Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 8

Yehova Anapenda Watu Wake Wakuwe Safi

Yehova Anapenda Watu Wake Wakuwe Safi

“Kwa mwenye kuwa safi unajionyesha kuwa safi.”​—ZABURI 18:26.

1-3. (a) Juu ya nini mama anahakikisha kama mutoto wake iko safi? (b) Juu ya nini Yehova anapenda watu wake wakuwe safi?

WAZIA mama mumoja mwenye upendo anatayarisha mutoto wake ili aende ku masomo. Anahakikisha kuwa mutoto wake amenawa na kuwa nguo zake ziko safi na zenye kufaa. Ile inasaidia mutoto aendelee kuwa na afya ya muzuri na inaonyesha wengine kuwa wazazi wake wanamuchunga muzuri.

2 Baba yetu, Yehova, anapenda tukuwe safi na wenye kutakata. (Zaburi 18:26) Anajua kama kuwa safi kunatuletea faida. Na wakati tuko safi, tunamuletea heshima.​—Ezekieli 36:22; soma 1 Petro 2:12.

3 Kuwa safi maana yake nini? Na sababu gani ni muzuri tukuwe safi? Wakati tuko tunachunguza ile maulizo, pengine tunaweza kuona mabadiliko fulani yenye tunapaswa kufanya kipekee.

JUU YA NINI TUNAPASWA KUWA SAFI?

4, 5. (a) Juu ya nini tunapaswa kuwa safi? (b) Uumbaji unatufundisha nini juu ya namna Yehova anaona usafi?

4 Tunajifunza kuwa safi kupitia mufano wa Yehova mwenyewe. (Mambo ya Walawi 11:44, 45) Kwa hiyo, sababu kubwa yenye inapaswa kutuchochea tukuwe safi ni juu tunataka kuwa “waigaji wa Mungu.”​—Waefeso 5:1.

5 Uumbaji unatufundisha mambo mingi juu ya namna Yehova anaona usafi. Yehova aliumba mizunguko ya asili yenye kufanya hewa na maji viendelee kuwa safi. (Yeremia 10:12) Fikiria njia mingi zenye kufanya dunia iendelee kujisafisha yenyewe, hata kisha wanadamu kuichafua. Kwa mufano, Yehova aliumba viumbe vidogo-vidogo sana vyenye kuitwa mikrobe, vyenye vinaweza kuonekana tu kupitia darubini (ao, microscope). Mikrobe inaweza kubadilisha uchafu wenye sumu na kuufanya usikuwe na hatari. Ule ni utendaji wenye nguvu. Wanasayansi wanatumia hata mikrobe fulani ili kuondoa matokeo ya kuchafuliwa kwa hewa.​—Waroma 1:20.

6, 7. Sheria ya Musa ilionyesha namna gani kuwa wale wenye kumuabudu Yehova wanapaswa kuwa safi?

6 Pia, Sheria yenye Yehova alipatia Waisraeli kupitia Musa inatusaidia kuona kuwa usafi ni wa maana sana. Kwa mufano, watu walipaswa kuwa safi kimwili ili Yehova akubali ibada yao. Siku ya Upatanisho, kuhani mukubwa alipaswa kunawa mara mbili. (Mambo ya Walawi 16:4, 23, 24) Na mbele makuhani wengine watoe zabihu, walipaswa kunawa mikono na miguu yao. (Kutoka 30:17-21; 2 Mambo ya Nyakati 4:6) Katika hali fulani, malipizi ya kukosa kutii sheria juu ya usafi ilikuwa kifo.​—Mambo ya Walawi 15:31; Hesabu 19:17-20.

7 Namna gani leo? Tunaweza kujifunza mambo mingi zaidi juu ya kanuni za Yehova kupitia Sheria. (Malaki 3:6) Sheria hiyo ilionyesha waziwazi kama watumishi wa Yehova walipaswa kuwa safi. Kanuni za Yehova hazijabadilika. Leo, anatazamia waabudu wake wakuwe safi na wenye kutakata.​—Yakobo 1:27.

KUWA SAFI MAANA YAKE NINI?

8. Ni mu njia gani mbalimbali tunapaswa kuwa safi?

8 Kulingana na maoni ya Yehova, kuwa safi hakumaanishe tu kulinda mwili wetu, nguo, na nyumba yetu ikiwa safi. Usafi unahusu maisha yetu yote. Unatia ndani ibada yetu, mwenendo, na mawazo yetu. Kwa kweli, ili Yehova atuone kuwa safi, tunapaswa kuwa safi na wenye kutakata mu kila sehemu ya maisha yetu.

