Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

1

‘Aliyepotea Nitamutafuta’

‘Aliyepotea Nitamutafuta’

Kondoo inapotea. Pengine, wakati iliendelea kula majani hapa na pale katika malisho, ilijitenga polepole na kondoo wengine. Sasa haione tena kundi la kondoo wenzake, wala muchungaji wake. Usiku unaanza kuingia. Imepotea katika bonde, na humo muko wanyama wakali wenye kutembea-tembea, lakini kondoo hiyo haina nguvu ya kujikinga. Kisha inasikia sauti yenye inazoea, ile sauti ya muchungaji. Muchungaji huyo anaenda mbio kwenye kuwa kondoo yake, anainyangula na kuikumbatia, anaifunika na nguo yake, na anaipeleka nyumbani.

MARA kwa mara Yehova anajilinganisha na muchungaji kama huyo. Katika Neno lake, anakuhakikishia hivi: ‘Mimi mwenyewe nitawatafuta kondoo zangu na nitawatunza.’​—Ezekieli 34:11, 12.

Kondoo Ninaotunza

Kondoo wa Yehova ni nani? Kwa kifupi, kondoo wa Yehova ni watu wenye wanamupenda na kumuabudu. Biblia inasema: ‘Muingie, tuabudu na kuinama; na tupige magoti mbele ya Yehova Mutengenezaji wetu. Kwa maana yeye ni Mungu wetu, na sisi ni watu wa malisho yake na kondoo wa mukono wake [kondoo wenye anatunza].’ (Zaburi 95:6, 7) Waabudu wa Yehova ni kama vile kondoo wenye kupenda sana Muchungaji wao. Ni kusema, hawafanyake makosa? Hapana. Wao pia wanafanyaka makosa. Wakati fulani watumishi wa Mungu wamekuwa kama vile ‘kondoo wenye kutawanyika (kusambaa),’ “kondoo waliopotea,” “kondoo wanaopotea [ao wenye kuacha] njia.” (Ezekieli 34:12; Mathayo 15:24; 1 Petro 2:25) Hata hivyo, wakati mutu anaacha kutaniko, Yehova hamukatae, anaendelea kutumainia kwamba atamurudilia.

Ungali unajisikia kwamba Yehova ni Muchungaji wako? Ni nini inaonyesha kwamba hata leo Yehova angali Muchungaji wetu? Tuzungumuzie njia hizi tatu:

Anatulisha kiroho. Yehova anasema hivi: ‘Katika malisho mazuri nitawalisha. Huko watalala katika makao mazuri, na kwenye malisho manono [majani mabichi] watajilisha.’ (Ezekieli 34:14) Yehova hajakosa hata siku moja kututolea chakula kizuri cha kiroho kwa wakati wenye kufaa. Unakumbuka habari moja hivi, hotuba, ao video moja hivi yenye ilionekana kuwa jibu ya sala yako ya kumuomba Yehova akusaidie? Je, hilo halikukuhakikishia kwamba Yehova anakuhangaikia kipekee?

Anatulinda na kutupatia nguvu. Yehova anaahidi kwamba atarudisha kondoo yenye ilipotea, atafunga vitambaa kondoo yenye iliumizwa, na atatia nguvu kondoo yenye inagonjwa. (Ezekieli 34:16) Yehova anawapatia nguvu wazaifu na wale wenye kusumbuliwa na mahangaiko. Anafunga vidonda vyao kwa vitambaa, ikiwa waliumizwa; hata kama waliumizwa na Wakristo wenzao. Na anarudisha wale waliacha kutaniko na wale wenye kwa sasa wanasumbuliwa na mawazo mabaya.

Kutuchunga ni daraka lake. Yehova anasema hivi: ‘Nitawakomboa kutoka mahali pote ambapo wametawanyika. Aliyepotea nitamutafuta.’ (Ezekieli 34:12, 16) Hata kama kondoo inapotea, Yehova anaendelea kuwa na tumaini kwamba inaweza kumurudilia tena ao kubadilika. Wakati anaona kwamba kondoo moja inakosekana, anaenda kuitafuta, na anafurahi wakati anaipata. (Mathayo 18:12-14) Ndio sababu anawaita waabudu wake wa kweli kuwa ni kondoo wake, kondoo wenye anatunza. (Ezekieli 34:31) Wewe pia uko kati ya kondoo hao.

Hata kama kondoo inapotea, Yehova anaendelea kutumainia kwamba inaweza kumurudilia tena ao kubadilika. Anafurahia wakati kondoo hiyo inapatikana

Fanya Tena Siku Zetu Kama Siku za Zamani

Sababu gani Yehova anakutafuta na anakuomba umurudilie? Ni kwa sababu anapenda ukuwe na furaha. Anatuahidi kwamba baraka zitamwangika kama “mvua” juu ya kondoo zake. (Ezekieli 34:26) Ahadi hiyo ni ya kweli kabisa. Umekwisha kujionea jambo hilo.

Kumbuka wakati ulimujua Yehova. Kwa mufano, ulijisikia namna gani wakati kwa mara ya kwanza ulijua kweli zenye kuchangamusha juu ya jina la Mungu na makusudi (mapenzi) yake juu ya wanadamu? Unakumbuka furaha ulikuwa nayo wakati ulikuwa kwenye mikusanyiko ya muzunguko ao ya eneo pamoja na Wakristo wenzako? Unakumbuka furaha yenye ulikuwa unarudia nayo nyumbani, na namna ulikuwa mwenye kutosheka kisha kuhubiria mutu fulani mwenye kupendezwa kabisa na habari njema?

Unaweza tena kuwa na furaha hiyo. Watumishi wa Mungu wa zamani walisali hivi: ‘Uturudishe kwako, Ee Yehova, nasi tutarudi bila kukawia.’ Na walimuomba Yehova afanye tena siku zao kama siku za zamani. (Maombolezo 5:21) Yehova alijibu sala hiyo, na watu wake walimutumikia tena na walirudilia furaha yao ya zamani. (Nehemia 8:17) Yehova atakutendea hivyohivyo.

Ni mwepesi kusema ‘nitamurudilia Yehova,’ lakini kutenda haiko mwepesi. Tuone mambo fulani yenye inaweza kufanya ikuwe nguvu mutu kumurudilia Yehova na namna unaweza kushinda mambo hayo.