Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mashetani Wanafanya Ionekane Kama Wafu Wako Naishi

Mashetani Wanafanya Ionekane Kama Wafu Wako Naishi

Biblia inasema kama Shetani iko “anapotosha dunia yote yenye kuikaliwa na watu.” (Ufunuo 12:9) Shetani na pepo wake wachafu hawapendi tuamini mambo yenye Biblia inasema. Wanajaribu kufanya watu waamini kama wafu wako naishi fasi fulani mu makao ya roho. Tuone namna wanafanyaka vile.

Wanatumia Dini ya Uongo

Watu, wanyama, samaki, na ndege wote ni nafsi

Dini za mingi zinafundishaka kama kila mwanadamu iko na nafsi yenye inaendaka kuishi mu makao ya roho wakati mwili inakufa. Wanasemaka kama mwili inakufaka lakini nafsi haikufake. Na wanasemaka kama nafsi haiwezi kufa.

Lakini Biblia haifundishe vile. Biblia inaonyesha kama nafsi njo mutu, hapana kitu yenye iko ndani ya mutu. Kwa mufano, wakati Biblia inazungumuzia namna Adamu aliumbwa, inasema hivi: “Na Yehova Mungu akaumba mwanadamu kutoka katika mavumbi ya udongo na akapuliza katika matundu ya pua yake pumuzi ya uzima, na mwanadamu akakuwa nafsi yenye uzima.” (Mwanzo 2:7, maelezo ya chini) Ni kusema, Mungu hakupatia Adamu nafsi; Adamu njo alikuwa nafsi.

Wanyama wanaitwa pia nafsi.​—Mwanzo 1:20, 21, 24, 30.

Mu Biblia, neno “nafsi” inamaanisha mutu yeye mwenyewe, njo maana hatuwezi kushangala wakati Biblia inasema kama nafsi inakufaka. Maandiko fulani ya Biblia inasema hivi:

  • “Nafsi yenye inatenda zambi ndiyo itakufa.”​—Ezekieli 18:4.

  • “Samsoni akasema kwa sauti kubwa: ‘Acha nafsi yangu ikufe pamoja na Wafilisti!’”​—Waamuzi 16:30. Maelezo ya chini.

  • “Je, inaruhusiwa siku ya Sabato kufanya mema ao mabaya, kuokoa nafsi ao kuua?”​—Marko 3:4. Maelezo ya chini.

Biblia inaonyesha kama nafsi inakufaka

Maandiko ingine inaonyesha kama nafsi inaweza kuharibiwa, (Mwanzo 17:14), kupigwa kwa upanga (Yoshua 10:37), kukosa pumuzi (Yobu 7:15), na kufunikwa na maji (Yona 2:5). Ile inaonyesha kama nafsi inakufaka.

Kama unasoma Biblia kuanzia mwanzo mupaka mwisho, hakuna kwenye utakutana maneno “nafsi yenye haikufake.” Nafsi ya mwanadamu haiko roho. Biblia haifundishe kama nafsi haikufake. Ile ni fundisho ya Shetani na pepo wake wachafu. Yehova anachukia mambo yote ya uongo yenye dini zinafundishaka.​—Mezali 6:16-19; 1 Timoteo 4:1, 2.

Wanatumia Wachawi

Pepo wachafu wanafanyaka ionekane kama wao ni roho za wafu

Njia ingine yenye Shetani na pepo wake wachafu wanatumia juu ya kudanganya watu ni wachawi. Muchawi ni mutu mwenye anaweza kuzungumuza moja kwa moja na pepo wachafu. Watu wengi sana, na hata wachawi wenyewe, wanawazaka kama wako njo nazungumuza na roho za wafu. Lakini vile tuliona mu Biblia, ile haiwezekane.​—Muhubiri 9:5, 6, 10.

Sasa, wanakuwaka wanazungumuza na nani? Na pepo wachafu! Wakati mutu iko muzima, pepo wachafu wanaweza kumuchunguza. Wanajua namna alikuwa anazungumuza, namna alikuwa anafanana, mambo yenye alikuwa anafanya, na mambo yenye alikuwa anajua. Njo maana ni mwepesi kwao kujifanya sawa vile ule mutu mwenye alikufa.​—1 Samweli 28:3-19.

Wanatumia Habari za Uongo

Njia ingine yenye Shetani anatumia juu ya kudanganya watu ni habari za uongo. Mara mingi zile habari zinafanyaka watu wasiamini kweli yenye iko mu Biblia.​—2 Timoteo 4:4.

