Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

14

Mutumwa Mwenye Alimutii Mungu

Mutumwa Mwenye Alimutii Mungu

Yosefu alikuwa kati ya watoto wa mwisho-mwisho wa Yakobo. Ndugu za Yosefu waliona kama Yosefu njo mwenye baba yao alikuwa anapenda sana. Unawaza ile ilifanya wajisikie namna gani? Walimusikilia Yosefu wivu na walimuchukia. Wakati Yosefu alilota ndoto za kushangaza, aliwaelezea zile ndoto. Waliwaza kama zile ndoto zinamaanisha kama siku moja watamuinamiaka. Na wakamuchukia tena sana!

Siku moja, ndugu za Yosefu walikuwa wanachunga kondoo karibu na muji wa Shekemu. Yakobo alituma Yosefu aende aone kama walikuwa namna gani. Waliona Yosefu kwa mbali, na wakaambiana: ‘Ule mulota-ndoto anakuja. Tumuue!’ Wakamukamata na kumutupa mu shimo ya murefu. Lakini Yuda, mumoja kati ya ndugu za Yosefu, akasema: ‘Musimuue! Lakini tumuuzishe akuwe mutumwa.’ Kwa hiyo, wakamuuzisha Yosefu kwa vipande 20 vya feza kwa wafanyabiashara Wamidiani wenye walikuwa wanaenda Misri.

Kisha, ndugu za Yosefu wakaingiza nguo yake ndani ya damu ya mbuzi, wakaipeleka kwa baba yao na kusema: ‘Hii, haiko nguo ya mutoto wako?’ Na Yakobo akawaza kama munyama wa pori alikuwa ameua Yosefu. Yakobo alihuzunika sana. Hakuna mutu mwenye aliweza kumufariji.

Wakati alifika Misri, Yosefu aliuzishwa akuwe mutumwa wa mutu mwenye cheo cha juu mwenye aliitwa Potifa. Lakini Yehova alikuwa pamoja na Yosefu. Potifa aliona kama Yosefu alifanya kazi muzuri na alimutumainia. Kisha, Potifa akamufanya asimamie vitu vyake vyote.

Bibi ya Potifa aliona kama Yosefu alikuwa na sura ya muzuri na nguvu ya mingi. Kila siku alikuwa anaambia Yosefu alale naye. Yosefu alifanya nini? Alikataa na kusema: ‘Hapana! Ni kosa kufanya vile. Bwana wangu ananitumainia, na wewe uko bibi yake. Nikilala na wewe, nitamutendea Mungu zambi!’

Siku moja, bibi ya Potifa alijaribu kumukaza Yosefu alale naye. Alimukamata ku nguo, lakini Yosefu akakimbia. Wakati Potifa alirudia kwake, bibi yake alimuambia kama Yosefu alitaka kulala naye. Alisema uongo. Potifa alikasirika sana na kumutupa Yosefu mu gereza. Lakini Yehova hakusahau Yosefu.

“Kwa hiyo, mujinyenyekeze chini ya mukono wenye nguvu wa Mungu, ili awainue ninyi katika wakati wenye kufaa.”​—1 Petro 5:6