Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

76

Yesu Anasafisha Hekalu

Yesu Anasafisha Hekalu

Yesu alienda Yerusalemu katika Mwezi wa 4 hivi mu mwaka wa 30. Watu mingi walikuwa wamekuja Yerusalemu kwa ajili ya Pasaka. Walikuwa wanatoa zabihu za wanyama ku hekalu, kama vile walizoea kufanya. Wamoja walikuja na wanyama wao, lakini wengine waliuza wanyama pale Yerusalemu.

Wakati Yesu alifika ku hekalu, aliona wafanyabiashara wako wanauzisha wanyama ndani ya hekalu. Walikuwa wanafanya biashara mu nyumba ya Yehova ya ibada! Yesu alifanya nini? Alitengeneza mujeledi wa kamba (fimbo ya kamba) na alifukuza kondoo na ngombe zenye zilikuwa mu hekalu. Alipindua meza za watu wenye walikuwa wanabadilisha feza na akamwanga chini feza zao za vichele. Yesu aliambia wale wenye walikuwa wanauzisha njiwa: ‘Mutoshe hivi vitu hapa! Muache kufanya nyumba ya Baba yangu kuwa nafasi ya biashara!’

Watu wenye walikuwa ku hekalu walishangaa kuona mambo yenye Yesu alifanya. Wanafunzi wake walikumbuka unabii fulani juu ya Masiya wenye unasema hivi: ‘Nitakuwa na bidii sana kwa ajili ya nyumba ya Yehova.’

Kisha wakati fulani, mu mwaka wa 33, Yesu alisafisha hekalu mara ya pili. Hakuruhusu mutu yeyote azarau nyumba ya Baba yake.

“Hamuwezi kuwa watumwa wa Mungu na wa Utajiri.”​—Luka 16:13