Yesu​—Ni Njia, Kweli, na Uzima

Katika kitabu hiki, soma kuhusu kila tukio katika maisha ya Yesu lenye limeandikwa katika Biblia.

UTANGULIZI

Njia, Kweli, na Uzima

Mafundisho ya Yesu na matendo yake, yenye inapatikana katika vitabu vya Injili, inaweza kubadilisha maisha yako.

SURA YA 1

Ujumbe Mbili Kutoka kwa Mungu

Malaika Gabrieli alitoa ujumbe wenye ulikuwa vigumu kuamini.

SURA YA 2

Yesu Anapewa Heshima Mbele ya Kuzaliwa Kwake

Namna gani Elizabeti na mutoto mwenye kuwa katika tumbo lake la uzazi walimupatia Yesu heshima?

SURA YA  3

Mutu Fulani wa Kutayarisha Njia Anazaliwa

Kisha tu Zekaria kurudishiwa uwezo wake wa kusema kwa njia ya muujiza, alitoa unabii wa maana.

SURA YA 4

Maria Iko na Mimba Lakini Hajaolewa

Je, Yosefu anaamini wakati Maria anamuambia kama iko na mimba kwa nguvu za roho takatifu, lakini si ya mwanaume fulani?

SURA YA 5

Yesu Alizaliwa Wapi na Wakati Gani?

Tunajua namna gani kama Yesu hakuzaliwa tarehe 25 Mwezi wa 12?

SURA YA 6

Mutoto Mwenye Aliahidiwa

Wakati Yosefu na Maria wanamupeleka mutoto Yesu kwenye hekalu, Waisraeli wawili wenye kuzeeka wanatoa unabii juu ya wakati unaokuja wa Yesu.

SURA YA 7

Watu Wenye Elimu ya Nyota Wanaenda Kumuona Yesu

Sababu gani nyota yenye waliona mwanzoni Mashariki iliwapeleka kwa Mufalme muuaji Herode kuliko kuwapeleka mara moja kwenye Yesu iko?

SURA YA 8

Wanakimbia Mutawala Mukali

Unabii tatu wa Biblia kuhusu Masiya umetimia mwanzoni mwa maisha ya Yesu.

SURA YA 9

Anakomalia Katika Nazareti

Ndugu na dada wa Yesu wako ngapi?

SURA YA 10

Yesu na Familia Yake Wanasafiri Kuenda Yerusalemu

Yosefu na Maria wako na wasiwasi wakati hawamupate Yesu, wakati huo Yesu anashangaa kusikia kuwa hawakujua palepale nafasi kwenye walipaswa kumutafutia.

SURA YA 11

Yohana Mubatizaji Anatayarisha Njia

Wakati Wafarisayo fulani na Wasadukayo wanakuja kwa Yohana, Anawalaumu. Sababu gani?

SURA YA 12

Yesu Anabatizwa

Sababu gani Yesu anabatizwa hata kama hajafanyaka zambi?

SURA YA 13

Mambo Tunaweza Kujifunza Kupitia Namna Yesu Alipambana na Majaribu

Majaribu yenye Yesu alipata yanaonyesha mambo mbili ya musingi juu ya Ibilisi.

SURA YA 14

Yesu Anaanza Kufanya Wanafunzi

Ni nini ilisadikishia wanafunzi sita wa kwanza wa Yesu kwamba wamepata Masiya?

SURA YA 15

Anafanya Muujiza Wake wa Kwanza

Yesu anamuambia mama yake kama haiko yeye ndiye anamuongoza kwa sasa, lakini anaongozwa na Baba yake wa mbinguni.

SURA YA 16

Yesu Anaonyesha Bidii kwa Ajili ya Ibada ya Kweli

Sheria ya Mungu iliruhusu watu kuuza wanyama katika Yerusalemu kwa ajili ya toleo, sasa, sababu gani Yesu anakasirikia wafanyabiashara katika hekalu?

