Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

8

Abrahamu na Sara Walimutii Mungu

Abrahamu na Sara Walimutii Mungu

Muji wa Uru ulikuwa karibu na muji wa Babeli. Watu wa Uru waliabudu miungu mingi kuliko kumuabudu Yehova. Lakini kulikuwa mwanaume mumoja mwenye aliishi mu muji wa Uru, mwenye alimuabudu Yehova tu. Aliitwa Abrahamu.

Yehova alimuambia Abrahamu hivi: ‘Utoke mu inchi yako na uache watu wa jamaa yako, uende mu inchi yenye nitakuonyesha.’ Kisha Mungu alimupatia hii ahadi: ‘Nitakufanya ukuwe taifa kubwa, nitafanyia watu mambo ya muzuri mu dunia yote kwa sababu yako.’

Abrahamu hakujua kwenye Yehova alimuambia aende, lakini alimutumainia. Kwa hiyo Abrahamu, bibi yake Sara, baba yake Tera, na Loti, mutoto wa kaka yake, walitii, wakafunga mizigo na kuanza safari ya murefu.

Abrahamu alikuwa na miaka 75, wakati yeye na familia yake walifika mu inchi yenye Yehova alipenda kuwaonyesha. Ile inchi iliitwa Kanaani. Kule, Mungu alisema na Abrahamu na akamuambia hivi: ‘Nitapatia watoto wako hii inchi.’ Lakini Abrahamu na Sara walikuwa wazee na hawakukuwa na watoto. Basi, Yehova angetimiza ile maneno namna gani?

“Kwa imani, Abrahamu . . . alitii kwa kutoka na kuenda mahali kwenye angepokea kuwa uriti; alitoka, hata kama hakujua mahali alikuwa anaenda.”​—Waebrania 11:8