Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

24

Walishindwa Kutimiza Ahadi Yao

Walishindwa Kutimiza Ahadi Yao

Yehova aliambia Musa hivi: ‘Panda kwenye mulima, tukutane. Nitaandika sheria zangu juu ya mabamba ya majiwe, kisha nitakupatia.’ Musa akapanda ku mulima na kukaa kule siku 40 muchana na usiku. Wakati alikuwa kule, Yehova aliandika zile Amri Kumi juu ya mabamba mbili ya majiwe na akamupatia Musa ile mabamba.

Kisha wakati fulani, Waisraeli wakawaza kama Musa amewaacha. Wakaambia Haruni: ‘Tunataka mutu wa kutuongoza. Ututengenezee mungu!’ Haruni akasema: ‘Munipatie zahabu yenu.’ Akayeyusha ile zahabu na kutengeneza sanamu ya kitoto-dume cha ngombe. Watu wakasema: ‘Huyu njo Mungu mwenye alitutosha Misri.’ Wakaanza kuabudu ile sanamu ya zahabu na wakafanya karamu. Kufanya vile ilikuwa mubaya? Ndiyo, kwa sababu wale watu walitoaka ahadi kama watamuabudu Yehova tu. Lakini sasa walishindwa kutimiza ahadi yao.

Yehova aliona ile mambo, na akaambia Musa: ‘Shuka urudie kwenye watu wako. Hawanitii na wanaabudu mungu wa uongo.’ Musa akashuka mbio kutoka ku mulima, na alikuwa anabeba ile mabamba mbili.

Wakati Musa alikaribia kambi alisikia watu wako wanaimba. Kisha akawaona wako wanacheza na kuinamia ile sanamu ya kitoto-dume cha ngombe. Musa alikasirika sana. Alitupa ile mabamba mbili chini na ikavunjika vipande-vipande. Palepale akaharibu ile sanamu. Kisha akauliza Haruni: ‘Hawa watu walikuambia nini juu uitike kufanya hili jambo la mubaya sana?’ Haruni akasema: ‘Usikasirike. Unajua vile hawa watu wanakuwaka. Walitaka niwatengenezee mungu, kwa hiyo nikatupa zahabu yao katika moto na ile sanamu ya kitoto-dume cha ngombe ikatokea!’ Haruni hakupaswa kufanya vile. Musa akarudia ku mulima na kumubembeleza Yehova asamehe wale watu.

Yehova alisamehe wale wenye walikuwa tayari kumutii. Hauone kama ilikuwa jambo la maana Waisraeli waache Musa awaongoze?

“Kila mara wakati unaweka naziri kwa Mungu, usikawie kuitimiza, kwa maana hafurahie wajinga. Naziri yenye unaweka, uitimize.”​—Muhubiri 5:4