SURA YA 17

Anafundisha Nikodemo Wakati wa Usiku

“Kuzaliwa tena,” maana yake nini?

SURA YA 18

Yesu Anaongezeka na Yohana Anapunguka

Wanafunzi wa Yohana Mubatizaji wako na wivu, hata kama Yohana yeye hana wivu.

SURA YA 19

Anafundisha Mwanamuke Musamaria

Yesu anamuambia mwanamuke huyo jambo lenye pengine hajaambia mutu yeyote.

SURA YA 20

Muujiza wa Pili Katika Kana

Yesu anaponyesha mutoto kwa mbali, kwenye kilometre 26.

SURA YA 21

Kwenye Sinagogi ya Nazareti

Yesu alisema jambo gani lenye lilifanya watu wa muji wake watafute kumuua?

SURA YA 22

Wanafunzi Ine Watakuwa Wavuvi wa Watu

Anawaomba waache kufanya aina fulani ya kazi ya kuvua na waanze kufanya aina ingine.

SURA YA 23

Yesu Anafanya Miujiza Katika Kapernaumu

Wakati Yesu iko anafukuza pepo wachafu, anakataza pepo hao wachafu kuambia watu kama yeye ni Mwana wa Mungu. Sababu gani?

SURA YA 24

Utumishi Wake Unapanuka Katika Galilaya

Watu wanakuja kwa Yesu ili awaponyeshe, lakini Yesu anafasiria kuwa utumishi wake uko na kusudi kubwa zaidi.

SURA YA 25

Anaponyesha Mutu Mwenye Ukoma kwa Huruma

Kwa kutumia maneno mepesi lakini yenye nguvu, Yesu anaonyesha kuwa anahangaikia kabisa watu wenye anaponyesha.

SURA YA 26

“Zambi Zako Zimesamehewa”

Yesu anaonyesha kuwa kuko uhusiano gani kati ya zambi na magonjwa?

SURA YA 27

Matayo Anaalikwa

Sababu gani Yesu anakula chakula na watu wenye kujulikana kuwa watenda-zambi?

SURA YA 28

Sababu Gani Wanafunzi wa Yesu Hawafunge?

Yesu anatumia mufano juu ya chupa ya ngozi ya kuwekea divai ili kutoa jibu.

SURA YA 29

Mutu Anaweza Kufanya Matendo ya Muzuri Siku ya Sabato?

Juu ya nini Wayahudi wanamutesa Yesu kwa sababu anaponyesha mwanaume mwenye alikuwa mugonjwa kwa miaka 38?

SURA YA 30

Uhusiano wa Yesu Pamoja na Baba Yake

Wayahudi wanafikiri kuwa Yesu anajifanya sawasawa na Mungu, lakini Yesu anaonyesha wazi kuwa Mungu ni mukubwa kuliko yeye.

SURA YA 31

Wanakata Masuke ya Nafaka Siku ya Sabato

Sababu gani Yesu anajiita “Bwana wa Sabato”?

SURA YA 32

Ni Nini Inaruhusiwa Kufanya Siku ya Sabato?

Kwa kawaida Wasadukayo na Wafarisayo hawasikilizane; sasa wanajiunga kwa ajili ya jambo moja.

SURA YA 33

Anatimiza Unabii wa Isaya

Sababu gani Yesu anakataza wale wote wenye anaponyesha wasiambie wengine yeye ni nani ao kusema mambo yenye amefanya?

SURA YA 34

Yesu Anachagua Mitume Kumi na Mbili

Kuko tofauti gani kati ya mutume na mwanafunzi?

SURA YA 35

Mahubiri ya Mulimani Yenye Kujulikana Sana

Pata mafasirio ya mambo makubwa ya mahubiri ya Yesu.

SURA YA 36

Mukubwa Fulani wa Jeshi Anaonyesha Imani Kubwa

Mukubwa huyo wa jeshi anafanya jambo gani lenye linamushangaza Yesu?

