Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

2

Mahangaiko​—Tunabanwa “Katika Kila Njia”

Mahangaiko​—Tunabanwa “Katika Kila Njia”

“Kisha miaka 25 ya maisha ya ndoa, ndoa yetu ilivunjika. Watoto wangu waliacha kweli. Nilipatwa na magonjwa mbalimbali ya hatari. Kisha nikavunjika moyo sana. Nilijisikia kama vile nafika mwisho na sikuwa tena na nguvu ya kufanya jambo lolote. Niliacha kuenda ku mikutano, na niliacha kuhubiri.”​—Dada June.

MAHANGAIKO yanafikia watu wote, hata watumishi wa Mungu. Mutunga-zaburi aliandika kwamba alikuwa na mahangaiko mengi sana. (Zaburi 94:19) Wakati wa mwisho, kwa sababu ya “mahangaiko ya maisha,” haingekuwa mwepesi kumutumikia Yehova. (Luka 21:34) Wewe pia unapatikana katika hali hiyo? Unajisikia kwamba magumu ya feza, magumu ya familia yanakuhangaisha, ao unahangaishwa na magonjwa? Namna gani Yehova anaweza kukusaidia upiganishe hali hiyo?

‘Nguvu Zenye Kupita Zile za Kawaida’

Hatuwezi kushinda mahangaiko kwa nguvu yetu wenyewe. Mutume Paulo aliandika hivi: ‘Tunakazwa (tunabanwa) katika kila njia, tunafazaishwa; tunaangushwa chini.’ Lakini alisema tena, ‘hatubanwe kupita kiasi cha kuweza kusonga (kuenda mbele),’ “si bila njia ya kutokea kabisa,” na ‘hatuangamizwe.’ Ni nini inatusaidia kuvumilia? Ni ile ‘nguvu yenye kupita ile ya kawaida,’ ni kusema, nguvu yenye kutoka kwa Yehova Mungu, mwenye uwezo wote.​—2 Wakorintho 4:7-9.

Kumbuka vile, hapo zamani, ulipata ‘nguvu yenye kupita ile ya kawaida.’ Unakumbuka namna hotuba moja hivi ilikufanya ufurahie upendo mushikamanifu wa Yehova? Je, imani yako katika ahadi za Yehova iliongezeka na kuwa nguvu wakati ulielezea wengine juu ya tumaini la Paradiso? Wakati tunahuzuria mikutano na kuelezea wengine mambo yenye tunaamini, tunapata nguvu ya kupiganisha mahangaiko ya maisha na tunapata amani ya akili, mambo hayo yanaweza kutusaidia tumutumikie Yehova kwa furaha.

‘Onja Uone Kwamba Yehova Ni Mwema’

Pengine unaweza kuona kwamba mambo ya kufanya ni mengi. Kwa mufano, Yehova anatuomba tutafute kwanza Ufalme na kufanya kwa kawaida mambo mengine ya kiroho. (Mathayo 6:33; Luka 13:24) Utafanya nini ikiwa mambo kama vile upinzani, magonjwa, ao magumu ya familia yanakuchokesha sana? Ao ikiwa kazi yako ya kimwili inakuchokesha sana na inakubeba wakati wote wenye ungepaswa kutumia juu ya mambo ya kutaniko? Kupambana na mambo mengi kama hayo, na kukosa wakati wa kushugulikia mambo hayo, kunaweza kufanya ujisikie kama unashindwa. Pengine umefikia hata kuwaza kama Yehova anakuomba mambo mengi.

Yehova anajua hali ya kila mumoja wetu. Hakuombe ufanye mambo yenye kupita uwezo wako. Na anajua kwamba inaomba wakati juu mutu arudilie tena hali yake muzuri ya kimwili na ya kiakili.​—Zaburi 103:13, 14.

Kwa mufano, angalia namna Yehova alimutendea nabii Eliya. Wakati Eliya alivunjika moyo na kuogopa alikimbilia katika jangwa. Je, Yehova alimufokea nabii huyo na kumuambia arudie mara moja kufanya kazi yenye alimupatia? Hapana. Yehova alituma malaika mara mbili juu amuamushe Eliya kwa upole na amupatie chakula. Hata hivyo, kisha siku 40, Eliya aliendelea kuwa na mahangaiko na woga. Yehova alifanya tena nini juu ya kumusaidia? Jambo la kwanza, Yehova alionyesha kwamba angeweza kumulinda. Jambo la pili, Yehova alimufariji Eliya kwa “sauti tulivu, ya chini.” Na jambo la tatu, Yehova alimufunulia kwamba kulikuwa maelfu ya watu wengine wenye walimuabudu Mungu kwa uaminifu. Mara moja, Eliya alipata tena nguvu na bidii ya kuendelesha kazi yake ya nabii. (1 Wafalme 19:1-19) Habari hiyo inatufundisha nini? Wakati Eliya alisumbuliwa na mahangaiko, Yehova aliweka pa nafasi yake na alimuvumilia. Yehova hajabadilika. Anatuhangaikia sisi pia hivyo katika njia nyingi.

Wakati unawazia kufanya jambo fulani juu ya Yehova, wazia hali yako ya sasa. Usilinganishe mambo yenye unaweza kufanya leo na yale ulikuwa unafanya zamani. Tuchukue mufano: Mukimbiaji mwenye ameacha kukimbia kwa miezi ao miaka mingi hawezi kuanza kukimbia mara moja kama zamani. Lakini, anaanza kufanya mazoezi kidogokidogo na hilo litamusaidia kuwa tena na nguvu na uvumilivu. Wakristo ni kama wakimbiaji. Wakati wanakimbia wako na muradi (kusudi) fulani katika akili. (1 Wakorintho 9:24-27) Juu ya nini usifuatie muradi moja wa kiroho wenye unaweza kufikia sasa? Kwa mufano, unaweza kujiwekea muradi wa kuhuzuria mukutano fulani wa kutaniko. Umuombe Yehova akusaidie ufikie muradi wako. Wakati unaendelea kupata tena nguvu yako ya kiroho, ‘utaonja na kuona kwamba Yehova ni mwema.’ (Zaburi 34:8) Kumbuka kwamba Yehova anapendezwa sana na kila jambo lenye unafanya ili kuonyesha upendo wako kwake. Jambo hilo linaweza kuwa ndogo ao kubwa.​—Luka 21:1-4.

Yehova hakuombe ufanye mambo yenye kupita uwezo wako

“Nilipata Tena Nguvu”

Namna gani Yehova alimupatia dada June nguvu ya kumurudilia? Anatuambia hivi: “Niliendelea kusali kwa Yehova na kumuomba musaada. Kisha bibi ya mutoto yangu akanielezea juu ya mukusanyiko mumoja katika muji wangu. Nikaamua kuhuzuria siku moja ya mukusanyiko huo. Ni ajabu, nilijisikia mwenye furaha sana kuwa tena kati ya watu wa Yehova! Mukusanyiko huo ulinipatia tena nguvu. Sasa namutumikia tena Yehova kwa furaha. Maisha yamekuwa tena ya maana kwangu. Zaidi ya hilo, ninaelewa kwamba niko na lazima ya ndugu na dada na ninapaswa kukubali musaada wao. Ninashuruku sana kuona kwamba nilikuwa ningali na wakati wa kumurudilia Yehova.”