Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

3

Kuumizwa na Matendo ya Wengine​—Wakati ‘Tuko na Sababu ya Kunungunika’

Kuumizwa na Matendo ya Wengine​—Wakati ‘Tuko na Sababu ya Kunungunika’

“Katika kutaniko letu, dada moja alinisingizia (alinisemea uongo) kwamba nilimuiba feza. Wengine katika kutaniko walisikia habari hiyo na wakaanza kunikimbia. Kisha, dada huyo aliambiwa kwamba ni mutu mwengine, na akakuja kuniomba musamaha. Nilisikia katika moyo wangu kama singeweza kumusamehe hata kidogo.”​—Dada Linda.

UMEKWISHA kujisikia kama vile dada Linda, mwenye aliumizwa sana na matendo ya dada huyo? Jambo la kusikitisha ni kuona ndugu na dada fulani wamesumbuliwa sana na mwenendo wa wengine na hilo limeharibu urafiki wao pamoja na Yehova. Jambo kama hilo limekwisha kukufikia?

Mutu fulani Anaweza ‘Kututenganisha na Upendo wa Mungu’?

Kwa kweli, wakati tunaumizwa na matendo ya ndugu ao dada inaweza kuwa vigumu sana kusamehe. Hata hivyo, Wakristo wanapaswa kupendana. (Yohana 13:34, 35) Ikiwa Shahidi mwenzetu ametukosea, tunaweza kuumizwa sana na kuvunjika moyo kabisa.​—Zaburi 55:12.

Bila shaka, Biblia inaonyesha kwamba kuna wakati Wakristo wanaweza kufanya mambo yenye inaweza kuwapatia wengine “sababu ya kulalamika (kunungunika).” (Wakolosai 3:13) Wakati mambo kama hayo yanatokea, pengine tunaweza kuona kuwa vigumu kuvumilia. Je, kuna jambo lenye linaweza kutusaidia? Tuone kanuni hizi tatu za Biblia:

Baba yetu wa mbinguni anaona kila kitu. Yehova anaona kila jambo lenye kutupata, anaona pia mateso yenye tunapata kwa sababu ya kutendewa bila haki. (Waebrania 4:13) Zaidi ya hiyo, wakati sisi tunateseka, Yehova naye anateseka. (Isaya 63:9) Hataruhusu hata kidogo ‘ziki ao taabu,’ wala hata mutumishi wake ao jambo lingine lolote ‘litutenganishe na upendo wa Mungu.’ (Waroma 8:35, 38, 39) Kwa hiyo basi, na sisi hatupaswe kuruhusu jambo lolote ao mutu yeyote atutenganishe na Yehova.

Kusamehe hakumaanishe kuachilia makosa. Kuwasamehe wale walitukosea, hakumaanishe kupunguza uzito wa makosa yao. Tena hakumaanishe kutetea, kuachilia ao kukubali matendo yao. Usisahau jambo hili: Yehova hapendake zambi, lakini anasamehe ikiwa kuna sababu ya kufanya hivyo. (Zaburi 103:12, 13; Habakuki 1:13) Kwa hiyo, wakati Yehova anatushauri tuwasamehe wengine, anatuomba tufuate mufano wake. ‘Haweke kinyongo kwa wakati usio na kipimo,’ ao milele. ​—Zaburi 103:9; Mathayo 6:14.

Wakati hatuweke kinyongo, ni sisi tunapata faida. Namna gani? Tukamate mufano. Unakamata jiwe, pengine jiwe hilo halina uzito sana, kisha unanyoosha mukono wako wenye kukamata jiwe hilo. Unaweza kubakia katika hali hiyo kwa wakati mufupi. Lakini itakuwa namna gani kama unapenda kubakia na jiwe hilo kwa muda murefu? Unawaza utafanya hivyo dakika ngapi? Saa moja? ao muda murefu sana? Bila shaka, mukono wako utachoka sana! Kwa kweli, uzito wa jiwe hautabadilika. Lakini ukiendelea kukamata jiwe hilo kwa wakati murefu sana, utasikia sawa linakuwa na uzito sana. Kuweka kinyongo ni hivyo pia. Wakati tunaendelea kuweka kinyongo, hata kakinyongo kadogo, kwa wakati murefu, tunajiumiza sisi wenyewe katika moyo. Kwa hiyo, tusishangae ikiwa Yehova anatukataza kuweka kinyongo. Kwa kweli, kuacha kuweka kinyongo ni kwa faida yetu.​—Methali 11:17.

Kuacha kuweka kinyongo ni kwa faida yetu

“Ni Kama Vile Yehova Mwenyewe Alikuwa Anazungumuza na Mimi”

Ni jambo gani lilimusaidia Linda asiweke kinyongo wakati Shahidi mwenzake alimuumiza sana? Kuna mambo mengi yenye ilimusaidia. Kwa mufano, aliwaza sana juu ya sababu za Maandiko zenye kutuomba tuwasamehe wengine. (Zaburi 130:3, 4) Jambo lenye lilimusaidia sana Linda, ni kujua kama wakati tunawasamehe wengine, Yehova naye anatusamehe. (Waefeso 4:32–5:2) Wakati alikuwa anawaza namna maandiko hayo yalimusaidia, alisema hivi: “Ni kama vile Yehova mwenyewe alikuwa anazungumuza na mimi.”

Kisha, Linda aliacha kuwekea dada yake kinyongo. Alimusamehe, na sasa yeye na dada huyo ni marafiki sana. Linda ameendelea kumutumikia Yehova. Ukuwe hakika kwamba Yehova anapenda kukusaidia ufanye hivyo pia.