SURA YA 37

Yesu Anafufua Mutoto wa Mujane

Wale wenye waliona muujiza huo walielewa kabisa maana.

SURA YA 38

Yohana Anapenda Kupata Habari Juu ya Yesu

Sababu gani Yohana Mubatizaji anauliza ikiwa Yesu ndiye Masiya? Je, Yohana anakosa imani?

SURA YA 39

Ole kwa Kizazi Chenye Kukataa Kusikiliza

Yesu anasema kuwa katika Siku ya Hukumu, itakuwa mwepesi zaidi kwa Sodoma kuliko kwa Kapernaumu, muji wenye ulikuwa makao yake makubwa.

SURA YA 40

Anafundisha Watu Kusamehe

Kwa kuambia mwanamuke mwenye alikuwa mwasherati kama zambi zake zimesamehewa, je, Yesu alikuwa anasema kama haiko mubaya kuvunja sheria za Mungu?

SURA YA 41

Anafanya Miujiza kwa Nguvu za Nani?

Ndugu za Yesu wanawaza kuwa amepoteza akili.

SURA YA 42

Yesu Anakemea Wafarisayo

“Alama ya nabii Yona” ni nini?

SURA YA 43

Mifano Mbalimbali Kuhusu Ufalme

Yesu anatoa mifano munane ili kufasiria mambo mbalimbali juu ya Ufalme wa mbinguni.

SURA YA 44

Yesu Ananyamazisha Upepo Mukali Kwenye Bahari

Wakati Yesu alituliza upepo na mawimbi, alifundisha jambo la maana sana juu ya namna maisha yatakuwa wakati wa utawala wake katika Ufalme wa mbinguni.

SURA YA 45

Iko na Mamlaka Juu ya Pepo Wengi Wachafu

Je, mutu anaweza kuwa na pepo wengi wachafu?

SURA YA 46

Anaponyeshwa kwa Kugusa Nguo ya Yesu

Yesu anaonyesha kuwa iko na uwezo na huruma katika hali hii yenye kugusa moyo.

SURA YA 47

Mutoto Mwanamuke Anaishi Tena!

Watu wanamucheka Yesu wakati anasema kuwa mutoto mwanamuke mwenye amekufa ni mwenye kulala tu usingizi. Ni jambo gani lenye Yesu anajua ambalo watu hao hawajue?

SURA YA 48

Anafanya Miujiza, Lakini Anakataliwa Hata Katika Nazareti

Watu wa Nazareti wanamukataa Yesu, haiko kwa sababu ya mafundisho ao miujiza yake, lakini wanamukataa juu sababu ingine.

SURA YA 49

Anahubiri Katika Galilaya na Anazoeza Mitume

Maneno ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia’ yanamaanisha kabisa nini?

SURA YA 50

Wanatayarishwa Kuhubiri Hata Katika Mateso

Sababu gani anawaambia wakimbie wakati wanateswa ikiwa hapaswe kuogopa kifo?

SURA YA 51

Mutu Anauawa Wakati wa Karamu ya Sikukuu ya Kuzaliwa

Namna Salome anacheza dansi inafurahisha Herode sana hivi kwamba anamuahidi kumupatia kitu chochote chenye ataomba. Ni kitu gani chenye anaomba chenye kinaleta huzuni sana?

SURA YA 52

Anatumia Mikate Tano na Samaki Wawili ili Kukulisha Maelfu ya Watu

Muujiza wa Yesu ni wa maana sana hivi kwamba vitabu vyote ine vya Injili vinauzungumuzia.

SURA YA 53

Mutawala Mwenye Kuwa na Mamlaka Juu ya Nguvu za Asili

Mitume wanajifunza mambo gani wakati Yesu anatembea juu ya maji na kutuliza upepo?

SURA YA 54

Yesu Ni “Mukate wa Uzima”

Sababu gani Yesu anakemea watu hata kama wamejikaza sana ili kuja kwenye iko?

