Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mashetani Wanachochea Watu Wasimutii Mungu

Mashetani Wanachochea Watu Wasimutii Mungu

Desturi fulani zinatokana na wazo ya uongo yenye kuonyesha kama wafu wanaweza kutuona

Juu ya nini Shetani na pepo wachafu wanajikazaka sana kudanganya watu? Juu wanapenda na siye tusimutii Mungu. Wanapenda tuwaabudu. Na wanapenda tuamini mambo yao ya uongo na tufanye mambo yenye Yehova anachukia. Kwa mufano, wanapenda tujiingize mu desturi zenye zinahusu wafu.

Wakati mutu mwenye tunapenda anakufa, tunahuzunikaka sana. Ni kawaida kusijikia vile, na haiko mubaya. Hata Yesu “alitokwa na machozi” wakati rafiki yake Lazaro alikufa.​—Yohana 11:35.

Kuko desturi za mingi zenye watu wanafanyaka kisha mutu kufa. Na kila watu wako na desturi zao zenye wanafanyaka. Za mingi hazivunje kanuni za Biblia. Lakini, kuko desturi zenye zinatokana na wazo yenye kuonyesha kama wafu wako naishi, na kama wanaweza kuona watu wenye wangali wazima. Kwa mufano, kukesha, kuomboleza kupita kiasi, na maziko ya ajabu-ajabu. Watu wanawaza kuwa kama hawafanye ile mambo, roho za wafu zitakasirika. Lakini juu “wafu hawajue kitu chochote,” wale wenye kufanya ile mambo wako njo naunga mukono uongo wa Shetani.​—Muhubiri 9:5.

Desturi zingine zinatokana na wazo ya uongo yenye kuonyesha kama wafu wako na lazima ya musaada wetu

Desturi zingine zinatokana na wazo yenye kuonyesha kama wafu wako na lazima ya musaada ya watu wenye wangali wazima. Na kama watu wenye wangali wazima hawawasaidie, wafu wanaweza kuwafanyia mambo ya mubaya. Mu inchi fulani, siku 40 ao mwaka moja kisha mutu kufa, watu wanafanyaka karamu ao kutoa zabihu. Wanawazaka kama wakati wanafanya vile, wanasaidia mutu mwenye alikufa avuke na kuingia mu makao ya roho. Desturi ingine yenye watu wanazoea kufanya ni kutolea wafu chakula na kinywaji.

Zile desturi zote ni za mubaya juu zinaunga mukono uongo wa Shetani kuhusu wafu. Yehova hapendi tujiingize hata kidogo mu desturi zenye zinatokana na mafundisho ya mashetani!​—2 Wakorinto 6:14-18.

Watumishi wa Mungu wa kweli hawajiingizake hata kidogo mu desturi zenye zinaunga mukono uongo wa Shetani. Lakini juu wanapenda watu, wanajikazaka kusaidia wale wenye wangali wazima na kuwafariji. Wanajua kama ikiwa mutu alishakufa, Yehova tu njo anaweza kumusaidia.​—Yobu 14:14, 15.

Mungu Anakataza Kuzungumuza na Pepo Wachafu

Watu fulani wanazungumuzaka na pepo wachafu moja kwa moja ao kupitia muchawi. Kwa mufano, watu wanazungumuzaka na pepo wachafu kwa kufanya mambo sawa vile uchawi, ulozi, kutabiri matukio, na kutafuta habari kutoka kwa wafu.

Mungu anachukia zile desturi zote. Anapenda tushikamane na yeye tu.—Kutoka 20:5

Biblia inakataza ile mambo yote. Inasema hivi: “Asipatikane katikati yako mutu yeyote . . . mwenye kufanya uaguzi, mutu yeyote mwenye kufanya uchawi, mutu yeyote mwenye kutafuta alama za mambo yenye yatatokea, mulozi, mutu yeyote mwenye anafunga wengine kwa uchawi, mutu yeyote mwenye anatafuta shauri kwa mutu mwenye kupashana habari na pepo wachafu ao mutu mwenye kutabiri matukio, ao mutu yeyote mwenye kuuliza habari kwa wafu. Kwa maana kila mutu mwenye kufanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova.”​—Kumbukumbu la Torati 18:10-12.

Juu ya nini Yehova anakataza kabisa ile mambo?

Juu Yehova anatupenda, anatuambia tusijiingize mu desturi yoyote ya kuzungumuza na pepo wachafu. Anapenda watu na anawahangaikia. Anajua kama wale wenye wanazungumuza na pepo wachafu watapata tu magumu.

Kwa mufano, Nilda, wa Brazili, alikuwa anazoea kuzungumuza na mashetani. Mashetani walimutesa sana. Anasema hivi: “Mashetani . . . walinitawala; walikuwa wananiambia mambo ya kufanya. Wakati fulani nilikuwa na ufahamu, lakini wakati ingine nilikuwa napoteza ufahamu. Na nilipangishwa ku hopitale juu ya matatizo ya akili. Wale mashetani walinitesa sana mupaka mishipa yangu ya ubongo haikukuwa natumika tena muzuri. Nilikuwa nakunywa madawa ya kunituliza na nikaanza kunywa pombe na kuvuta kila wakati. Ile hali iliendelea miaka mingi.”

Mara mingi, wale wenye wanazungumuzaka na pepo wachafu wanatesekaka sana. Wanaweza kupoteza nyumba yao, uhuru wao, na hata maisha yao

Kisha wakati fulani, kwa musaada wa Yehova na wa Mashahidi wake hapa ku dunia, Nilda aliachana kabisa na pepo wachafu, na sasa iko na maisha ya muzuri. Anasema hivi: “Ninashauria watu wote, wasipime hata kidogo kujiingiza mu mambo ya pepo wachafu.”