Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 12

Sema Maneno ya ‘Muzuri ili Kujenga’

Sema Maneno ya ‘Muzuri ili Kujenga’

“Neno lenye kuoza lisitoke katika kinywa chenu, lakini neno la muzuri tu ili kujenga.”​—WAEFESO 4:29.

1-3. (a) Taja zawadi moja kati ya zawadi za muzuri zenye Yehova ametupatia. Namna gani tunaweza kuitumia mubaya? (b) Namna gani tunapaswa kutumia zawadi ya kusema?

BABA anamupatia kinga mutoto wake kijana mwanaume. Anafurahi kumupatia mutoto wake ile zawadi ya pekee. Lakini, mambo itakuwa namna gani kama ule mutoto anatembeza ile kinga ovyoovyo, anagonga mutu fulani, na kumuumiza? Ule baba atajisikia namna gani?

2 Yehova ni Mutoaji wa “kila zawadi ya muzuri na kila zawadi kamilifu.” (Yakobo 1:17) Moja kati ya zawadi za muzuri zenye ametupatia ni uwezo wa kusema. Zawadi ya kusema inatuwezesha kueleza mawazo yetu na namna tunajisikia. Tuko na uwezo wa kusema mambo yenye inasaidia watu na kuwafanya wajisikie muzuri. Lakini mambo yenye tunasema inaweza pia kuwaumiza wengine ao kuwafanya wajisikie mubaya.

3 Maneno ni yenye nguvu sana, na Yehova anatufundisha namna ya kutumia muzuri zawadi ya kusema. Anatuambia hivi: “Neno lenye kuoza lisitoke katika kinywa chenu, lakini neno la muzuri tu ili kujenga wengine kulingana na uhitaji, kusudi lipatie faida wale wenye wanalisikia.” (Waefeso 4:29) Acha tuzungumuzie namna tunaweza kutumia ile zawadi yenye Mungu ametupatia mu njia yenye itamufurahisha na kutia wengine moyo.

UFANYE ANGALISHO NA MANENO YAKO

4, 5. Kitabu cha Biblia cha Mezali kinatufundisha nini juu ya uwezo wetu wa kusema?

4 Maneno iko na nguvu, kwa hiyo tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu mambo yenye tunasema na namna tunaisema. Mezali 15:4 inasema hivi: “Ulimi mutulivu ni muti wa uzima, lakini maneno yenye kupotoka yanakatisha tumaini.” Kama vile tu muti muzuri unatuliza na kutoa uzima, maneno ya muzuri inatuliza mutu mwenye kuisikia. Kwa upande mwingine, maneno makali inaumiza wengine na kuwafanya wajisikie mubaya.​—Mezali 18:21.

Maneno ya upole inatuliza

5 Andiko la Mezali 12:18 linasema hivi: “Maneno yenye kusemwa bila kufikiri yanatoboa kama upanga.” Maneno makali inaweza kufanya moyo uumie na kuharibu urafiki. Pengine unaweza kukumbuka wakati mutu fulani aliongea na wewe kwa ukali na kukuumiza sana. Lakini, ile mezali inaendelea hivi: “Ulimi wa mwenye hekima unaponyesha.” Maneno ya muzuri inaweza kuponyesha moyo wenye kuumia na kutengeneza urafiki wenye umeharibika kwa sababu ya kukosa kuelewana. (Soma Mezali 16:24.) Ikiwa tunakumbuka kama maneno yetu inakuwaka na matokeo juu ya wengine, tutaitumia kwa uangalifu.

6. Juu ya nini haiko mwepesi kuzuia maneno yetu?

6 Sababu ingine yenye kutuchochea tukuwe waangalifu kuhusu namna yetu ya kusema ni juu sisi wote hatukamilike. “Muelekeo wa moyo wa mwanadamu ni mubaya,” na mara mingi maneno yetu inaonyesha mambo yenye kuwa ndani ya moyo wetu. (Mwanzo 8:21; Luka 6:45) Haiko mwepesi kabisa kuzuia maneno yetu. (Soma Yakobo 3:2-4.) Lakini tunapaswa kuendelea kujikaza ili kufanya namna yetu ya kuzungumuza na wengine ikuwe muzuri zaidi.

7, 8. Maneno yetu inaweza kuwa na matokeo gani juu ya urafiki wetu pamoja na Yehova?

