Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utangulizi

Utangulizi

Dauda, wa Sierra Leone, anasema hivi: “Nilikomalia mu kijiji kidogo mu jimbo ya kaskazini. Siku moja wakati nilikuwa mutoto, familia yangu na familia ingine zilipigania shamba. Kila familia ilikuwa nasema kama ile shamba ni yake. Juu ya kujua ile shamba ilikuwa ya nani, waliita mufumu. Alipatia mwanaume fulani kioo, kisha akamufunika nguo ya mweupe. Kisha ule mwanaume mwenye alikuwa ndani ya ile nguo, akaanza kutetemeka na kutokwa na jasho. Wakati ule mwanaume aliangalia mu ile kioo, alisema hivi kwa sauti: ‘Ninaona mwanaume muzee-muzee iko nakuya! Anavala manguo ya mweupe. Ni murefu na mwenye kuzeeka, iko na nywele za mweupe, na iko natembea na anagunjama mugongo.’

“Alikuwa nazungumuzia tate yangu mwanaume! Kisha akaanza kulia bila kujizuia na kulalamika hivi: ‘Kama hamuamini mambo yenye niko nasema, mukuye mujionee!’ Lakini, kila mutu aliogopa kufanya vile! Kisha, juu ya kumutuliza, ule mufumu alimumwangia dawa fulani ya kichawi yenye ilikuwa ndani ya kibuyu yenye ilitengenezwa kwa majani na maji.

“Tate yangu mwanaume alizungumuza kupitia ule mwanaume mwenye alikuwa na kioo. Alisema kama ile shamba ilikuwa ya familia yetu. Aliambia tate yangu mwanamuke kama anapaswa kulima ile shamba bila kuogopa. Ile familia ingine iliitika na mambo ikaishia pale.”

Ni kawaida kusikia habari za vile mu Afrika ya mangaribi. Kule, na mu sehemu zingine za ulimwengu, watu wengi sana wanaamini kama wafu wanaendaka mu ulimwengu wa roho, na kule wanaweza kuona watu wenye wako ku dunia na kuwatendea muzuri ao mubaya. Ile ni kweli? Wafu wako naishi fasi fulani? Kama haiko vile, wale wenye kuitwa roho za wafu ni nani? Ni jambo ya maana sana kujua majibu ya ile maulizo, juu inaweza kutusaidia tukuwe na tumaini ya uzima.