Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Dunia Itakuwa Paradiso

Dunia Itakuwa Paradiso

Yehova atatosha mambo yote ya mubaya yenye Shetani amefanya. Yehova amefanya Yesu kuwa Mufalme wa dunia yote. Wakati Yesu atatawala dunia, dunia yote itakuwa paradiso.—Danieli 7:13, 14; Luka 23:43.

Yehova anasema kama atafanya hii mambo:

  • KUTAKUWA CHAKULA YA MINGI: “Dunia itatoa mazao yake; Mungu, Mungu wetu, atatubariki.” “Kutakuwa nafaka nyingi juu ya dunia; itajaa sana kwenye kichwa cha milima.”—Zaburi 67:6; 72:16.

  • HAKUTAKUWA VITA: “Mukuje na mujionee matendo ya Yehova,namna amefanya mambo yenye kushangaza katika dunia. Anamaliza vita katika dunia yote.”—Zaburi 46:8, 9.

  • HAKUTAKUWA WATU WABAYA: “Kwa maana waovu wataharibiwa. . . Kunabakia wakati kidogo tu, waovu hawatakuwa tena; utaangalia mahali walikuwa, nao hawatakuwa pale.”—Zaburi 37:9, 10.

  • HAKUTAKUWA MAGONJWA, HUZUNI, AO KIFO: “Wakati huo macho ya vipofu yatafunguliwa, na masikio ya viziwi yatafunguliwa. Wakati huo kilema wa miguu ataruka-ruka kama paa na ulimi wa bubu utapiga vigelegele vya shangwe.”—Isaya 35:5, 6.

    “Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Na atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena. Mambo ya zamani yamepita kabisa.”—Ufunuo 21:3, 4.

Yehova hasemake uongo hata kidogo. Haiko sawa Shetani na mashetani wake. Mambo yote yenye anasema, anaifanyaka. (Luka 1:36, 37) Yehova anakupenda na anataka uishi mu Paradiso yenye ataleta. Zungumuza na Mashahidi wa Yehova juu wakusaidie kujua mambo ingine ya muzuri yenye inapatikana mu Neno ya Mungu. Ukitumikisha mafundisho ya Biblia mu maisha yako, hautakuwa tena mutumwa wa mafundisho ya uongo, ushirikina, na mambo ya kuwazia-wazia. Na mu siku zenye ziko nakuya, utakombolewa kutoka mu utumwa wa zambi na kifo. Sawa vile Yesu alisema: “Utajua kweli, na kweli itakuweka huru.’—Yohana 8:32.