Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

53

Yehoyada Anatenda kwa Uhodari

Yehoyada Anatenda kwa Uhodari

Yezebeli alikuwa na mutoto mwanamuke, jina lake Atalia. Ule Atalia alikuwa mubaya sana sawa tu mama yake. Atalia alikuwa bibi ya mufalme wa Yuda. Wakati bwana yake alikufa, mutoto wake mwanaume alianza kutawala. Kisha ule mutoto akakufa, na Atalia akajifanya kuwa mutawala wa Yuda. Kisha alijaribu kuua watu wote wenye wangeweza kutawala pa nafasi yake. Aliua watoto wote wanaume wa mu familia ya kifalme, hata wajukuu wake. Kwa hiyo kila mutu alimuogopa.

Kuhani Mukubwa Yehoyada na bibi yake, Yehosheba, walijua kama jambo lenye Atalia alikuwa anafanya lilikuwa la mubaya sana. Kwa hiyo, walitia uzima wao mu hatari juu wafiche mujukuu mumoja kati ya wajukuu wa Atalia, mwenye alikuwa angali mudogo sana. Jina lake lilikuwa Yehoashi. Walimukomalishia mu hekalu.

Wakati Yehoashi alikuwa na miaka saba, Yehoyada alikusanya wakubwa na Walawi na kuwaambia hivi: ‘Mulinde milango ya hekalu na musiache mutu aingie.’ Kisha Yehoyada akafanya Yehoashi kuwa mufalme wa Yuda na akamuvalisha taji ku kichwa. Watu wa Yuda wakasema hivi kwa sauti: ‘Mufalme aishi siku mingi!’

Wakati Atalia alisikia sauti za watu, akaenda mara moja ku hekalu. Wakati aliona mufalme wa mupya, akalalamika: “Ni mupango mubaya! Ni mupango mubaya!” Wakubwa wakakamata Atalia, malkia mubaya, wakamutosha mu hekalu na wakamuua. Lakini, kwa miaka mingi, Atalia alikuwa mufano mubaya kwa taifa. Kungetokea nini sasa?

Yehoyada alisaidia wakaaji wa Yuda wafanye agano na Yehova, na walimutolea ahadi kama yeye tu njo wataabudu. Yehoyada aliwaambia wabomoe hekalu ya Baali na waharibu sanamu zote. Kisha, aliweka makuhani na Walawi watumike ku hekalu ili watu waanze tena kumuabudu Yehova kule. Aliweka watunza-milango wachunge milango ili mutu mwenye haiko safi asiingie. Kisha Yehoyada na wakubwa walipeleka Yehoashi ku nyumba ya mufalme na kumuikalisha ku kiti cha ufalme. Watu wa Yuda walifurahi sana. Sasa, Atalia hakukuwa tena na ibada ya Baali haikukuwa tena, kwa hiyo wangeweza kumutumikia Yehova muzuri. Hauone kama Yehoyada alisaidia watu mingi kwa sababu alitenda kwa uhodari?

“Musiogope wale wenye wanaua mwili lakini hawawezi kuua nafsi; lakini, muogope ule mwenye anaweza kuharibu vyote viwili, nafsi na mwili katika Gehena.”​—Matayo 10:28