Yehova anatufurahia!​—Zaburi 5:12; Mezali 12:2; ona Mafasirio Ingine ya 2.

11 Hatumutii Yehova tu wakati ni mwepesi kufanya vile ao wakati hatuna jambo lingine la kufanya. Na kati ya sheria na kanuni zake, hatuchague zenye tunapaswa kufuata na zile zenye hatupaswe kufuata. (Kumbukumbu la Torati 12:32) Lakini, tunamutii mu mambo yote, kama muandikaji mumoja wa zaburi mwenye alisema hivi: “Ninapenda sana amri zako, ndiyo, ninazipenda.” (Zaburi 119:47; Waroma 6:17) Tunapenda kuwa kama vile Noa, mwenye alionyesha upendo wake kwa Yehova kwa kufanya mambo yote yenye Yehova alimuambia afanye. Biblia inasema kama “ni vile [Noa] alifanya kabisa.” (Mwanzo 6:22) Unapenda Yehova aseme vile juu yako?

12. Namna gani tunaweza kumufurahisha Yehova?

12 Yehova anajisikia namna gani wakati tunamutii? ‘Tunafurahisha moyo wake.’ (Mezali 11:20; 27:11) Waza juu ya jambo hili! Tunafanya Muumbaji wa ulimwengu wote afurahi wakati tunamutii. Lakini hatukazake kufanya vile. Kuliko kutukaza, ametupatia uhuru wa kuchagua. Hilo linamaanisha kama tuko na uhuru wa kuchagua kufanya mambo ya muzuri ao mambo ya mubaya. Yehova anapenda upendo wetu kwake utuchochee kukamata maamuzi ya muzuri ili tukuwe na maisha ya muzuri zaidi.​—Kumbukumbu la Torati 30:15, 16, 19, 20; ona Mafasirio Ingine ya 3.

“AMRI ZAKE HAZIKO MUZIGO MUZITO”

13, 14. Namna gani tunajua kama haiko nguvu kutii amri za Mungu? Toa mufano.

13 Sasa, namna gani ikiwa tunawaza kuwa ni nguvu kutii amri za Yehova ao kama amri hizo zitafanya tusikuwe tena na uhuru? Biblia inasema waziwazi hivi: “amri zake haziko muzigo muzito.” (1 Yohana 5:3) Neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa na “muzigo muzito” linamaanisha “kitu chenye kuwa kilo.” Mu maandiko ingine, neno hilo linatumiwa ili kuzungumuzia sheria zenye kupita mipaka ao watu wenye wanajaribu kutawala ao kuumiza wengine. (Matayo 23:4; Matendo 20:29, 30) Tafsiri ya New English Translation inasema hivi: ‘Amri zake hazituchokeshe.’ Amri za Yehova haziko “kilo,” ni kusema, haiko nguvu kwetu kuzitii. Sikuzote anaonyesha usawaziko mu mambo yenye anatuomba kufanya.

14 Kwa mufano, wazia uko unasaidia rafiki yako kuhamia mu nyumba ingine. Ametayarisha mizigo mbalimbali ya kuhama nayo. Mizigo fulani iko mwepesi kubeba, lakini mizigo ingine iko kilo sana hivi kwamba inaomba kunyanguliwa na watu wawili. Je, rafiki yako atakuomba unyangule muzigo wenye kuwa kilo sana wewe peke yako? Bila shaka hapana! Juu ya nini? Ni juu hapendi uumie. Kama rafiki huyo, Yehova hawezi hata kidogo kutuomba tufanye jambo fulani lenye kuwa nguvu sana. (Kumbukumbu la Torati 30:11-14) Yehova anajua tuko namna gani. “Anajua muzuri namna tumeumbwa, anakumbuka kwamba tuko mavumbi.”​—Zaburi 103:14.

15. Juu ya nini tunaweza kuwa hakika kama amri za Yehova ziko kwa faida yetu?

15 Musa aliambia taifa la Israeli kuwa amri za Yehova zilikuwa kwa ‘faida yao ya kudumu’ na kuwa utii wao ungewasaidia ‘waendelee kuishi.’ (Kumbukumbu la Torati 5:28-33; 6:24) Leo pia ni vile. Jambo lolote lenye Yehova anatuomba tufanye litafanya maisha yetu ikuwe muzuri zaidi. (Soma Isaya 48:17.) Baba yetu, Yehova, sikuzote anajua mambo yenye inaweza kutuletea faida. (Waroma 11:33) Biblia inatuambia hivi: “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Ile inamaanisha kama kila jambo lenye Yehova anasema na kufanya linachochewa na upendo.

16. Namna gani tunajua kama tunaweza kutii hata kama hatukamilike na hata kama tunaishi mu ulimwengu muovu?

16 Haiko mwepesi sikuzote kumutii Mungu. Tunaishi mu ulimwengu muovu wenye kutawaliwa na Ibilisi. Anajaribu kuchochea watu wafanye mambo ya mubaya. (1 Yohana 5:19) Tunapaswa pia kupambana na mawazo na hisia (ao, sentiments) zetu zenye hazikamilike, juu zinaweza kufanya tukose kumutii Mungu. (Waroma 7:21-25) Lakini upendo wetu kwa Yehova unatupatia nguvu ya kufanya mambo yenye kuwa sawa. Anaona namna tunajikaza kumutii, na anatusaidia kwa kutupatia roho yake takatifu yenye nguvu. (1 Samweli 15:22, 23; Matendo 5:32) Roho takatifu inatusaidia kukomalisha sifa zenye zinafanya ikuwe mwepesi kwetu kumutii.​—Wagalatia 5:22, 23.

17, 18. (a) Tutajifunza nini katika kitabu hiki? (b) Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

17 Katika kitabu hiki, tutajifunza namna tunaweza kuishi kwa njia yenye kumufurahisha Yehova. Tutajifunza namna ya kutumikisha kanuni zake na sheria zake kuhusu mwenendo safi mu maisha yetu. Kumbuka kama Yehova hatulazimishe hata kidogo tumutii. Wakati tunachagua kumutii, maisha yetu itakuwa muzuri zaidi na wakati wetu wenye kuja utakuwa wa muzuri sana. Jambo la maana zaidi, kumutii Mungu kutaonyesha ni kwa kadiri gani tunamupenda.​—Ona Mafasirio Ingine ya 4.

18 Ili kutusaidia kujua mambo ya muzuri na mambo ya mubaya, Yehova amepatia kila mumoja wetu zamiri. Ikiwa tunazoeza zamiri yetu, inaweza kutusaidia “tushike amri zake.” Kwa hiyo, zamiri ni nini, na namna gani tunaweza kuizoeza? Tutazungumuzia jambo hilo.