9, 10. Kuwa safi katika ibada yetu maana yake nini?

9 Ibada safi. Hatupaswe kuwa na uhusiano na dini ya uongo kwa njia yoyote ile. Wakati Waisraeli walikuwa wafungwa mu Babiloni, waliishi kati ya watu wenye walikuwa mu dini chafu ya kipagani. Isaya alitabiri kama Waisraeli wangerudia kwao Israeli na kurudisha ibada safi. Yehova aliwaambia hivi: “Mutoke kule, musiguse kitu chochote kichafu! Mutoke katikati yake, mujilinde mukiwa safi.” Hawakupaswa kuchanga ibada yao kwa Mungu na mafundisho, tabia, ao desturi za dini ya uongo ya Babiloni.​—Isaya 52:11.

10 Leo pia, Wakristo wa kweli wanaepuka dini ya uongo. (Soma 1 Wakorinto 10:21.) Mu dunia yote, desturi mingi, imani, na tabia zenye kupendwa na watu wengi vinategemea mafundisho ya dini za uongo. Kwa mufano, katika desturi mingi, watu wanaamini kama kuko kitu fulani ndani yetu chenye kinaendelea kuishi kisha mutu kufa, na kuko tabia mingi zenye kutegemea ile imani. (Muhubiri 9:5, 6, 10) Wakristo wanapaswa kuepuka zile desturi. Watu wa familia yetu wanaweza kutukaza tujiingize mu desturi fulani kati ya zile. Lakini, kwa kuwa tunapenda Yehova atuone kuwa watu safi, hatutakubali watukaze.​—Matendo 5:29.

11. Kuwa safi katika mwenendo wetu maana yake nini?

11 Mwenendo safi. Ili Yehova atuone kuwa safi, tunapaswa kuepuka uasherati wa kila namna. (Soma Waefeso 5:5.) Mu Biblia, Yehova anatuambia ‘tukimbie uasherati.’ Anaonyesha wazi kuwa wale wenye kuwa na mwenendo mubaya na wenye wanakataa kutubu “hawatariti Ufalme wa Mungu.”​—1 Wakorinto 6:9, 10, 18; ona Mafasirio Ingine ya 22.

12, 13. Juu ya nini tunapaswa kuwa safi katika mawazo yetu?

12 Mawazo safi. Mara mingi mawazo inaongoza kwenye matendo. (Matayo 5:28; 15:18, 19) Mawazo yenye kuwa safi itatuchochea kutenda kwa njia safi. Ni kweli kwamba hatukamilike, kwa hiyo tunaweza kuwa na mawazo ya mubaya mara kwa mara. Wakati tunakuwa na mawazo ya mubaya, tunapaswa kuachana nayo bila kukawia. Kama hatufanye vile, tunaweza kufikia kutambua kama moyo wetu hauko safi tena. Tunaweza kuanza kupenda kufanya mambo yenye tunaendelea kufikiria. Kuliko kufanya vile, tunapaswa kujaza akili yetu na mawazo yenye kuwa safi. (Soma Wafilipi 4:8.) Kwa hiyo, tunaepuka kujifurahisha na mambo machafu na yenye jeuri. Tunachagua kwa uangalifu mambo yenye tunasoma, kuangalia, na kuzungumuzia.​—Zaburi 19:8, 9.

13 Ili tubakie katika upendo wa Mungu, tunapaswa kuwa safi katika ibada yetu, mwenendo, na katika mawazo yetu. Lakini pia, Yehova anaona kuwa ni jambo la maana tukuwe safi kimwili.

TUNAWEZA KUFANYA NINI ILI TUKUWE SAFI KIMWILI?

14. Juu ya nini ni jambo la maana tukuwe safi kimwili?

14 Wakati mwili wetu unaendelea kuwa safi na pia mahali kwenye tunaishi, sisi na watu wenye kutuzunguka tutapata faida. Tutajisikia muzuri, na wengine watafurahia kuwa pamoja na sisi. Lakini kuko sababu moja ya maana zaidi ya kuwa safi kimwili. Wakati tuko safi tunamuletea Yehova heshima. Waza juu ya jambo hili: Kama unaona mutoto mwenye kila mara iko muchafu, unaweza kuwa na mawazo ya mubaya juu ya wazazi wake. Vilevile, kama hatujihangaikie wenyewe na kama hatuendelee kuwa safi, watu wanaweza kuwa na mawazo ya mubaya juu ya Yehova. Paulo alisema hivi: “Hatutoe sababu yoyote ya kukwaza kwa njia yoyote, ili kosa lolote lisipatikane katika utumishi wetu; lakini katika kila njia tunajipendekeza sisi wenyewe kuwa watumishi wa Mungu.”​—2 Wakorinto 6:3, 4.