Watu fulani wanawazaka kama waliona watu wenye walirudia kisha kufa

Mu Afrika muko hadisi za mingi zenye zinaonyesha kama kuko watu wenye walionekana wazima kisha wao kufa. Mara mingi wale watu wanaonekanaka mbali sana na fasi kwenye walikuwa naishi. Sasa ujiulize hivi: ‘Kama mutu iko na uwezo wa kurudia kisha kufa, anaweza kabisa kurudia mbali na watu wa familia yake na marafiki wake?’

Tena, inawezekana kuwa mutu mwenye wanasema kama waliona anafanana tu ule mutu mwenye alikufaka, lakini haiko yeye. Kwa mufano, wakati Mashahidi wawili walikuwa wanahubiri mu kijiji fulani waliona kama mwanaume fulani mwenye kuzeeka alikuwa nawafuata nyuma. Wakati walimuuliza juu ya nini iko nawafuata, aliwaambia kama aliwaza kama mumoja kati yao ni ndugu yake mwenye alikufaka zamani. Lakini haikukuwa vile, na hata kama walimufasiria hakupenda kuamini. Wazia sasa habari yenye ule muzee aliendaka kuelezea marafiki na majirani wake!

Wanatumia Maono, Ndoto, na Sauti

Pepo wachafu wanatumia ndoto, maono, na sauti juu ya kudanganya watu

Inawezekana ulishakasikia watu wenye walionaka, walisikiaka, ao kulota mambo ya ajabu-ajabu. Mara mingi mambo ya vile inaogopeshaka wale watu. Marein, mwenye alikuwaka naishi mu Afrika ya Mangaribi alikuwaka anasikia sauti ya tate yake iko anamuita usiku. Juu ya woga, Marein alikuwa analalamika na kulamusha watu wote mu nyumba. Na ku mwisho akakuwa mwenda-wazimu.

Sasa kama wafu wanaishi kabisa, wanaweza kabisa kuogopesha wapendwa wao? Hapana. Pepo wachafu njo tu wanafanyaka mambo ya vile juu ya kuumiza wengine.

Halafu kama wafu wanaonekana kuwa wanasema mambo ya kusaidia na ya kufariji? Kwa mufano, Gbassay, wa Sierra Leone, alikuwaka mugonjwa. Alilotaka ndoto. Mu ile ndoto, baba yake mwenye alikuwaka alishakufa alimutokeaka na kumuambia aende ku muti fulani, akate mayani ya ile muti, aichange na maji, kisha aikunywe. Hakupaswa kuzungumuza na mutu yeyote mbele ya kufanya ile mambo. Alifanya vile na akapona.

Mwanamuke mwingine alisema kama kisha bwana yake kufa, alimutokeaka usiku. Alisema kama bwana yake alikuwaka anapendeza na alikuwaka anavala muzuri.

Ile mambo inaonekana kuwa ya muzuri na ya kusaidia, lakini inatoka kwa Mungu? Hapana! Yehova ni “Mungu wa ukweli.” (Zaburi 31:5) Hawezi hata kidogo kutudanganya. Pepo wachafu njo wanafanyaka vile.

Kuko mashetani wazuri? Hapana. Hata kama inaweza kuonekana kama wanasaidiaka wakati fulani, wote ni wabaya. Wakati Ibilisi alizungumuzaka na Eva, alijifanyaka sawa mutu muzuri. (Mwanzo 3:1) Lakini, nini ilifikiaka Eva kisha kusikiliza na kufanya mambo yenye Shetani alimuambiaka? Alifikiaka kufa.

Shetani aliambia Eva kama hatakufa. Eva alimuamini, lakini ku mwisho alikufa

Unajua kama mara mingi watu wabaya wanajifanyaka kuwa watu wazuri kama wanapenda kudanganya watu wengine. Mezali moja ya Afrika inasema kama “sura si roho.” Biblia nayo inasema hivi: “Shetani mwenyewe anaendelea kujifanya kuwa malaika wa mwangaza.”​—2 Wakorinto 11:14.

Mungu hatumiake tena ndoto, maono ao sauti juu ya kuzungumuza na wanadamu ku dunia. Anawaongoza na kuwafundisha kupitia Biblia, yenye inaweza kufanya mutu ‘akuwe na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.’​—2 Timoteo 3:17.

Yehova anatupenda. Njo maana anatuambia tufanye angalisho na ujanja wa Shetani. Anajua kama pepo wachafu ni maadui wenye wanaweza kutufanyia mambo ya mubaya.