Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 2

Namna ya Kuzungumuza

Namna ya Kuzungumuza

2 Wakorinto 2:17

JAMBO LA KUFANYA: Sema kwa njia ya kawaida, na useme mambo yenye inatoka mu moyo mu njia yenye inaonyesha namna unajisikia kuhusu habari na kuhusu wasikilizaji wako.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Sali na ujitayarishe muzuri. Umuombe Yehova akusaidie usikaze akili juu yako mwenyewe, lakini juu ya habari yenye utazungumuzia. Uweke mu akili yako mambo makubwa yenye unapenda kuzungumuzia. Sema mawazo yako mu maneno yako mwenyewe; usirudilie-rudilie tu maneno vile inaandikwa mu kichapo.

  • Sema mambo yenye inatoka mu moyo. Fikiria juu ya nini ile habari ni ya lazima kwa wasikilizaji wako. Uwafikirie sana. Ukifanya vile, namna yako ya kusimama ao kukaa, ishara zako za mwili na za uso, yote itaonyesha kama uko mwenye uchangamufu na mwenye urafiki.

  • Angalia wasikilizaji wako. Angalia wasikilizaji wako kama haiko mubaya kufanya vile kwenye unaishi. Wakati unatoa hotuba, angalia musikilizaji mumoja, kisha angalia mwengine, kuliko kuangalia watu wote mara moja.