Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA 4

Walimusikiliza Shetani, Walipatwa na Nini?

Walimusikiliza Shetani, Walipatwa na Nini?

Adamu na Eva hawakumutii ao kumusikia Mungu, njo maana walikufa. Mwanzo 3:​6, 23

Eva alisikiliza nyoka na akakula tunda lenye Mungu aliwakataza. Kisha, akamupatia Adamu tunda hilo naye akakula.

Jambo lenye walifanya lilikuwa la mubaya; walifanya zambi. Mungu aliwafukuza mu Paradiso, kwenye walikuwa wanaishi.

Adamu na Eva na watoto wao wakaanza kuishi maisha ya nguvu sana. Adamu na Eva wakazeeka na kisha wakakufa. Wakati walikufa hawakuenda mbinguni ao mu moto wa mateso. Hawakuendelea kuishi.

Watu wenye wamekufa hawana uzima, kama vile mavumbi haina uzima. Mwanzo 3:​19

Tunakufaka juu sisi wote tuko watoto wa Adamu na Eva. Watu wenye wamekufa hawawezi kuona ao kusikia ao kufanya hata kitu fulani.​—Muhubiri 9:​5, 10.

Yehova hakupenda watu wakuwe wanakufa. Hivi karibuni, atafufua watu wenye wamekufa. Kama wanamusikiliza, wataishi milele.