Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

4

Kuumizwa na Zamiri​—Unisafishe ‘Zambi Zangu’

Kuumizwa na Zamiri​—Unisafishe ‘Zambi Zangu’

“Kazi yangu mupya ilisaidia familia yangu ikuwe na maisha mazuri, lakini iliniingiza pia katika mambo mengi ya mubaya. Nilianza kufanya karamu za ulimwengu, kuingia katika mambo ya politike na hata kuingia katika makanisa. Niliacha kukusanyika na kuhubiri kwa miaka 40. Siku nyingi zilipita, na nikaanza kuona kwamba Yehova hawezi kunisamehe. Niliwaza kwamba hata mimi mwenyewe siwezi kujisamehe. Lakini, mwishowe nilibadilisha mawazo na sikuendelea tena katika njia mubaya.”​—Dada Martha.

MUTU mwenye kujihukumu anaweza kujisikia sawa anabeba muzigo muzito sana wenye kumutesa. Mufalme Daudi aliandika hivi: ‘Makosa yangu yamepita juu ya kichwa changu; kama muzigo muzito, ni mazito sana kwangu.’ (Zaburi 38:4) Huzuni ya kupita mipaka imewafanya ndugu na dada fulani wajisikie kwamba Yehova hawezi hata kidogo kuwasamehe. (2 Wakorintho 2:7) Mawazo kama hayo ni ya kweli? Hata kama ulifanya zambi nzito, unawaza uko mbali sana na Yehova, na hawezi kabisa kukusamehe? Hapana, anaweza kukusamehe!

Tutengeneze “Mambo Kati Yetu”

Yehova hawatupilie watenda-zambi wenye kutubu. Kumbuka kwamba anawatafuta! Katika mufano wa mwana mupotevu, Yesu alimulinganisha Yehova na baba mwenye upendo aliyekuwa na mutoto mwenye aliacha familia yao na kuenda kuishi maisha machafu. Siku moja hivi, mutoto huyo akaamua kurudi kwao. ‘Alikuwa angali mbali, baba yake akamuona, akamusikitikia [akamusikilia huruma], akakimbia, akamuangukia kwenye shingo [akamukumbatia] na kumubusu kwa wororo (kwa upendo).’ (Luka 15:11-20) Je, unapenda kumurudilia Yehova, lakini unajisikia kama ‘ungali mbali sana’ naye? Kama baba huyo katika mufano wa Yesu, Yehova atakusikilia huruma. Iko tayari kukukaribisha.

Lakini, namna gani ikiwa unawaza kama zambi zako ni nzito sana ao nyingi sana, na kwamba Yehova hawezi kukusamehe? Tafazali, Yehova anakuita. Kwenye Isaya 1:18 anasema hivi: “‘Sasa, njooni, nasi tunyooshe mambo kati yetu,’ asema Yehova. ‘Hata zambi zenu zikiwa nyekundu, zitafanywa kuwa nyeupe kama teluji.’” Ndiyo, Yehova anaweza kusamehe hata zambi zenye kuonekana kuwa haziwezi kuvutwa, zenye kuwa kama vile rangi nyekundu kwenye nguo mweupe.

Yehova hapendi uendelee kuumizwa na zamiri yako. Musamaha wa Mungu unatuliza kabisa na unafanya mutu akuwe na zamiri safi. Basi, unaweza kufanya nini juu ufaidike na mupango huo? Ona mambo mbili yenye Mufalme Daudi alifanya. Kwanza alisema hivi: “Nitaungamana makosa yangu kwa Yehova.” (Zaburi 32:5) Kumbuka, Yehova amekwisha kukuomba umukaribie katika sala na kutengeneza “mambo” pamoja naye. Kubali mualiko huo. Ungama zambi zako kwa Yehova, na umuelezee vile unajisikia. Daudi alijua vizuri kwamba Yehova anasamehe, ndio sababu alisali kwa uhakika wote ili Yehova amusamehe zambi zake. Aliongeza tena hivi: ‘Moyo uliovunjika na kupondwa, Ee Mungu, hautauzarau.’​—Zaburi 51:2, 17.

Jambo la pili, Mungu alimutumia Daudi mutu wa kumusaidia. Alimutumia nabii Nathani. (2 Samweli 12:13) Leo, Yehova ameweka wazee katika makutaniko; wanaume hao wamezoezwa vizuri ili kusaidia watenda-zambi wenye kutubu warudilie urafiki wao pamoja naye. Wakati unaungamana zambi zako, wazee watatumia Maandiko na kutoa sala ili kutuliza moyo wako, kupunguza ao kuondoa kabisa mawazo yako mabaya, na kukusaidia upone kiroho.​​—Yakobo 5:14-16.

Yehova anapenda ufaidike na zamiri safi

‘Mwenye Furaha Ni Mutu Ambaye Amesamehewa Maasi [Makosa] Yake’

Bila shaka, unaweza kuona kwamba ni jambo ngumu sana kuungama zambi zako kwa Yehova na kuenda kuwaona wazee. Ni kweli Daudi pia alijisikia hivyo. Kisha kufanya zambi, ‘alikaa kimya’ kwa wakati fulani. (Zaburi 32:3) Lakini, kisha aliungama zambi zake na kubadilisha mwenendo wake; hilo lilimuletea faida sana.

Faida kubwa ni kwamba Daudi alipata tena furaha yake. Aliandika hivi: ‘Mwenye furaha ni mutu ambaye amesamehewa maasi [makosa] yake, mwenye zambi yake imefunikwa.’ (Zaburi 32:1) Alisali tena hivi: ‘Ee Yehova, na uifungue hii midomo yangu, ili kinywa changu kipate kutangaza sifa yako.’ (Zaburi 51:15) Kwa kuwa Mungu alimusamehe Daudi, zamiri ya Daudi iliacha kumusumbua. Kwa hiyo, Daudi alisikia furaha ya kuwaambia wengine juu ya sifa za Yehova.

Zamiri safi inatuliza, na Yehova anapenda ufaidike na zamiri kama hiyo. Na anapenda uwaambie wengine juu yake na makusudi yake kwa furaha kubwa na kwa zamiri safi. (Zaburi 65:1-4) Kumbuka kwamba anakuita ili ‘kuvuta zambi zako, ili majira ya kuburudisha yapate kuja kutoka kwa uso wa Yehova.’​—Matendo 3:19.

Jambo hilo ndilo lilimufikia Martha. Anasema hivi: “Kijana wangu aliendelea kunitumia Munara wa Mulinzi na Amuka! Polepole nikaanzisha tena urafiki pamoja na Yehova. Jambo lenye lilikuwa nguvu kwangu juu ya kurudia, ilikuwa ni kuomba musamaha wa zambi zote zenye nilifanya. Lakini, mwishowe, nilimukaribia Yehova katika sala na kumuomba anisamehe. Inaweza kuwa nguvu kuamini kwamba nilimuacha Yehova miaka 40, kisha nikamurudilia. Maisha yangu yanaonyesha kwamba hata kisha miaka mingi, inawezekana mutu amutumikie tena Mungu na kumupenda tena.”