Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA 3

Maisha Ilikuwa Namna Gani mu Paradiso?

Maisha Ilikuwa Namna Gani mu Paradiso?

Yehova alipatia Adamu na Eva vitu mingi vya muzuri. Mwanzo 1:28

Yehova aliumba Eva, mwanamuke wa kwanza, kisha akamupatia Adamu ule mwanamuke ili akuwe bibi yake.​—Mwanzo 2:21, 22.

Wakati Yehova aliwaumba, aliwapatia akili kamilifu na mwili mukamilifu, hawakukuwa hata na uzaifu.

Walikuwa wanaishi mu bustani ao shamba ya Edeni, ilikuwa nafasi ya muzuri sana. Mu ile bustani mulikuwa mutoni, miti ya matunda, na wanyama.

Yehova alikuwa anazungumuza na Adamu na Eva; alikuwa anawafundisha. Kama wangemusikiliza, wangeishi milele mu Paradiso ku dunia.

Mungu aliambia Adamu na Eva wasikule matunda ya muti moja kati ya miti ya mu bustani. Mwanzo 2:16, 17

Mu bustani ya Edeni, Yehova alionyesha Adamu na Eva muti moja wa matunda na akawaambia kama wakikula matunda ya muti huo watakufa.

Malaika mumoja alimupinga Mungu. Ule malaika mubaya anaitwa Shetani Ibilisi.

Shetani hakupenda Adamu na Eva wamutii ao kumusikia Yehova. Basi, alitumia nyoka ili kumuambia Eva kama akikula matunda ya muti huo hatakufa, lakini atakuwa sawa na Mungu. Alimudanganya kabisa.​—Mwanzo 3:1-5.