Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Matangazo

Matangazo

Matangazo

MUKUTANO WA PEKEE

MASOMO KWA AJILI YA WAENEZA-INJILI WA UFALME Mapainia wenye kuwa na miaka 23 mupaka 65 wenye wanafurahia kupanua utumishi wao, wanaalikwa kuhuzuria mukutano wa wale wenye wanataka kufuata Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme Siku ya Yenga kisha midi. Mahali na saa ya mukutano huo vitatangazwa.

MATANGAZO

WAKARIBISHAJI Ndugu wenye kukaribisha watu wako tayari kukusaidia. Tafazali, uwasikilize na ufuate maagizo yao kuhusu mahali pa kuweka motokari, mahali pa kuingilia na kutokea, ao maagizo kuhusu kuchungia wengine viti, na mambo mengine.

UBATIZO Ikiwa hakuna mabadiliko yoyote, viti vya mbele ya jukwaa vitatayarishwa kwa ajili ya wale wenye watabatizwa. Wale wenye watabatizwa wanapaswa kukaa hapo Siku ya Posho asubui mbele hotuba ya ubatizo ianze. Kila mumoja wao anapaswa kuwa na nguo ya kujipanguza nayo maji na mavazi yenye kustahili ya kubatizwa nayo.

MICHANGO Tumetumia feza nyingi ili tupate mahali pazuri pa kufanyia mukusanyiko wetu, tupate vyombo vizuri vya sauti na vya video, na kufanya mambo mengine ili tufurahie mukusanyiko wetu na kutusaidia tumukaribie Yehova zaidi. Michango yenu ya kujipendea inasaidia kulipia mambo hayo yote na kutegemeza kazi ya duniani pote. Visanduku vya michango vyenye kuonekana wazi vinapatikana nafasi mbalimbali mahali hapa. Tunapendezwa sana na michango yote yenye munatoa. Baraza Lenye Kuongoza linawashukuru kwa michango yenye munatoa kwa moyo wote ili kutegemeza faida za Ufalme.

MATUNZO YA KWANZA Tafazali, ukumbuke kwamba biro hii inatoa MATUNZO YA HARAKA TU.

VITU VYENYE VILIOKOTWA Vitu vyote vyenye viliokotwa vinapaswa kupelekwa kwenye biro hii. Kama umepoteza kitu fulani, enda kwenye biro hiyo ili uone kama kimeokotwa. Ukimuona mutoto mwenye amepotea wazazi wake, umupeleke kwenye biro hiyo. Lakini, ili kuepuka wasiwasi wenye hauna na maana kwetu wote, tafazali muchunge watoto wenu na mukae pamoja nao.

VITI Tafazali, ufikirie wengine. Kumbuka kama unaweza kuchunga viti kwa ajili tu ya watu wa familia yako, watu wenye umekuja nao katika motokari moja, watu wenye unakaa nao katika nyumba moja, ao watu wenye unajifunza nao Biblia kwa sasa. Tafazali, usitie vitu kwenye viti vyenye hauchungiane.

KAZI YA KUJITOLEA Kama unataka kujitolea ili kusaidia kufanya kazi kwenye mukusanyiko, tafazali ujulishe ndugu wenye kusimamia biro hii.

“UKUWE HODARI”!

Mukusanyiko wa Mashahidi wa Yehova wa 2018

Umetayarishwa na Baraza Lenye Kuongoza la Mashahidi wa Yehova