Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kuko Mamilioni ya Viumbe wa Roho

Kuko Mamilioni ya Viumbe wa Roho

Biblia inasema kama kuko watu wengi sana wenye kuwa na mwili wa roho. Hata Yehova ni roho.​—Yohana 4:24; 2 Wakorinto 3:17, 18.

Wakati fulani Yehova alikuwaka yeye peke mu ulimwengu. Kisha akaanza kuumba watu wenye kuwa na mwili wa roho, wenye wanaitwa malaika. Wako na nguvu mingi na akili mingi kupita wanadamu. Yehova aliumba malaika wengi sana. Mutumishi wa Mungu, mwenye kuitwa Danieli, aliona mu maono mamia ya mamilioni ya malaika.​—Danieli 7:10; Waebrania 1:7.

Mungu aliumbaka wale malaika mbele hata aumbe dunia. (Yobu 38:4-7) Kati ya wale malaika hakuna mwenye alikuwaka naishi kwanza ku dunia sawa mwanadamu, kisha akakufa na kuwa kiumbe wa roho.

Yehova, Roho mwenye uwezo zaidi, aliumba mamilioni ya viumbe wa roho