Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

10

Mukumbuke Bibi ya Loti

Mukumbuke Bibi ya Loti

Loti aliishi na Abrahamu, baba yake mudogo, mu inchi ya Kanaani. Kisha, Abrahamu na Loti wakakuwa na wanyama mingi. Lakini fasi ya kukulishia wanyama ikakuwa kidogo. Abrahamu aliambia Loti: ‘Hatuwezi tena kuishi pamoja hapa. Unaweza kuchagua kwenye unapenda kuenda na mimi nitaenda ngambo ingine.’ Abrahamu hakujipendelea, hauone vile?

Loti aliona fasi ya muzuri sana karibu na muji wenye kuitwa Sodoma. Kulikuwa maji mingi na majani ya mubichi. Basi akachagua ile fasi na akahamia kule na familia yake.

Watu wa Sodoma na Gomora walikuwa wabaya sana; Gomora ilikuwa pembeni ya Sodoma. Kusema kweli, walikuwa wabaya sana mupaka Yehova akaamua kuharibu ile miji. Lakini Mungu alipenda kuokoa Loti na familia yake. Alituma malaika wawili wawaambie: ‘Mufanye haraka! Mutoke katika muji huu! Yehova anataka kuuharibu!’

Loti hakutoka palepale. Aliendelea kukawia. Kwa hiyo malaika walikamata mukono wa Loti, wa bibi yake, na watoto wake wawili wanamuke na kuwapeleka inje ya muji, kisha wakawaambia: ‘Mukimbie ili musikufe! Musiangalie nyuma, mukiangalia nyuma mutakufa!’

Wakati walifika mu muji wa Soari, Yehova alifanya mvua ya moto na kiberiti inyeshe mu miji ya Sodoma na Gomora. Ile miji mbili iliharibiwa kabisa. Bibi ya Loti hakumutii Yehova, aliangalia nyuma na akakuwa nguzo ya chumvi! Lakini Loti na watoto wake wanamuke waliokoka kwa sababu walimutii Yehova. Walijisikia mubaya sana kwa sababu bibi ya Loti hakumutii Yehova. Lakini, walifurahi kwa sababu walisikiliza Yehova.

“Mukumbuke bibi ya Loti.”​—Luka 17:32