Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

5

Safina ya Noa

Safina ya Noa

Watu waliendelea kuongezeka mu dunia na watu mingi kati yao walikuwa wanafanya mambo ya mubaya. Hata malaika fulani kule mbinguni walifikia kuwa wabaya. Walitoka mbinguni na kuja ku dunia. Unajua ni juu ya nini walifanya vile? Ni juu wavae mwili wa watu na kuoa wanamuke.

Malaika na wale wanamuke walizaa watoto wanaume. Wale watoto walikuwa wenye nguvu sana na walikuwa wanafanya mambo ya mubaya sana. Walitesa watu sana. Yehova hangeacha ile mambo iendelee. Njo maana aliamua kuharibu watu wabaya kupitia garika ao mvua kubwa.

Lakini kulikuwa mwanaume mumoja mwenye alikuwa mutu muzuri. Alimupenda Yehova. Aliitwa Noa. Alikuwa na bibi na watoto tatu, ni kusema, Shemu, Hamu, na Yafeti, na kila mutoto alikuwa na bibi. Yehova alimuambia Noa ajenge safina kubwa, ili yeye na familia yake wasikufe wakati wa Garika. Safina ni sanduku kubwa lenye linaweza kubakia juu ya maji. Tena, Yehova alimuambia Noa aingize wanyama ndani ya safina ili wasikufe wakati wa Garika.

Palepale, Noa alianza kujenga safina. Noa na familia yake walifanya miaka karibu 50 na wako wanajenga safina. Walijenga safina sawasawa na vile Yehova aliwaambia. Wakati walikuwa wanajenga, Noa aliambia watu kama mvua kubwa itanyesha. Lakini, watu hawakumusikiliza.

Kisha, wakati wa kuingia ndani ya safina ukafika. Acha tuone jambo lenye lilitokea kisha.

“Vile siku za Noa zilikuwa, ni vile kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakuwa.”​—Matayo 24:37