Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utangulizi wa Sehemu ya 12

Utangulizi wa Sehemu ya 12

Yesu alifundisha watu juu ya Ufalme wa mbinguni. Tena aliwaambia kama inafaa wakuwe wanasali jina la Mungu litakaswe, Ufalme wake ukuje, na mapenzi yake ifanyike ku dunia. Kama uko muzazi, saidia mutoto wako aelewe juu ya nini ile sala ni ya maana kwetu. Yesu hakuruhusu Shetani amufanye avunje ushikamanifu wake. Mitume, wenye Yesu alichaguaka njo washiriki wa kwanza wa Ufalme, na wako na kazi ya maana sana katika ule Ufalme. Onyesha mutoto wako kama Yesu alikuwa na bidii kwa ajili ya ibada safi. Kwa sababu alitaka kusaidia watu, Yesu aliponyesha wagonjwa, alipatia wenye kuwa na njaa chakula, na hata alifufua wafu. Kwa kufanya vile, alionyesha mambo yenye Ufalme utafanyia wanadamu.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 74

Yesu Anakuwa Masiya

Yohana anamaanisha nini wakati anasema kama Yesu njo Mwana-Kondoo wa Mungu?

SOMO LA 75

Ibilisi Anamujaribu Yesu

Ibilisi anamujaribu Yesu mara tatu. Anamujaribu namna gani? Yesu anatenda namna gani?

SOMO LA 76

Yesu Anasafisha Hekalu

Juu ya nini Yesu anafukuza wanyama inje ya hekalu na kupindua meza za wenye wako wanabadilisha feza?

SOMO LA 77

Mwanamuke Kwenye Kisima

Mwanamuke Musamaria anashangaa wakati Yesu anazungumuza naye. Juu ya nini? Yesu anamuambia jambo gani lenye alikuwa hajaambiaka mutu mwingine?

SOMO LA 78

Yesu Anahubiri Habari ya Ufalme

Yesu anaalika wanafunzi wake fulani wakuwe ‘wavuvi wa watu.’ Kisha, anachagua wafuasi 70 ili wahubiri habari njema.

SOMO LA 79

Yesu Anafanya Miujiza Mingi

Kila fasi kwenye Yesu anaenda, wagonjwa wanakuja kumuona juu awasaidie, na anawaponyesha. Hata anamufufua mutoto mwanamuke.

SOMO LA 80

Yesu Anachagua Mitume 12

Juu ya nini Yesu anawachagua? Unakumbuka majina yao?

SOMO LA 81

Mahubiri Kwenye Mulima

Yesu anafundisha watu mingi wenye walikusanyika pembeni ya mulima mambo ya maana sana.

SOMO LA 82

Yesu Anafundisha Wanafunzi Wake Namna ya Kusali

Yesu anawaambia wanafunzi wake waendelee kuomba mambo gani?

SOMO LA 83

Yesu Anakulisha Maelfu ya Watu

Huu muujiza unatufundisha nini juu ya Yehova na Yesu?

SOMO LA 84

Yesu Anatembea Juu ya Maji

Unaweza kuwazia namna mitume wanajisikia wakati wanaona ule muujiza?

SOMO LA 85

Yesu Anaponyesha Mutu Siku ya Sabato

Juu ya nini haiko watu wote njo wanafurahia mambo yenye Yesu iko anafanya?

SOMO LA 86

Yesu Anamufufua Lazaro

Wakati Yesu anaona namna Maria iko analia, yeye pia anaanza kulia. Lakini huzuni yao iligeuka kuwa furaha.