Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

92

Yesu Anawatokea Wavuvi

Yesu Anawatokea Wavuvi

Wakati fulani kisha Yesu kutokea mitume, Petro aliamua kuenda kuvua ao kuloa samaki mu Bahari ya Galilaya. Tomasi, Yakobo, Yohana, na wanafunzi wengine walimufuata. Walivua samaki usiku wote, lakini hawakupata kitu.

Siku yenye ilifuata, asubui sana, wakaona mwanaume mumoja amesimama pembeni ya bahari. Akawauliza: ‘Mulipata samaki?’ Wakamuambia, “Hapana!” Akasema, ‘Mutupe wavu (filet) ngambo ya kuume ya mashua.’ Wakati walifanya vile, wavu ukajaa samaki mupaka wakashindwa kuukokota. Palepale Yohana akatambua kama ule mwanaume ni Yesu na akasema: “Ni Bwana!” Mara moja, Petro akajitupa mu maji na akaogelea mupaka pembeni ya bahari. Wanafunzi wengine wakamufuata na mashua.

Wakati walifika pembeni ya bahari, wakaona mukate na samaki ku moto. Yesu akawaambia walete samaki fulani kati ya samaki wenye walivua. Kisha akawaambia: “Mukuje mukule.”

Kisha kula, Yesu akamuuliza Petro: ‘Unanipenda kupita kazi ya kuvua samaki?’ Petro akasema, “Ndiyo, Bwana, unajua kama ninakupenda.” Yesu akamuambia, ‘Basi lisha wana-kondoo wangu.’ Yesu akamuuliza tena: ‘Petro, unanipenda?’ Petro akasema, ‘Bwana, unajua kama ninakupenda.’ Yesu akamuambia, “Chunga kondoo wangu wadogo.” Yesu akamuuliza tena mara ya tatu. Petro akahuzunika sana. Akasema, “Bwana, unajua mambo yote; unajua kama ninakupenda.” Yesu akamuambia, “Lisha kondoo wangu wadogo.” Kisha akamuambia Petro: “Endelea kunifuata.”

“[Yesu] akawaambia: ‘Munifuate, na mimi nitawafanya ninyi kuwa wavuvi wa watu.’ Mara moja wakaacha nyavu zao na kumufuata.”​—Matayo 4:19, 20