Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 16

Kutia Watu Moyo

Kutia Watu Moyo

Yobu 16:5

JAMBO LA KUFANYA: Zungumuzia mambo yenye inatia moyo na yenye inaleta tumaini.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Ukuwe na mawazo ya muzuri juu ya wasikilizaji wako. Jua kama waamini wenzako wanapenda kumufurahisha Yehova. Hata kama inaomba ulete shauri, toa kwanza pongezi yenye inatoka mu moyo wakati inawezekana kufanya vile.

  • Usizungumuzie sana mambo ya kuvunja moyo. Zungumuzia mambo fulani yenye inaweza kuvunja moyo ikiwa tu kuko sababu ya maana ya kufanya vile. Mambo mingi yenye unazungumuzia inapaswa kuwa ya kutia moyo.

  • Tumia muzuri Neno la Mungu. Saidia watu waone mambo yenye Yehova amefanya, yenye iko anafanya, na yenye atafanyia wanadamu. Tia moyo na utie nguvu wasikilizaji wako.