Kwa kuwa tuko watu wa Yehova, tunapaswa kuendelea kuwa safi na kulinda safi nafasi kwenye tunaishi

15, 16. Tunaweza kufanya nini ili tuendelee kuwa safi?

15 Mwili na nguo zetu. Kuendelea kuwa safi inapaswa kuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku. Kwa mufano, inaomba kunawa kwa ukawaida, kila siku kama inawezekana. Tunanawa mikono yetu kwa kutumia maji na sabuni, zaidi sana mbele ya kupika ao kula, na ni lazima tufanye vile kisha kutoka ku choo (ao, W.C) ao kisha kugusa kitu kichafu. Kunawa mikono kunaweza kuonekana kuwa jambo la kawaida tu, lakini ni kwa maana ili kuzuia mikrobe na magonjwa kuendelea. Kufanya vile kunaweza hata kuokoa uzima. Kama hatuna choo ao mufumo wa kutosha uchafu, tunaweza kupata njia zenye kufaa ili kujiepusha na uchafu. Waisraeli wa zamani hawakuwa na mufumo wa kutosha uchafu, kwa hiyo walizika uchafu wao mu udongo, mbali na nyumba zao, na mbali na maji.​—Kumbukumbu la Torati 23:12, 13.

16 Haiko lazima nguo zetu zikuwe za hali ya juu, za bei sana, ao zenye zimetokea hivi karibuni zaidi. Lakini zinapaswa kuwa safi na zenye kufaa. (Soma 1 Timoteo 2:9, 10.) Tunapenda namna yetu ya kuonekana imuletee Yehova heshima sikuzote.​—Tito 2:10.

17. Juu ya nini tunapenda nyumba yetu na nafasi kwenye tunaishi vikuwe safi?

17 Nyumba yetu na nafasi kwenye tunaishi. Ikuwe tunaishi wapi, tunalinda nyumba yetu ikiwa safi. Pia, tunahakikisha kuwa gari, pikipiki, kinga, ao chombo chochote chenye kutusaidia kuenda mahali fulani kiko safi, zaidi sana kama tunakitumia wakati tunaenda ku mikutano ao mu mahubiri. Zaidi ya ile, mu kazi yetu ya kuhubiri, tunazungumuza na wengine juu ya uzima mu dunia paradiso yenye kuwa safi. (Luka 23:43; Ufunuo 11:18) Namna nyumba yetu na nafasi kwenye tunaishi vinaonekana, inaweza kuonyesha kuwa tuko tunajitayarisha sasa kwa ajili ya uzima mu ulimwengu mupya wenye utakuwa safi.

18. Juu ya nini tunapenda nafasi kwenye tunafanyia ibada pakuwe safi?

18 Nafasi kwenye tunafanyia ibada. Tunaonyesha kuwa tunaona usafi kuwa wa maana kwa kulinda nafasi kwenye tunafanyia mikutano ikiwa safi, ikuwe Jumba la Ufalme ao nafasi kwenye tunafanyia mikusanyiko. Wakati watu wanakuja ku Jumba la Ufalme kwa mara ya kwanza, mara mingi wanaona namna liko safi. Ile inamuletea Yehova heshima. Kwa kuwa tuko sehemu ya kutaniko, sisi wote tuko na nafasi ya kusaidia kusafisha Jumba letu la Ufalme na kuendelea kulilinda mu hali ya muzuri.​—2 Mambo ya Nyakati 34:10.

ACHANA NA TABIA CHAFU

19. Tunapaswa kuepuka kufanya nini?

19 Hata kama Biblia haitaje kila tabia ya mubaya yenye tunapaswa kuepuka, inatutolea kanuni zenye kutusaidia kuelewa namna Yehova anajisikia juu ya ile mambo. Hapendi tuvute tumbako ao kutumia mubaya pombe ao dawa za kulewesha. Kama tuko marafiki wa Mungu, tutaepuka kufanya mambo hayo. Juu ya nini? Ni juu tunaheshimia sana zawadi ya uzima. Tabia kama zile zinaweza kufanya maisha yetu ikuwe mufupi, kuharibu afya yetu, na kuharibu afya ya watu wenye tunaishi nao. Watu wengi wanajikaza kuacha zile tabia juu ya afya yao. Lakini, kwa kuwa tuko marafiki wa Yehova, tuko na sababu ya muzuri zaidi ya kuacha zile tabia​—upendo wetu kwa Mungu. Kijana mumoja mwanamuke alisema hivi: “Kupitia musaada wa Yehova, nilisafisha maisha yangu na niliachana na utumwa wangu wa tabia za mubaya. . . . Nawaza haingewezekana nifanye ile mabadiliko kwa nguvu yangu mwenyewe.” Tuzungumuzie basi kanuni tano za Biblia zenye zitasaidia mutu kuacha tabia zenye kuharibu.

