Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Roho Hawako Watu Wenye Waliishi ku Dunia Kisha Wakakufa

Roho Hawako Watu Wenye Waliishi ku Dunia Kisha Wakakufa

Roho wanakuwaka! Mu makao ya roho yenye haionekanake, kuko roho wazuri na roho wabaya. Wale roho ni watu wenye waliishi ku dunia kisha wakakufa?

Hapana. Wakati mutu anakufa, haendake kuishi mu makao fulani ya roho sawa vile watu wengi wanawazaka. Nini njo inatusaidia kujua vile? Mambo yenye Biblia inasema. Biblia ni kitabu yenye inasemaka kweli na mwenye aliiandikishaka ni Mungu wa kweli, mwenye jina yake ni Yehova. Yehova njo aliumbaka wanadamu, njo maana anajua kama wanakuwaka mu hali gani wakati wanakufa.​—Zaburi 83:18; 2 Timoteo 3:16.

Adamu alitoka mu mavumbi, na alirudia mu mavumbi

Biblia inasema kama Mungu alifanya Adamu, mutu wa kwanza, “kutoka katika mavumbi ya udongo.” (Mwanzo 2:7) Mungu alimuweka mu bustani ya Edeni, yenye ilikuwa paradiso. Kama Adamu angetii sheria ya Yehova, hangekufaka, na hata leo angekuwa angali muzima hapa ku dunia. Lakini wakati Adamu alivunja sheria ya Mungu kimakusudi, Mungu alimuambia hivi: “Utarudia katika udongo, kwa maana ulitoshwa katika udongo. Kwa maana wewe ni mavumbi na utarudia katika mavumbi.”​—Mwanzo 3:19.

Ile inamaanisha nini? Adamu alikuwaka wapi mbele Yehova amuumbe kwa kutumia mavumbi? Hakukuwaka fasi. Hakukuwaka kiumbe wa roho kule mbinguni. Hakukuwaka tu. Kwa hiyo, wakati Yehova alisema kama Adamu ‘atarudia katika mavumbi,’ alimaanisha kama Adamu atakufa. Hakuenda kuishi mu makao ya roho. Wakati Adamu alikufa, hakukuwa tena muzima, hakukuwa tena. Wakati mutu anakufa ni kusema haiko tena muzima.

Halafu watu wengine wenye walishakakufa? Ni kusema wao pia hawako fasi yoyote? Ona vile Biblia inasema:

  • “Wote [wanadamu na wanyama] wanaenda mahali palepale. Wote wanatoka katika mavumbi, na wote wanarudia katika mavumbi.”​—Muhubiri 3:20.

  • “Wafu hawajue kitu chochote.”​—Muhubiri 9:5.

  • “Upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari vimepotea.”​—Muhubiri 9:6.

  • “Hakuna kazi wala mipango wala ujuzi wala hekima katika kaburi, mahali unaenda.”​—Muhubiri 9:10.

  • “[Mwanadamu] anarudia kwenye udongo; siku ileile mawazo yake yanapotea.”​—Zaburi 146:4.

Ni wazima tu njo wanaweza kufanya hii mambo

Unaona kama ni nguvu kuamini mambo yenye ile maandiko inasema? Kama ni vile, fikiria hii jambo: Mu familia za mingi, mwanaume njo anatumikaka juu apate makuta ya kusaidia familia yake. Kama anakufa, mara mingi watu wa familia yake wanatesekaka sana. Wakati fulani, bibi yake na watoto wake wanakosaka hata makuta ya kuuza chakula. Na pengine watu wenye walikuwa namuchukia, wanaweza hata kutendea bibi na watoto wake mubaya. Sasa ujiulize hivi: Kama ule mwanaume iko naishi mu makao ya roho, juu ya nini haendelee kusaidia familia yake? Juu ya nini halinde familia yake juu watu wasiwatendee mubaya?’ Ni juu maandiko inasema kweli. Ule mwanaume haiko tena muzima, hawezi kufanya kitu.​—Zaburi 115:17.

Wafu hawawezi kusaidia watu wenye wako na njala, ao kulinda wenye kutendewa mubaya

Ni kusema watu wenye walishakufa, hawawezi ishi tena? Hapana. Tutazungumuzia ufufuo mu sehemu za mwisho-mwisho za hii broshua. Lakini ujue kama wafu hawajue mambo yenye uko nafanya. Hawawezi kukuona, kukusikia, kuzungumuza na weye, ao kukusaidia. Na haupaswe kuwaogopa juu hawawezi kukutendea mubaya.​—Muhubiri 9:4; Isaya 26:14.