Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

5

Umurudilie ‘Muchungaji na Mwangalizi wa Nafsi Zetu’

Umurudilie ‘Muchungaji na Mwangalizi wa Nafsi Zetu’

Katika broshua hii tumezungumuzia mifano ya watu wenye walipatwa na magumu mbalimbali. Umejisikia kuwa kama mumoja wao? Ikiwa ndiyo, usiwaze kama ni wewe peke. Watumishi wengi waaminifu wa Mungu​—wa zamani na wa siku zetu, walipatwa na magumu kama hayo katika maisha yao. Yehova aliwasaidia na walishinda magumu hayo, wewe pia anaweza kukusaidia.

Yehova atakupokea wakati utamurudilia

UWE hakika kwamba Yehova atakupokea wakati utamurudilia. Atakusaidia upiganishe mahangaiko yako, mambo yenye kuumiza moyo wako. Utakuwa na zamiri safi, na hiyo itakusaidia ukuwe na amani ya akili na ya moyo. Kisha utakuwa na furaha ya kumutumikia tena Yehova pamoja na Mashahidi wenzako. Hali yako itafanana na ile ya Wakristo fulani wa wakati wa mitume. Mutume Petro aliwaandikia Wakristo hao hivi: ‘Mulikuwa kama kondoo, wanaopotea njia; lakini sasa mumerudilia muchungaji na mwangalizi wa nafsi zenu.’​—1 Petro 2:25.

Kumurudilia Yehova ndio jambo muzuri kabisa lenye unaweza kufanya. Juu ya nini? Ukifanya hivyo, utafurahisha moyo wa Yehova. (Methali 27:11) Kama vile unajua, matendo yetu yanaweza kumufurahisha Yehova ao kumusikitisha. Bila shaka, Yehova hatulazimishe tumupende na kumutumikia. (Kumbukumbu 30:19, 20) Mutu mumoja mwenye aliandika sana juu ya Biblia alisema hivi: “Moyo wa mwanadamu ni kama mulango wenye kufungiwa kwa ndani. Ni ule iko ndani tu ndiye anaweza kuufungua.” Tunaweza kufungua mulango huo wa mufano wakati sisi wenyewe tunaamua kumuabudu Yehova kwa moyo wenye kujaa upendo. Moyo kama huo, unatusukuma tumutolee Yehova zawadi za muzuri sana. Kumuabudu Yehova hivyo kunafurahisha moyo wake sana. Kumutolea Yehova ibada yenye anastahili kunaleta furaha sana. Hakuna jambo lingine linaweza kutupatia furaha kama hiyo.​—Matendo 20:35; Ufunuo 4:11.

Tena, wakati unarudilia utumishi wako kwa Yehova, mahitaji yako ya kiroho yatatimizwa. (Mathayo 5:3) Namna gani? Watu wengi wanajiuliza, ‘sababu gani tuko duniani?’ Wako na hamu ao njaa ya kupata majibu ya maulizo kama hayo. Wanadamu wanapenda kujua mambo hayo kwa sababu Yehova aliwaumba na tamaa hiyo. Alituumba tukuwe na furaha wakati tunamutumikia. Wakati tunamuabudu Yehova kwa sababu tunasukumwa na upendo, tutakuwa na furaha ya kweli katika maisha.​—Zaburi 63:1-5.

Tafazali, jua kwamba Yehova anapenda umurudilie. Namna gani unaweza kuwa hakika kwamba anapenda ufanye hivyo? Wazia jambo hili: Tulitayarisha broshua hii kwa uangalifu sana na kisha kusali sana. Pengine ni muzee ndiye alipatia broshua hii ao Shahidi mwengine. Kisha uliisoma na ukafuata mashauri yenye kuwa ndani. Yote hiyo inaonyesha kwamba Yehova hajakusahau. Lakini, anakuvuta kwa upole ili umurudilie.​—Yohana 6:44.

Tunatiwa moyo kujua kwamba Yehova hasahau hata kidogo watumishi wake wenye kupotea. Dada Donna alijionea jambo hilo. Anasema hivi: Niliacha kweli polepole, lakini mara nyingi nilikuwa ninafikiri sana juu ya Zaburi 139:23, 24, yenye kusema: ‘Unichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu. Unichunguze, na uzijue fikira zangu zinazofazaisha [zenye kuhangaika]. Ona kama ndani yangu muko njia yoyote yenye kuumiza [mawazo yoyote mubaya], na uniongoze katika njia ya wakati usio na kipimo [ya milele].’ Nilijua kama sikupaswa kuwa sehemu ya ulimwengu, sikujisikia vizuri humo, na nilijuwa kwamba ni katika tengenezo la Yehova ndimo ninapaswa kuwa. Nilianza kuona kwamba Yehova hajanitupa; iliomba tu nimurudilie. Na ninafurahi sana kwa kuwa nilifanya hivyo!”

“Nilianza kuona kwamba Yehova hajanitupa; iliomba tu nimurudilie

Tunasali kabisa ili wewe pia upate tena “shangwe ya Yehova.” (Nehemia 8:10) Utaona kwamba haukukosea kwa sababu umemurudilia Yehova.