Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Umalizio

Umalizio

Unaendelea kukumbuka ule wakati muzuri wenye ulikuwa unapitisha pamoja na watu wa Yehova; mukutano wenye kutia moyo, mukusanyiko wenye kuchochea, jambo lenye kupendeza katika mahubiri, ao mazungumuzo mazuri pamoja na Shahidi mwengine? Ikiwa ni hivyo, haujamusahau Yehova, yeye naye hajakusahau. Anakumbuka namna ulimutumikia kwa uaminifu. Na anapenda sana kukusaidia ili umurudilie.

Yehova anasema hivi: ‘Mimi mwenyewe nitawatafuta kondoo zangu na kuwatunza. Kulingana na utunzaji wa mutu anayelisha kundi lake katika siku ya kuja kwake kuwa katikati ya kondoo zake ambao wametawanyika kotekote, hivyo ndivyo nitakavyowatunza kondoo zangu; nami nitawakomboa kutoka mahali pote wametawanyika.’​—Ezekieli 34:11, 12.