Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA 11

Yehova Anasikilizaka Sala Zetu

Yehova Anasikilizaka Sala Zetu

Mungu anasikilizaka sala zetu. 1 Petro 3:12

Yehova ni “Musikiaji wa sala.” (Zaburi 65:2) Anapenda tumuambie mambo yenye kutoka mu moyo wetu.

Usali tu kwa Yehova, hapana kwa mutu mwingine.

Tunaweza kusali juu ya mambo mingi. 1 Yohana 5:14

Usali ili mapenzi ya Mungu ifanyike mbinguni na ku dunia.

Usali mu jina la Yesu ili kuonyesha kama unaona mambo yenye alikufanyia kuwa ya maana sana.

Umuombe Yehova akusaidie ufanye mambo ya muzuri. Unaweza pia kusali ili akusaidie kupata chakula, kazi, makao, manguo, na ukuwe na afya ya muzuri.