SURA YA 55

Watu Wengi Wanakwazika kwa Sababu ya Maneno ya Yesu

Yesu anafundisha jambo fulani lenye linakwaza sana watu hivi kwamba wanafunzi wake wengi wanaacha kumufuata.

SURA YA 56

Mutu Anachafuliwa na Nini?

Ni kile chenye kinaingia katika kinywa chake, ao kile chenye kinatoka?

SURA YA 57

Yesu Anaponyesha Mutoto Mwanamuke na Mwanaume Mwenye Kuwa Kiziwi

Sababu gani mwanamuke hakwazike wakati Yesu analinganisha watu wa taifa lake na imbwa wadogo?

SURA YA 58

Anazidisha Mikate na Kuonya Juu ya Chachu

Mwishowe, wanafunzi wa Yesu wanaelewa aina ya chachu yenye iko anazungumuzia.

SURA YA 59

Mwana wa Binadamu Ni Nani?

Funguo za Ufalme ni gani? Ni nani anazitumia, na namna gani?

SURA YA 60

Kugeuzwa Sura: Kristo Anaonekana Katika Utukufu

Kugeuzwa sura kulifanyika namna gani? Na tukio hilo lilimaanisha nini?

SURA YA 61

Yesu Anaponyesha Kijana Mwanaume Mwenye Kuwa na Pepo Muchafu

Yesu anasema kama ule kijana mwanaume hakuponyeshwa kwa sababu ya kukosa imani, lakini ni nani ndiye alikosa imani? Ni kijana mwanaume, baba yake, ao wanafunzi wa Yesu?

SURA YA 62

Anafundisha Somo la Maana Kuhusu Unyenyekevu

Wanaume wenye kukomaa wanajifunza jambo fulani la maana kupitia mutoto mudogo.

SURA YA 63

Yesu Anatoa Mashauri Kuhusu Kukwaza Wengine na Kuhusu Zambi

Anaonyesha hatua tatu za kufuata ili kumaliza magumu kati ya ndugu.

SURA YA 64

Ni Jambo la Lazima Kusamehe

Kwa kutumia mufano wa mutumwa mwenye hana huruma, Yesu anaonyesha kama Mungu anaona kuwa ni jambo la maana sana kuwa tayari kusamehe wengine.

SURA YA 65

Anafundisha Katika Safari Yake ya Kuenda Yerusalemu

Katika mazungumuzo hayo tatu ya mufupi-mufupi, Yesu anaonyesha mambo yenye yanaweza kuzuia mutu kuwa mwanafunzi wake.

SURA YA 66

Iko Katika Yerusalemu kwa Ajili ya Sikukuu ya Tabenakulo

Ni nini yenye ilifanya wale wenye walikuwa wanamusikiliza Yesu waamini kuwa iko na pepo muchafu?

SURA YA 67

“Hakuna Mutu Mwenye Amekwisha Kusema Kama Mutu Huyu”

Tribinali yote kubwa ya Wayahudi wanamupinga Yesu, lakini mutu mumoja anapata ujasiri wa kumusemea.

SURA YA 68

Mwana wa Mungu Ni “Mwangaza wa Ulimwengu”?

Yesu alisema, “kweli itawaweka ninyi huru.” Huru kutoka nini?

SURA YA 69

Baba yao Ni Nani: Abrahamu ao Ibilisi?

Yesu anaonyesha namna ya kutambua watoto wa Abrahamu, na pia anaonyesha kuwa Baba yake ni nani kabisa.

SURA YA 70

Yesu Anaponyesha Mwanaume Mwenye Alizaliwa Kipofu

Wanafunzi wanauliza sababu gani mwanaume fulani alizaliwa kipofu. Alifanya zambi? Ni wazazi wake ndio walifanya zambi? Watu wanatenda kwa namna tofauti wakati Yesu anamuponyesha.

SURA YA 71

Wafarisayo Wanauliza Maulizo Mwanaume Mwenye Alikuwa Kipofu

Mawazo yenye kupatana na akili ya mwanaume mwenye alikuwa kipofu zamani yanakasirikisha Wafarisayo. Kama vile tu wazazi wake walikuwa wanaogopa, Wafarisayo wanamufukuza katika sinagogi.

