Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA 7

Yesu Alikuwa Nani?

Yesu Alikuwa Nani?

Yehova alimutuma Yesu hapa ku dunia. 1 Yohana 4:9

Kama tunapenda kumufurahisha Yehova, tunapaswa kusikiliza mutu mwingine wa maana sana. Wakati murefu mbele ya kuumba Adamu, Yehova aliumba malaika mumoja mwenye nguvu kule mbinguni.

Kisha wakati fulani, Yehova alituma ule malaika azaliwe ku dunia. Bikira mwenye aliitwa Maria njo mwenye alimuzaa mu muji wa Betlehemu. Ule mutoto aliitwa Yesu.​—Yohana 6:38.

Wakati Yesu alikuwa mwanadamu ku dunia, alionyesha sifa za Mungu kwa ukamilifu. Alikuwa mwema, mwenye upendo, na watu hawakuogopa kumukaribia ili kuzungumuza naye. Bila kuogopa, alifundisha wengine kweli juu ya Yehova.

Yesu alifanya mambo ya muzuri lakini watu walimuchukia. 1 Petro 2:21-24

Tena, Yesu aliponyesha wagonjwa na kufufua watu fulani wenye walikuwa wamekufa.

Viongozi wa dini (réligion) walimuchukia Yesu juu alionyesha waziwazi mafundisho yao ya uongo na matendo yao ya mubaya.

Viongozi wa dini walisukuma Waroma ili wamupige Yesu na kumuua.