Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KUANZISHA MAZUNGUMUZO

SOMO YA 2

Kuzungumuza kwa Njia ya Kawaida

Kuzungumuza kwa Njia ya Kawaida

Kanuni: “Neno lenye kusemwa wakati wenye kufaa​—ni la muzuri sana!”​—Mez. 15:23.

Mambo Yenye Filipo Alifanya

1. Angalia VIDEO, ao usome Matendo 8:30, 31. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1.    Namna gani Filipo alianzisha mazungumuzo?

  2.   Nini njo inaonyesha kama Filipo alianzisha mazungumuzo na kumufundisha ule mwanaume kweli ya Biblia mu njia ya kawaida?

Mufano wa Filipo Unatufundisha Nini?

2. Kama tunazungumuza na mutu mu njia ya kawaida, ile itafanya ule mutu akuwe mwenye kutulia na afurahie kutusikiliza.

Umuige Filipo

3. Ukuwe muangalifu. Namna mutu anaonekana inaweza kutusaidia kujua mambo ya mingi juu yake. Vile unamuona ule mutu, iko tayari kuongea na weye? Pengine unaweza kuzungumuza naye habari fulani ya Biblia kwa kumuuliza tu “Unajuaka kama . . . ?” Usilazimishe mutu aongee na weye kama hapendi.

4. Ukuwe muvumilivu. Usiwaze kama wakati unaanza tu kuongea na mutu unapaswa kumuambia palepale kweli fulani ya Biblia. Muendelee tu na mazungumuzo; kuko saa nafasi itajitokeza, yenye unaweza kuingiza wazo fulani ya Biblia mu njia ya kawaida. Wakati fulani inaweza kuomba ungoye mupaka wakati mutazungumuza tena na ule mutu.

5. Ujipatanishe na hali. Wakati fulani musikilizaji anaweza kusema mambo yenye haukutazamia. Kama ni vile, unapaswa kuzungumuzia naye habari fulani yenye itapatana na mambo yenye alisema, hata kama ile habari haiko njo yenye ulipanga kuzungumza naye.