Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

17

Musa Alichagua Kumuabudu Yehova

Musa Alichagua Kumuabudu Yehova

Mu inchi ya Misri, watu wa familia ya Yakobo walikuwa wanaitwa Waisraeli. Kisha Yakobo na Yosefu kufa, Farao mwingine alianza kutawala. Aliogopa juu aliwaza kama Waisraeli wataongezeka na watakuwa na nguvu kupita Wamisri. Kwa hiyo, ule Farao alifanya Waisraeli kuwa watumwa. Aliwakaza kutengeneza matofali (briques) na kufanya kazi ya nguvu mu mashamba. Lakini hata kama Wamisri waliwakaza kufanya kazi ya nguvu, Waisraeli waliendelea kuongezeka. Kwa sababu Farao hakufurahia jambo hilo, alisema waue watoto wanaume wote Waisraeli wakati wanazaliwa. Waisraeli waliogopa sana, haiko vile?

Mwanamuke mumoja Mwisraeli mwenye aliitwa Yokebedi, alizaa mutoto mwanaume wa sura ya muzuri. Juu wasimuue, alimuweka mu kitunga, na akamuficha mu matete pembeni ya Muto Nile. Miriamu, dada ya ule mutoto, alibakia karibu na pale juu aone jambo lenye litatokea.

Binti ya Farao alienda kunawa ku muto na akaona kile kitunga. Mu kile kitunga, aliona mutoto iko analia, na akamusikilia huruma. Miriamu akamuuliza: ‘Nikutafutie mwanamuke mwenye atakunyonyeshea huyu mutoto?’ Wakati binti ya Farao aliitika, Miriamu akaleta Yokebedi, mama yake. Binti ya Farao akamuambia: ‘Kamata huyu mutoto, uanze kumunyonyesha, nitakulipa.’

Wakati ule mutoto alikomaa, Yokebedi akamuleta kwa binti ya Farao, naye akamupanga jina Musa na akamuchunga sawa vile mutoto wake. Walimukomalisha sawa vile mutoto wa mufalme na walimupatia kila kitu chenye alipenda. Lakini Musa hakusahau Yehova. Alijua kama yeye alikuwa Mwisraeli, hapana Mumisri. Na alichagua kumutumikia Yehova.

Wakati alikuwa na miaka 40, Musa alipenda kusaidia Waisraeli wenzake. Wakati aliona Mumisri iko anapiga mutumwa Mwisraeli, Musa alipiga sana ule Mumisri na kumuua. Kisha akamuficha mu muchanga. Wakati Farao alijua jambo hilo, alitafuta kumuua Musa. Lakini Musa akakimbilia mu inchi ya Midiani. Yehova alimuchunga wakati alikuwa kule.

“Kwa imani Musa, . . . alikataa kuitwa mwana wa binti ya Farao, akachagua kutendewa mubaya pamoja na watu wa Mungu.”​—Waebrania 11:24, 25