Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 3

Rahabu Alimuamini Yehova

Rahabu Alimuamini Yehova

Wazia tunaishi katika muji wa Yeriko. Muji huo unapatikana mu inchi ya Kanaani. Watu wa muji huo hawamuamini Yehova. Lakini katika muji huo kuko mwanamuke anayeitwa Rahabu.

Wakati Rahabu alikuwa angali mutoto mudogo alisikia hadisi juu ya Musa. Alisikia vile Musa aligawanya Bahari Nyekundu. Alisikia pia vile Musa aliwaondoa Waisraeli katika inchi ya Misri. Tena, Rahabu alisikia vile Yehova aliwasaidia Waisraeli kushinda maadui zao katika vita mbalimbali. Sasa, Rahabu anasikia kama Waisraeli wako karibu na Yeriko!

Rahabu anawaficha wapelelezi juu alimuamini Yehova

Siku moja mangaribi, Waisraeli wawili walikuja mu muji wa Yeriko ili kupeleleza muji huo. Nao wakafika kwa Rahabu. Naye Rahabu akawakaribisha mu nyumba yake. Wakati wa usiku, watu wanamuambia mufalme wa Yeriko kama wapelelezi wamekwisha kuingia mu muji, na wako kwa Rahabu. Kwa hiyo, mufalme anatuma wanaume ili kuwakamata wapelelezi hao. Rahabu anawaficha wapelelezi katika sehemu ya juu ya nyumba yake. Kisha Rahabu anawaambia hivi wanaume wenye mufalme alituma: ‘Ni kweli wapelelezi walikuwa hapa, lakini wamekwisha kuondoka katika muji. Mukiwafuata sasa, munaweza kuwakamata!’ Unajua ni juu ya nini Rahabu anawaficha wapelelezi hao?— Ni juu Rahabu anamuamini Yehova na anajua kama Yehova atawapatia Waisraeli inchi ya Kanaani.

Wapelelezi hao wanataka kuenda. Lakini mbele ya kuenda wanamuambia Rahabu hivi: ‘Weye na wazazi wako na ndugu zako mutaokoka wakati Yeriko itaharibiwa.’ Unajua mambo yenye wapelelezi wanamuomba Rahabu afanye?— Wanamuambia hivi: ‘Kamata kamba hii ya rangi nyekundu na uifunge ku dirisha ya nyumba yako. Ukifanya hivyo, kila mutu mwenye iko mu nyumba yako hatakufa.’ Rahabu alifanya kabisakabisa kama vile wapelelezi walimuambia. Unajua ni nini ilitokea kisha wapelelezi kuenda?—

Yehova aliokoa Rahabu na wazazi wake na ndugu zake

Kisha siku kidogo, Waisraeli wanafika Yeriko. Wanatembea kwa kuzunguka muji huo bila kufanya fujo. Wanazunguka muji mara moja kila siku kwa siku sita. Lakini siku ya saba wanazunguka muji mara saba. Kisha wote wanapiga kelele kwa sauti kubwa. Yehova akafanya ukuta wenye kuzunguka muji wa Yeriko ubomoke na kuanguka chini. Lakini nyumba yenye ilikuwa na kamba ya rangi nyekundu ku dirisha haikubomoka hata kidogo! Unaona nyumba hiyo ku hii picha?— Rahabu na wazazi wake na ndugu zake wanaokoka!

Mufano wa Rahabu unakufundisha nini?— Rahabu alimuamini Yehova juu alisikia mambo ya ajabu yenye Yehova alifanya. Weye pia unajifunza mambo mingi ya ajabu yenye Yehova alifanya. Unamuamini Yehova kama vile Rahabu?— Tunajua kama unafanya vile!