Utangulizi wa Sehemu ya 3
Biblia inazungumuzia watu kidogo sana wenye walimutumikia Yehova kisha Garika. Kwa mufano Abrahamu, mwenye alijulikana kuwa rafiki ya Yehova. Juu ya nini Yehova alimuita rafiki yake? Kama uko muzazi, fundisha mutoto wako kama Yehova anamupenda kabisa na anataka kumusaidia. Kama Abrahamu na wanaume wengine waaminifu, sawa vile Loti na Yakobo, tunaweza kumuomba Yehova kwa uhuru wote ili atusaidie. Tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatimiza mambo yote yenye anasema atafanya.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 7
Munara wa Babeli
Watu waliamua kujenga muji na munara wenye kufika mupaka mbinguni. Juu ya nini Mungu alifanya waseme luga za kuachana?
SOMO LA 8
Abrahamu na Sara Walimutii Mungu
Juu ya nini Abrahamu na Sara waliacha maisha yao ya muzuri na kuhamia mu inchi ya Kanaani?
SOMO LA 9
Wanapata Sasa Mutoto!
Namna gani Mungu alitimiza mambo yenye aliambia Abrahamu? Angefanya vile kupitia mutoto gani wa Abrahamu, Isaka ao Ishmaeli?
SOMO LA 10
Mukumbuke Bibi ya Loti
Mungu alifanya mvua ya moto na kiberiti inyeshe mu miji ya Sodoma na Gomora. Juu ya nini ile miji iliharibiwa? Juu ya nini tunapaswa kukumbuka bibi ya Loti?
SOMO LA 11
Imani Yake Inajaribiwa
Mungu aliambia Abrahamu: ‘Tafazali, ukamate mutoto wako wa pekee na umutoe zabihu ku mulima katika Moria.’ Namna gani Abrahamu alitenda mbele ya jaribu hilo la imani?
SOMO LA 12
Yakobo Alipata Uriti
Isaka na Rebeka walikuwa na watoto mapasa, Esau na Yakobo. Esau alizaliwa wa kwanza na yeye njo alipaswa kuwa na haki ya uriti. Juu ya nini aliuzisha ile haki kwa chakula?
SOMO LA 13
Yakobo na Esau Wanasikilizana
Namna gani malaika alimubariki Yakobo? Yakobo alifanya nini ili asikilizane na Esau?