Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

74

Yesu Anakuwa Masiya

Yesu Anakuwa Masiya

Yohana alikuwa anahubiri hivi: ‘Mutu fulani mukubwa kuliko mimi anakuja.’ Wakati Yesu alikuwa na miaka 30 hivi, alitoka Galilaya na kuenda ku Muto Yordani, kwenye Yohana alikuwa anabatiza watu. Alipenda Yohana amubatize. Lakini Yohana alimuambia: ‘Haiko mimi njo ninapaswa kukubatiza. Wewe njo unapaswa kunibatiza.’ Yesu akamuambia: ‘Yehova anapenda wewe unibatize.’ Kwa hiyo, wakaingia katika Muto Yordani, na Yohana akazamisha Yesu ndani ya maji.

Kisha Yesu kutoka ndani ya maji, alisali. Palepale, mbingu zikafunguliwa, na roho ya Mungu ikashuka juu yake kama njiwa. Kisha sauti ya Yehova ikatoka mbinguni na kusema: “Wewe ni Mwana wangu, mupendwa; nimekukubali.”

Wakati roho ya Yehova ilishuka juu ya Yesu njo sasa akakuwa Kristo, ao Masiya. Sasa angeweza kuanza kazi yenye Yehova alimutuma afanye ku dunia.

Kisha tu kubatizwa, Yesu alienda mu jangwa. Alifanya kule siku 40. Wakati alitoka mu jangwa, akaenda kuona Yohana. Wakati Yesu alifika karibu na Yohana, Yohana akasema: ‘Huyu njo Mwana-Kondoo wa Mungu mwenye ataondoa zambi ya ulimwengu.’ Wakati Yohana alisema vile, alisaidia watu wajue kama Yesu njo Masiya. Je, unajua mambo yenye ilimufikiaka Yesu wakati alikuwa mu jangwa? Ile njo tutaona mu sura yenye kufuata.

“Sauti ikatokea mbinguni: ‘Wewe ni Mwana wangu, mupendwa; nimekukubali.’”​—Marko 1:11