Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 15

Kuzungumuza kwa Usadikisho

Kuzungumuza kwa Usadikisho

1 Watesalonike 1:5

JAMBO LA KUFANYA: Onyesha kama unaamini kabisa kwamba mambo yenye uko unasema ni ya kweli na kwamba ni ya maana.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Jitayarishe muzuri kabisa. Jifunze habari yako mupaka uelewe mambo makubwa na namna gani Biblia inahakikisha kama ile mambo ni ya kweli. Pima kusema mambo makubwa ya sehemu yako mu maneno kidogo na ya mwepesi. Fikiria namna itasaidia wasikilizaji wako. Omba kusudi upate roho takatifu.

  • Tumia maneno yenye inaonyesha usadikisho. Kuliko kurudilia-rudilia tu maneno vile inaandikwa mu kichapo, tumia maneno yako. Chagua maneno yenye inaonyesha kama uko hakika na mambo yenye uko unasema.

  • Zungumuza kwa kukazia mambo na useme mambo yenye inatoka mu moyo. Sema na sauti ya kuenea. Angalia wasikilizaji wako, kama haiko mubaya kufanya vile kwenye unaishi.