Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA 8

Kifo cha Yesu Kitakuletea Faida Gani?

Kifo cha Yesu Kitakuletea Faida Gani?

Yesu alikufa ili tupate uzima. Yohana 3:16

Siku tatu kisha Yesu kufa, wanamuke fulani walienda ku kaburi lake na wakakuta liko wazi. Yehova alikuwa amemufufua Yesu.

Kisha, Yesu alitokea mitume wake.

Kwa kweli, Yehova alimufufua Yesu; alikuwa sasa malaika mwenye nguvu na mwenye hawezi kufa. Wanafunzi wa Yesu walimuona wakati alipanda mbinguni.

Mungu alimufufua Yesu na akamufanya kuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Danieli 7:13, 14

Yesu alitoa uzima wake ili kulipia wanadamu bei ya ukombozi. (Matayo 20:28) Kupitia ile bei ya ukombozi, Mungu alifanya iwezekane tuishi milele.

Yehova alimufanya Yesu kuwa Mufalme ili atawale dunia. Atakuwa pamoja na watu waaminifu 144000 wenye wanafufuliwa ili waende kuishi mbinguni. Yesu na wale 144000 njo wenye watafanyiza serikali ao guvernema ya mbinguni yenye itatawala kwa haki, ni kusema, Ufalme wa Mungu.​—Ufunuo 14:1-3.

Ufalme wa Mungu utafanya dunia ikuwe paradiso. Hakutakuwa tena vita, kuvunja sheria, umaskini, na njaa. Watu watakuwa na furaha kabisa.​—Zaburi 145:16.