7 Tunapaswa pia kuwa waangalifu kuhusu maneno yetu juu tutatoa hesabu kwa Yehova kuhusu mambo yenye tunasema na namna tunaisema. Yakobo 1:26 inasema hivi: “Kama mutu yeyote anawaza yeye ni muabudu wa Mungu lakini hazuie kabisa ulimi wake, anadanganya moyo wake mwenyewe, na ibada yake ni ya bure.” Kwa hiyo, kama hatuseme kwa uangalifu tunaweza kuharibu na hata kupoteza urafiki wetu pamoja na Yehova.​—Yakobo 3:8-10.

8 Ni wazi kuwa, tuko na sababu za muzuri za kuwa waangalifu juu ya mambo yenye tunasema na namna tunaisema. Ili tuweze kutumia zawadi yetu ya kusema mu njia yenye kumufurahisha Yehova, tunapaswa kujua ni maneno ya namna gani tunapaswa kuepuka.

MANENO YENYE KUBOMOA

9, 10. (a) Ni maneno ya namna gani watu wanatumia sana leo? (b) Juu ya nini tuepuke kutumia maneno machafu?

9 Leo, ni jambo la kawaida sana kutumia maneno machafu. Watu wengi wanawaza kama ili wengine wawaelewe, ni lazima watumie matusi na maneno machafu. Watu wenye kuchekesha wanazoea kufanya mizaha michafu na kutumia luga chafu ili kuchekesha watu wengine. Hata hivyo, mutume Paulo alisema hivi: “Munapaswa kuondoa mambo haya yote kutoka kwenu: kasirani kali, hasira, ubaya, matukano, na maneno machafu kutoka katika kinywa chenu.” (Wakolosai 3:8) Alisema pia kama “mizaha michafu” haipaswe ‘kutajwa hata kidogo katikati’ ya Wakristo wa kweli.​—Waefeso 5:3, 4.

10 Luga chafu inamuchukiza Yehova na wale wenye kumupenda. Haiko safi. Mu Biblia “uchafu” uko kati ya “matendo ya mwili.” (Wagalatia 5:19-21) “Uchafu” unaweza kutia ndani zambi mingi mbalimbali, na tabia moja ya uchafu inaweza kuongoza ku tabia ingine. Kama mutu anazoea kutumia luga na maneno machafu sana na anakataa kuacha, ile itaonyesha kama hapaswe tena kubakia mu kutaniko.​—2 Wakorinto 12:21; Waefeso 4:19; ona Mafasirio Ingine ya 23.

11, 12. (a) Porojo yenye kuumiza ni nini? (b) Juu ya nini tunapaswa kuepuka kusingizia mutu fulani?

11 Tunapaswa kuepuka pia porojo yenye kuumiza ao kusema-sema mubaya juu ya wengine. Ni jambo la kawaida kupendezwa na watu wengine na kuwaambia habari kuhusu marafiki na familia. Hata mu karne ya kwanza, Wakristo wa kwanza walikuwa wanapenda kujua habari juu ya ndugu na dada zao na mambo yenye wangefanya ili kuwasaidia. (Waefeso 6:21, 22; Wakolosai 4:8, 9) Lakini ni mwepesi mazungumuzo juu ya watu wengine igeuke na kuwa porojo yenye kuumiza. Kama tunaelezea wengine mambo yenye tulisikia, tunaweza kusema mambo yenye haiko ya kweli ao kuzungumuzia mambo yenye ilipaswa kubakia siri. Kama hatuko waangalifu tunaweza kufikia kusemea wengine mambo ya uongo, ao kuwasingizia. Wakati Wafarisayo walimushitaki Yesu juu ya mambo yenye hakufanya, walimusingizia. (Matayo 9:32-34; 12:22-24) Kusingiziana kunaharibisha sifa ya mutu, kunaongoza ku mabishano na maumivu, na kunaharibu urafiki.​—Mezali 26:20.

12 Yehova anataka tutumie maneno yetu ili kusaidia na kutia wengine moyo, haiko ili kufanya marafiki wakuwe maadui. Yehova anachukia wale wenye “kupanda ugomvi kati ya ndugu.” (Mezali 6:16-19) Musingiziaji wa kwanza ni Shetani Ibilisi, mwenye alimusingizia Mungu. (Ufunuo 12:9, 10) Katika ulimwengu wa leo, ni jambo la kawaida kwa watu kusemeana uongo. Lakini ile haipaswe kufanyika mu kutaniko la Kikristo. (Wagalatia 5:19-21) Kwa hiyo, tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu mambo yenye tunasema na sikuzote tunapaswa kufikiri mbele ya kusema. Mbele ya kusema jambo lenye ulisikia juu ya mutu fulani, ujiulize hivi: ‘Je, mambo yenye ninataka kusema ni ya kweli? Ni ya muzuri? Ni yenye faida? Nitapenda mutu mwenye niko ninazungumuza juu yake aisikie? Ninaweza kujisikia namna gani kama mutu mwingine anazungumuza ile mambo juu yangu?’​—Soma 1 Watesalonike 4:11.