SURA YA 72

Yesu Anatuma Wanafunzi 70 ili Waende Kuhubiri

Katika Yudea, Yesu anatuma wanafunzi 70 kama watangazaji wa Ufalme, wawili-wawili. Wanafunzi hao watapata watu wapi—katika masinagogi ao kwenye nyumba za watu?

SURA YA  73

Musamaria Anaonyesha Kuwa Yeye Ni Jirani wa Kweli

Namna gani Yesu anatumia mufano wa Musamaria mwema, ili kufundisha somo la maana sana?

SURA YA 74

Anafundisha Kuhusu Ukaribishaji-Wageni na Kuhusu Sala

Yesu anatembelea Maria na Marta kwenye nyumba yao. Anawafundisha nini kuhusu ukaribishaji-wageni? Na kisha, namna gani anafundisha wanafunzi wake kuhusu mambo yenye wanapaswa kumuomba Mungu?

SURA YA 75

Yesu Anaonyesha Siri ya Kupata Furaha

Yesu anajibia maadui wake kwa kuwaambia juu ya “kidole cha Mungu” na juu ya namna Ufalme wa Mungu umekwisha kuwafikia. Anaonyesha pia namna watu wanaweza kupata furaha ya kweli.

SURA YA 76

Anakula Pamoja na Mufarisayo

Yesu anafunua unafiki wa waandishi na Wafarisayo. Ni mizigo gani mizito wanakaza watu wabebe?

SURA YA 77

Yesu Anatoa Mashauri Kuhusu Utajiri

Yesu anatoa mufano wa mwanaume mumoja tajiri mwenye alijenga madepo makubwa zaidi. Anarudilia shauri gani kuhusu hatari za kutafuta utajiri?

SURA YA 78

Musimamizi-Nyumba Mwaminifu, Endelea Kuwa Tayari!

Yesu anaonyesha kuwa anahangaikia hali ya muzuri ya kiroho wanafunzi wake. Ili wakuwe na hali ya muzuri ya kiroho, musimamizi-nyumba huyo atakuwa na daraka gani? Sababu gani shauri la kuendelea kuwa tayari ni la maana sana?

SURA YA 79

Sababu Gani Uharibifu Uko Unakuja

Yesu anasema kuwa wale wenye iko anajikaza kusaidia wako katika hatari ya kuhabiriwa ikiwa hawatubu. Je, watajifunza somo la maana lenye Yesu anajikaza kuwafundisha kuhusu urafiki wao pamoja na Mungu?

SURA YA 80

Muchungaji Mwema na Mazizi ya Kondoo

Uhusiano kati ya muchungaji na kondoo unaonyesha muzuri namna Yesu anajisikia juu ya wanafunzi wake. Je, watatambua mafundisho yake na kufuata muongozo wake?

SEHEMU YA 81

Yesu na Baba Ni Kitu Kimoja, Lakini Haiko Mungu

Maadui fulani wa Yesu wanamushitaki kuwa iko anajifanya sawasawa na Mungu. Namna gani Yesu anapinga kwa hekima shitaka lao la uongo?

SURA YA 82

Utumishi wa Yesu Katika Perea

Yesu anaambia wasikilizaji wake kile wanapaswa kufanya ili kuokolewa. Shauri lake lilikuwa la maana zamani. Halafu leo?

SURA YA 83

Mialiko Kwenye Chakula

Wakati iko anakula kwenye nyumba ya Mufarisayo mumoja, Yesu anatoa mufano kuhusu chakula kikubwa cha mangaribi. Anatolea watu wote wa Mungu somo la maana. Ni somo gani hilo?

