Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 7

Kusema Mambo ya Kweli na Kusadikisha Wasikilizaji

Kusema Mambo ya Kweli na Kusadikisha Wasikilizaji

Luka 1:3

JAMBO LA KUFANYA: Tumia chanzo cha habari chenye kutegemeka juu ya kusaidia wasikilizaji wako wafikie kuamua mambo mu njia ya muzuri.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Tafuta na utumie habari zenye zinatokana na chanzo cha habari chenye kutegemeka. Toa maelezo yenye inategemea Neno la Mungu, soma moja kwa moja mu Biblia wakati inawezekana. Kama unazungumuzia habari ya sayansi, jambo lenye lilizungumuziwa ku radio, ku televizyo ao mu gazeti fulani, jambo lenye lilionwa, ao jambo lingine la kutegemeza habari yako, chunguza mbele ya wakati juu ya kuhakikisha kwamba chanzo cha habari yako ni chenye kutumainika na ni cha sasa.

  • Tumia muzuri habari zenye umepata. Fasiria andiko kulingana na maandiko yenye inatangulia na yenye inafuata ile andiko, kulingana na ujumbe wa Biblia, na kulingana na vichapo vya “mutumwa muaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45) Tumia maandishi yenye haizungumuzie mambo ya Biblia bila kubadilisha kitu na kulingana na wazo lenye muandikaji alitaka kusema.

  • Fikiri na wasikilizaji wako. Kisha kusoma andiko ao kutaja habari fulani, uliza maulizo fulani kwa busara ao toa mufano juu ya kusaidia wasikilizaji wako wafikie kuamua mambo wao wenyewe.