13, 14. (a) Matukano inaweza kuwa na matokeo gani juu ya watu wengine? (b) Matusi ni nini? Juu ya nini Wakristo wanapaswa kuepuka kutumia matusi?

13 Wakati fulani, sisi wote tunasemaka mambo yenye tunafikia kuhuzunikia. Lakini hatupende kuwa na tabia ya kuchambua-chambua wengine ao kusema maneno makali ao ya mubaya. Matukano haina fasi mu maisha yetu. Paulo alisema hivi: “Muondoe kutoka kwenu kila namna ya uchungu wenye uovu, hasira, kasirani kali, kufoka, matukano.” (Waefeso 4:31) Biblia zingine zinatafsiri “matukano” kuwa “maneno maovu,” “luga yenye kuumiza,” na “luga ya matusi.” Matukano inashushia watu heshima yao na inafanya wajione kuwa wa bure. Zaidi sana watoto wanaweza kuumia haraka sana. Kwa hiyo tunataka kuwa waangalifu zaidi ili tusiwavunje moyo kupitia maneno yetu.​—Wakolosai 3:21.

14 Biblia inatuonya juu ya aina fulani ya kutukana yenye kuwa mubaya sana​—matusi. Matusi ni kuendelea kutukana wengine ili kuwaumiza. Inaweza kuhuzunisha sana kama mutu fulani anamutendea vile bibi ao bwana yake ao watoto wake. Kwa kweli, mutu mwenye anakataa kuacha kutumia matusi hastahili kubakia mu kutaniko. (1 Wakorinto 5:11-13; 6:9, 10) Kama vile tumejifunza, ikiwa tunasema mambo machafu, ya uongo, ao ya mubaya, tutaharibu uhusiano wetu pamoja na Yehova na pia pamoja na wengine.

MANENO YENYE KUJENGA

15. Ni maneno ya namna gani inafanya uhusiano wetu pamoja na wengine ukuwe wenye nguvu?

15 Namna gani tunaweza kutumia zawadi yetu ya kusema kwa njia yenye kumufurahisha Yehova? Hata kama Biblia haituambie waziwazi mambo yenye tunapaswa kusema na ile yenye hatupaswe kusema, inatuambia tuseme maneno ya “muzuri tu ili kujenga.” (Waefeso 4:29) Maneno yenye kujenga iko safi, ya muzuri, na ni ya kweli. Yehova anapenda tutumie maneno yetu ili kutia wengine moyo na kuwasaidia. Inaweza kuwa nguvu kufanya vile. Ni mwepesi sana kusema maneno makali na ya ovyoovyo, lakini ili kusema maneno ya muzuri inaomba kujikaza sana. (Tito 2:8) Tuzungumuzie basi njia fulani zenye tunaweza kutumia ili kujenga wengine kupitia maneno yetu.

16, 17. (a) Juu ya nini tunapaswa kuwapongeza wengine? (b) Ni nani wenye tunaweza kupongeza?

16 Yehova na Yesu wako tayari kila mara kutoa pongezi. Tunapenda kuwaiga. (Matayo 3:17; 25:19-23; Yohana 1:47) Ili tuweze kutoa pongezi yenye itatia kabisa mutu fulani moyo, inaomba kuonyesha kama unamuhangaikia na kupendezwa naye kipekee. Mezali 15:23 inasema hivi: “Neno lenye kusemwa wakati wenye kufaa​—ni la muzuri sana!” Tunatiwa moyo wakati mutu fulani anatupongeza kutoka moyoni kwa sababu ya kazi yetu yenye bidii ao wakati anaonyesha kama anafurahia jambo fulani lenye tulifanya.​—Soma Matayo 7:12; ona Mafasirio Ingine ya 27.