SURA YA 84

Kuwa Mwanafunzi wa Yesu Ni Daraka Nzito

Kuwa mwanafunzi wa Kristo ni daraka nzito. Yesu anaonyesha waziwazi mambo yenye yanaombwa ili kuwa mwanafunzi wake. Pengine maneno yake yanakwaza watu fulani wenye wangekuwa wafuasi wake.

SURA YA 85

Wanafurahi Wakati Mutenda-Zambi Anatubu

Waandishi na Wafarisayo wanamulaumu Yesu kwa sababu anasaidia watu wa kawaida. Ili kuwajibu, Yesu anatumia mifano ili kuonyesha namna Mungu anaona watenda-zambi.

SURA YA 86

Mutoto Mwenye Alipotea Anarudia

Mufano wa Yesu wa mutoto mupotevu unaweza kutufundisha nini?

SURA YA 87

Tumia Hekima Yenye Kutenda kwa Kupanga Mambo Mbele ya Wakati

Yesu anatumia mufano wa musimamizi-nyumba mujanja, na mwenye haiko mwaminifu ili kufundisha kweli yenye kushangaza.

SURA YA 88

Kubadilika kwa Hali ya Tajiri na Hali ya Lazaro

Ili kuelewa mufano wa Yesu ni lazima kutambua watu wawili wenye kuzungumuziwa sana wanafananisha nani.

SURA YA 89

Anafundisha Katika Perea Wakati Iko Anaenda Yudea

Anazungumuzia sifa yenye inaweza kutusaidia tusamehe wengine hata wale wenye wametukosea mara nyingi.

SURA YA 90

“Ufufuo na Uzima”

Yesu anamaanisha nini wakati alisema kwamba wale wenye wanamuamini “hawatakufa hata kidogo”?

SURA YA 91

Lazaro Anafufuliwa

Hali mbili za maana katika tukio hili, zinafanya isiwezekane kabisa kwa wapinzani wa Yesu kukataa muujiza.

SURA YA 92

Watu Kumi Wenye Ukoma Wanaponyeshwa ​—Mumoja Anaonyesha Shukrani

Mutu mwenye ameponyeshwa anaonyesha shukrani yake, hapana kwa Yesu tu lakini pia kwa mutu mwengine.

SURA YA 93

Mwana wa Binadamu Atafunuliwa

Namna gani kuwapo kwa Kristo kutafanana na mwangaza wa radi?

SURA YA 94

Mambo Mbili ya Lazima Sana​—Sala na Unyenyekevu

Katika mufano wake wa mwamuzi muovu na mujane, Yesu anakazia samani ya sifa fulani ya pekee.

SURA YA 95

Anafundisha Kuhusu Kuvunja Ndoa na Somo Kuhusu Watoto

Namna Yesu anaona watoto iko tofauti sana na namna wanafunzi wake wanawaona. Sababu gani?

SURA YA 96

Yesu Anamujibu Mutawala Kijana Mwenye Kuwa Tajiri

Ni nini ilimuchochea Yesu kusema kama ni vyepesi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la shindano ya kushonea kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu?

SURA YA 97

Mufano wa Wafanyakazi Katika Shamba la Mizabibu

Namna gani wa kwanza wanakuwa wa mwisho na wa mwisho wanakuwa wa kwanza?

SURA YA 98

Mitume Wanabishana Tena ili Kutafuta Ukubwa

Yakobo na Yohana wanaomba fasi ya pekee katika Ufalme, lakini haiko wao wenyewe tu.

SURA YA 99

Yesu Anaponyesha Vipofu Wanaume na Anasaidia Zakayo

Namna gani tunaweza kupatanisha maelezo ya Biblia yenye kuonekana kuwa tofauti, yenye kuzungumuzia Yesu akiponyesha kipofu mwanaume karibu na Yeriko?

SURA YA 100

Mufano Wake wa Mina Kumi

Yesu alimaanisha nini wakati alisema: “Kila mutu mwenye kuwa na kitu, ataongezewa, lakini ule mwenye hana, hata kile chenye iko nacho kitachukuliwa”?

