Utangulizi wa Sehemu ya 6
Wakati Waisraeli walifika mu Inchi ya Ahadi, tabenakulo ikakuwa nafasi kubwa ya ibada ya kweli. Makuhani walifundisha watu Sheria, na waamuzi waliongoza taifa. Hii sehemu inaonyesha namna maamuzi na matendo ya mutu inaweza kuchochea sana wengine wafanye mambo ya muzuri ao ya mubaya. Kila Mwisraeli alipaswa kuwa muaminifu kwa Yehova na kwa watu wengine. Inaonyesha namna Debora, Naomi, Yoshua, Hana, binti ya Yefta, na Samweli walikuwa mifano ya muzuri kwa wengine. Inaonyesha tena kama hata watu fulani wenye hawakukuwa Waisraeli, kama vile Rahabu, Rutu, Yaeli, na Wagibeoni walichagua kuwa upande wa Waisraeli kwa sababu walitambua kama Mungu alikuwa pamoja nao.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 30
Rahabu Alificha Wapelelezi
Kuta za Yeriko zilianguka. Lakini nyumba ya Rahabu haikuanguka, hata kama ilikuwa imejengwa ku ukuta.
SOMO LA 31
Yoshua na Wagibeoni
Yoshua alisali kwa Mungu na kusema: “Jua, simama bila kutikisika!” Je, Mungu alijibu?
SOMO LA 32
Kiongozi Mupya na Wanamuke Mbili Wenye Uhodari
Kisha Yoshua kufa, Waisraeli walianza kuabudu sanamu. Maisha ilikuwa nguvu, lakini Yehova aliwasaidia kupitia muamuzi Baraka, nabii mwanamuke Debora, na Yaeli!
SOMO LA 33
Rutu na Naomi
Wanamuke wawili wenye bwana zao walikufa walirudia Israeli. Rutu, mumoja kati ya wale wanamuke, alienda kufanya kazi mu shamba, na kule Boazi akamuona.
SOMO LA 34
Gideoni Alishinda Wamidiani
Kisha Wamidiani kutesa Waisraeli, watu walianza kumulilia Yehova awasaidie. Namna gani maaskari kidogo wa Gideoni waliweza kushinda maaskari 135000 Wamidiani?
SOMO LA 35
Hana Anasali Apate Mutoto Mwanaume
Elkana, Hana, Penina, na watoto wao walienda kuabudu ku tabenakulo kule Shilo. Wakati wako kule, Hana anasali apate mutoto. Mwaka wa kufuata, Samweli anazaliwa!
SOMO LA 36
Ahadi ya Yefta
Yefta alitoa ahadi gani, na juu ya nini? Binti ya Yefta alifanya nini kisha kujua ahadi ya baba yake?
SOMO LA 37
Yehova Anazungumuza na Samweli
Kuhani Mukubwa Eli alikuwa na watoto mbili wanaume wenye walikuwa makuhani ku tabenakulo, lakini hawakutii sheria za Yehova. Kijana Samweli hakukuwa vile, na Yehova alizungumuza naye.
SOMO LA 38
Yehova Alipatia Samsoni Nguvu
Mungu alipatia Samsoni nguvu mingi juu apigane na Wafilisti, lakini wakati Samsoni alikamata uamuzi wa mubaya, Wafilisti walimukamata.