17 Kama unakuwa na tabia ya kuona mambo ya muzuri yenye wengine wanafanya, itakuwa mwepesi kwako kuwapongeza kutoka moyoni. Kwa mufano, pengine unaona kama mutu fulani mu kutaniko anatayarishaka muzuri hotuba zake ao anajikazaka kutoa maelezo ku mikutano. Kijana fulani anaweza kutetea kweli ku masomo, ao mutu mwenye kuzeeka anaweza kuhubiri kwa ukawaida. Maneno yako ya pongezi inaweza kuwa njo jambo lenye wako nalo lazima. Pia, ni jambo la maana sana bwana amuambie bibi yake kama anamupenda na kama anamufurahia. (Mezali 31:10, 28) Kama vile mimea iko na lazima ya mwangaza na maji, watu wako na lazima ya kujisikia kuwa wengine wanawafurahia. Zaidi sana watoto wako na lazima ya kujisikia vile. Tafuta nafasi za kuwapongeza juu ya sifa zao za muzuri na bidii yenye wanaonyesha. Pongezi inaweza kuwatia moyo sana, kuwafanya wajiaminie, na inaweza hata kuwachochea wajikaze sana kufanya mambo yenye kuwa sawa.

Tunaweza kutia wengine moyo na kuwafariji kupitia maneno yenye tunasema na namna tunaisema

18, 19. Juu ya nini tunapaswa kujikaza sana kutia wengine moyo na kuwafariji? Tunaweza kufanya vile namna gani?

18 Wakati tunatia moyo wengine na kuwafariji, tunafuata mufano wa Yehova. Anahangaikia sana “watu wa hali ya chini” na “wale wenye kupondwa.” (Isaya 57:15) Yehova anapenda ‘tuendelee kutiana moyo’ na ‘kusema kwa namna yenye kufariji wale wenye wameshuka moyo.’ (1 Watesalonike 5:11, 14) Wakati tunajikaza kufanya vile, anaona jambo hilo na kupendezwa na bidii yenye tunafanya.

19 Unaweza kutambua kama mutu fulani mu kutaniko ni mwenye kuvunjika moyo ao mwenye kushuka moyo. Unaweza kusema nini yenye inaweza kumusaidia? Pengine hautaweza kumaliza tatizo lake, lakini unaweza kumufanya aone kama unamuhangaikia. Kwa mufano, unaweza kupanga kupitisha wakati pamoja naye. Unaweza kumusomea andiko moja la Biblia lenye kutia moyo na hata kusali pamoja naye. (Zaburi 34:18; Matayo 10:29-31) Uwahakikishie kama ndugu na dada mu kutaniko wanawapenda. (1 Wakorinto 12:12-26; Yakobo 5:14, 15) Na useme kwa njia yenye kuonyesha kama maneno yako inatoka katika moyo na kama uko hakika na mambo yenye uko unasema.​—Soma Mezali 12:25.

20, 21. Ni nini inaweza kufanya watu wakuwe tayari kukubali mashauri?

20 Pia, tunajenga wengine kwa kuwapatia mashauri ya muzuri. Kwa kuwa hatukamilike, sisi wote tuko na lazima ya mashauri kila mara. Mezali 19:20 inasema hivi: “Sikiliza shauri na ukubali nizamu, ili ukuwe na hekima katika wakati wako wenye kuja.” Haiko wazee tu njo wanaweza kutoa mashauri ao muongozo. Wazazi wanapaswa kuongoza watoto wao. (Waefeso 6:4) Na dada wanaweza kutoleana mashauri ya muzuri. (Tito 2:3-5) Kwa kuwa tunapenda ndugu na dada zetu, tunapenda kuhakikisha kama tunatoa mashauri mu njia yenye haitawafanya wajisikie mubaya. Ni nini inaweza kutusaidia?

21 Pengine unakumbuka wakati wenye mutu fulani alikupatia shauri fulani la muzuri mu njia yenye ilikuwa mwepesi kwako kuikubali. Ni nini ilifanya ile shauri ikuwe ya muzuri? Bila shaka ulijisikia kama ule mutu alikuhangaikia kabisa. Ao pengine alisema kwa upole na kwa upendo. (Wakolosai 4:6) Inawezekana, ile shauri ilitegemea Biblia. (2 Timoteo 3:16) Ikuwe tunataja moja kwa moja andiko fulani la Biblia ao hapana, shauri lolote lenye tunatoa linapaswa kutegemea Maandiko. Hakuna mutu mwenye anapaswa kulazimisha wengine wakubali mawazo yake ao kutumia maandiko mubaya ili kutegemeza mawazo yake. Kukumbuka namna ulipewa shauri fulani kunaweza kukusaidia wakati unatolea wengine mashauri.

22. Utapenda kutumia namna gani zawadi yako ya kusema?

22 Uwezo wa kusema ni zawadi kutoka kwa Mungu. Upendo wetu kwake unapaswa kutuchochea kuitumia muzuri. Tukumbuke kama maneno iko na uwezo wa kubomoa ao kujenga. Kwa hiyo, tufanye nguvu yetu yote ili maneno yetu itie nguvu wengine na kuwatia moyo.