SURA YA 101

Anatumia Chakula Katika Nyumba ya Simoni Katika Betania

Maria, dada yake na Lazaro, anafanya jambo lenye linaleta mabishano, lakini Yesu anamutetea.

SURA YA 102

Mufalme Anaingia Yerusalemu Akiwa Juu ya Mwana-punda

Anatimiza unabii wenye ulitabiriwa miaka mia tano mbele.

SURA 103

Anasafisha Tena Hekalu

Wafanya-biashara katika Yerusalemu wanaoneka kuwa wanaendesha biashara yenye kukubalika, basi, sababu gani anawaita wanyanganyi?

SURA YA 104

Wayahudi Wanasikia Sauti ya Mungu​—Wataonyesha Imani?

Kuko tofauti kati ya kumuamini Yesu na kutenda kulingana na imani hiyo?

SURA YA 105

Anatumia Muti wa Tini ili Kufundisha Somo Fulani Kuhusu Imani

Yesu anafundisha wanafunzi wake kuhusu uwezo wa imani na anawaelezea sababu gani Mungu anakataa taifa la Israeli.

SURA YA 106

Anatoa Mifano Mbili Kuhusu Mashamba ya Mizabibu

Tafuta maana ya mifano ya mwanaume mwenye aliomba watoto wake watumike katika shamba lake la mizabibu na ya mwanaume mwenye alipangisha shamba lake la mizabibu kwa walimaji.

SURA YA 108

Wanashindwa Kumunasa Yesu Katika Mitego Yao

Ananyamazisha kwanza Wafarisayo, kisha Wasadukayo, na mwishowe maadui wake wenye walijiunga pamoja.

SURA YA 109

Anakemea Waziwazi Viongozi Wa Dini Wenye Kumupinga

Sababu gani Yesu havumilie makosa yenye kutendeka katika dini?

SURA YA 110

Siku ya Mwisho ya Yesu Kwenye Hekalu

Anatoa mufano wa mujane masikini ili kufundisha somo la muzuri.

SURA YA 111

Mitume Wanaomba Alama

Unabii wake ulitimia kwa mara ya kwanza wakati wa mitume. Je, ungekuwa na utimizo mwengine mukubwa zaidi?

SURA YA 112

Mufano wa Mabikira Kumi​—Somo Kuhusu Kukesha

Je, Yesu alifundisha kama nusu ya wanafunzi wake ni wapumbavu na nusu ni wenye busara?

SURA YA 113

Mufano wa Talanta​—Somo Kuhusu Bidii

Mufano wa Yesu unaonyesha kanuni yake: “Kila mutu mwenye kuwa na kitu, ataongezewa.”

SURA YA 114

Mufalme Yesu Kristo Anahukumu Kondoo na Mbuzi

Akitumia mufano wenye kugusa moyo, Yesu anaonyesha hukumu ya milele itafanywa juu ya musingi gani.

SURA YA 115

Pasaka ya Mwisho ya Yesu Inakaribia

Viongozi wa dini wanaitika kumulipa Yuda vipande 30 vya feza ili amusaliti Yesu. Jambo hilo linatukumbusha nini?

SURA YA 116

Anafundisha Unyenyekevu Kwenye Pasaka ya Mwisho

Anashangaza mitume wake kwa kufanya kazi ya mutumwa.

SURA YA 117

Chakula cha Mangaribi cha Bwana

Yesu alianzisha ukumbusho wenye wafuasi wake wanaombwa kufanya tarehe 14 Mwezi wa Nisani ya kila mwaka.

SURA YA 118

Wanabishana ili Kujua Ni Nani Ndiye Mukubwa Zaidi Kati yao

Mitume wamekwisha kusahau somo lenye Yesu aliwafundisha hapo mbele mangaribi hiyo.

SURA YA 119

Yesu​—Ni Njia, Kweli, na Uzima

Yesu anafundisha kweli nzito juu ya namna ya kumukaribia Mungu.