20, 21. Ni tabia za namna gani Yehova anatuomba tuepuke?

20 “Kwa kuwa tuko na ahadi hizi, tujisafishe kila uchafu wa mwili na roho, tukikamilisha utakatifu katika kumuogopa Mungu.” (2 Wakorinto 7:1) Yehova anapenda tuachane na tabia chafu zenye zinaweza kuharibu akili ao mwili wetu.

21 Sababu kubwa yenye kufanya “tujisafishe kila uchafu” inazungumuziwa mu 2 Wakorinto 6:17, 18. Yehova anatuambia hivi: “Muache kugusa kitu kichafu.” Kisha anaahidi: “Nitawakaribisha ninyi ndani. Na nitakuwa baba kwenu, na ninyi mutakuwa wana na mabinti kwangu.” Kwa kweli, Yehova atatupenda kama vile baba anapenda watoto wake, ikiwa tunaepuka kitu chochote chenye kinaweza kufanya tusikuwe safi ao tusikuwe wenye kutakata mbele yake.

22-25. Ni kanuni gani za Biblia zinaweza kutusaidia kuepuka tabia chafu?

22 “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.” (Matayo 22:37) Hii ndiyo amri kubwa zaidi kuliko amri zote. (Matayo 22:38) Yehova anastahili tumuonyeshe upendo wetu wote. Namna gani tunaweza kumupenda kabisa ikiwa tunachagua kufanya jambo lenye linaweza kufupisha maisha yetu ao kuharibisha ubongo wetu? Kuliko kufanya vile, tunafanya nguvu yetu yote ili kuheshimia uzima wenye ametupatia.

23 “[Yehova] anapatia watu wote uzima na pumuzi na vitu vyote.” (Matendo 17:24, 25) Ikiwa rafiki yako anakupatia zawadi ya pekee, utaitupa ao kuiharibisha? Uzima ni zawadi ya ajabu kutoka kwa Yehova. Tunaifurahia kabisa. Kwa hiyo tunapenda kutumia uzima wetu kwa njia yenye itamuletea utukufu.​—Zaburi 36:9.

24 “Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.” (Matayo 22:39) Tabia chafu hazituumize tu sisi wenyewe. Zinaweza hata kuumiza wale wenye tunaishi nao, mara mingi wale wenye tunapenda sana. Kwa mufano, mutu mwenye anaishi mu nyumba moja na muvutaji wa tumbako anaweza kuwa na matatizo makubwa ya afya kwa sababu tu ya kupumua moshi. Lakini wakati tunaacha tabia za mubaya, tunaonyesha wale wenye tunaishi nao kama tunawapenda.​—1 Yohana 4:20, 21.

25 “Endelea kuwakumbusha wajitiishe na kutii serikali na mamlaka.” (Tito 3:1) Katika inchi mingi sheria inakataza kuwa na dawa fulani za kulewesha ao kuzitumia. Kwa kuwa Yehova anatuomba kuheshimia serikali, tunatii sheria kama zile.​—Waroma 13:1.

Wakati tunaendelea kuwa safi na wenye kutakata, tunamuletea Yehova heshima

26. (a) Tunapaswa kufanya nini ili Yehova akubali ibada yetu? (b) Juu ya nini kuendelea kuwa safi mbele ya Mungu njo namna ya muzuri zaidi ya kuishi?

26 Kama tunapenda kuwa marafiki wa Yehova, tunaweza kuona kama tunapaswa kufanya mabadiliko fulani. Kama ni vile, tunapaswa kuanza bila kukawia. Haiko mwepesi sikuzote kuacha tabia chafu, lakini tunaweza kuachana nazo! Yehova anaahidi kutusaidia. Anasema hivi: “Mimi, Yehova, niko Mungu wako, Mwenye anakufundisha ili ujipatie faida, Mwenye anakuongoza katika njia yenye unapaswa kutembea ndani yake.” (Isaya 48:17) Wakati tunafanya nguvu yetu yote ili kuwa safi na wenye kutakata, tunaweza kuwa hakika kama tunamuletea Mungu heshima.