Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mambo Itakuwa Muzuri mu Siku Zenye Ziko Nakuya

Mambo Itakuwa Muzuri mu Siku Zenye Ziko Nakuya

Mu siku zenye ziko nakuya Shetani na mashetani wake watafungwa

Shetani na mashetani wake hawatadanganya wanadamu milele. Yehova alishawafukuza mbinguni. (Ufunuo 12:9) Mu siku zenye ziko nakuya, Yehova Mungu atafunga Shetani na mashetani wake. Kisha kuona maono kutoka kwa Mungu, mutume Yohana alisema hivi juu ya ile jambo: “Na nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni akiwa na funguo ya abiso na munyororo mukubwa katika mukono wake. Akamukamata ule nyoka mukubwa, ule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, na akamufunga kwa miaka elfu moja (1 000). Na akamutupa ndani ya abiso na kuifunga na kutia muhuri juu yake, ili asipotoshe mataifa tena mupaka wakati ile miaka elfu moja (1 000) itaisha.” (Ufunuo 20:1-3) Na kisha, Shetani na mashetani wake wataharibiwa milele.—Ufunuo 20:10.

Watu wabaya nao wataharibiwa.—Zaburi 37:9, 10; Luka 13:5.

Wafu Wataishi Tena!

Wafu watafufuliwa hapa ku dunia

Kisha Shetani na mashetani wake kufungwa, Yehova ataletea wanadamu baraka za mingi. Unakumbuka tuliona kama wafu hawako tena. Hawaishi fasi fulani. Yesu alisema kama kifo iko sawa vile usingizi, usingizi wa sana wa bila kulota. (Yohana 11:11-14) Alisema vile juu alijua kama wale wenye wamekufa wataamuka tena na kuishi. Alisema hivi: “Saa inakuja yenye wale wote wenye kuwa katika makaburi ya ukumbusho . . . watatoka.”—Yohana 5:28, 29; linganisha na Matendo 24:15.

Watafufuliwa hapa ku dunia. Matangazo ya kifo haitakuwa tena. Lakini tutasikia njo habari za kufurahisha za wale wenye wamefufuliwa! Tutafurahia sana kukaribisha wapendwa wetu wenye watafufuliwa!