Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

102

Yohana Anapokea Ufunuo

Yohana Anapokea Ufunuo

Wakati mutume Yohana alikuwa mufungwa mu kisiwa cha Patmo, Yesu alimuonyesha maono 16, ao picha ya mambo ya wakati wenye kuja. Ile maono ilionyesha vile jina la Yehova litatakaswa, vile Ufalme wake utakuja, na vile mapenzi yake itafanyika hapa ku dunia sawa vile mbinguni.

Katika maono fulani, Yohana alimuona Yehova amekaa kwenye kiti chake cha ufalme mbinguni. Wazee 24 walikuwa wamemuzunguka. Walikuwa wamevaa nguo za mweupe na mataji ya zahabu ilikuwa juu ya vichwa vyao. Mwangaza wa radi na sauti za mingurumo zilikuwa zinatoka mu kile kiti cha ufalme. Wale wazee 24 waliinama mbele ya Yehova na kumuabudu. Katika maono ingine, Yohana aliona kundi kubwa la watu wenye walikuwa wanamuabudu Yehova: walitoka mu mataifa yote na vikundi vyote vya watu, na luga zote. Mwana-Kondoo, ni kusema Yesu, alikuwa anawachunga na kuwapeleka kwenye maji ya uzima. Kisha, katika maono ingine, Yohana aliona Yesu anaanza kutawala mbinguni pamoja na wale wazee 24. Katika maono ingine, Yohana aliona Yesu iko anapigana na ule nyoka mukubwa, ni kusema Shetani, pamoja na pepo wake wachafu. Yesu aliwafukuza mbinguni na kuwatupa ku dunia.

Kisha Yohana aliona maono ya muzuri sana, mu ile maono aliona Mwana-Kondoo amesimama ku Mulima Sayuni na wale 144000. Tena, aliona malaika mwenye alikuwa anaruka mu dunia yote na iko anaambia watu wamuogope Mungu na kumupatia utukufu.

Katika maono ingine, Yohana aliona vita ya Armagedoni. Katika ile vita, Yesu na majeshi yake walipata ushindi juu ya ulimwengu mubaya wa Shetani. Mu maono ya mwisho, Yohana aliona umoja wa muzuri sana kati ya mbingu na dunia. Shetani na wote wenye kuwa upande wake waliharibiwa kabisa. Kisha, watu wote mbinguni na duniani walitukuza jina la Yehova na kumuabudu yeye peke yake.

“Na nitatia uadui kati yako na ule mwanamuke na kati ya uzao wako na uzao wake. Ataponda kichwa chako, na wewe utamupiga kwenye kisigino.”​—Mwanzo 3:15