SURA YA 120

Kuzaa Matunda Kama Matawi na Kuwa Marafiki wa Yesu

Ni katika njia gani wanafunzi wa Yesu “wanazaa matunda”?

SURA YA 121

“Musiogope! Mimi Nimepata Ushindi juu ya Ulimwengu”

Namna gani Yesu alishinda ulimwengu hata kama ulimwengu ulimuua?

SURA YA 122

Sala ya Mwisho ya Yesu Katika Chumba cha Juu

Anaonyesha waziwazi kuwa alitimiza jambo la maana zaidi kuliko kuletea wanadamu wokovu.

SURA YA 123

Anasali Wakati Iko na Huzuni Nyingi

Sababu gani Yesu anasali: “Uniondolee kikombe hiki”? Anakataa daraka lake wa kufa ili kukomboa wanadamu?

SURA YA 124

Kristo Anasalitiwa na Kufungwa

Yuda anamupata Yesu hata kama ni katikati ya usiku.

SURA YA 125

Yesu Anapelekwa kwa Anasi, Kisha kwa Kayafa

Wanamusambisha Yesu bila kufuata sheria.

SURA YA 126

Petro Anamukana Yesu Kwenye Nyumba ya Kayafa

Namna gani Petro mutu mwenye alikuwa na imani na ushikamanifu, angeweza kumukana mbio Yesu?

SURA YA 127

Sanhedrini Inamusambisha, Kisha Anapelekwa kwa Pilato

Viongozi wa dini Wayahudi wanafunua nia yao ya kweli.

SURA YA 128

Pilato na Herode Wanaona Kuwa Yesu Hana Kosa

Why does Pilate send Jesus to Herod for judgment? Does Pilate not have the authority to judge Jesus?

SURA YA 129

Pilato Anasema: “Muangalie! Mwanaume!”

Hata Pilato anaona sifa za muzuri sana zenye Yesu anaonyesha.

SURA YA 130

Yesu Anatolewa na Kupelekwa ili Auawe

Sababu gani Yesu anaambia wanamuke wenye kulia wajililie wao wenyewe na watoto wao kuliko kumulilia?

SURA YA 131

Mufalme Mwenye Hana Kosa Anateseka Kwenye Muti

Yesu atolea mutenda zambi mumoja mwenye kutundikwa pembeni yake tumaini la wakati wenye kuja.

SURA YA 132

“Hakika Huyu Alikuwa Mwana wa Mungu”

Giza la muujiza lenye lilitokea muchana, tetemeko kubwa la inchi, na kupasuka kwa pazia yote yanahakikisha jambo moja.

SURA YA 133

Mwili wa Yesu Unatayarishwa na Kuzikwa

Sababu gani maziko ya Yesu yalifanywa haraka mbele ya jua kushuka?

SURA YA 134

Kaburi Liko Wazi, Kwa Sababu Yesu Ni Mwenye Kuishi!

Kisha Yesu kufufuliwa, anatokea kwanza mwanafunzi mwanamuke kuliko kutokea mitume wake.

SURA YA 135

Yesu Mwenye Amefufuliwa Anatokea Wengi

Namna gani Yesu anahakikishia wanafunzi wake kuwa amefufuliwa?

SURA YA 136

Pembeni ya Bahari ya Galilaya

Petro anakumbushwa mara tatu namna anaweza kuonyesha kuwa anamupenda Yesu.

SURA YA 137

Mamia Wanamuona Mbele ya Pentekoste

Tangu wakati alifufuliwa mupaka wakati alipanda mbinguni, Yesu aliambia mara kwa mara wanafunzi wake jambo lenye wangepata na namna gani walipaswa kulitumia.

SURA YA 138

Kristo Iko Kwenye Mukono wa Kuume wa Mungu

Yesu anafanya nini wakati anangojea wakati wa kutenda juu ya maadui wake?

SURA YA 139

Yesu Analeta Paradiso na Kumaliza Mugawo Wake

Angali na mengi ya kufanya mbele arudishe Ufalme kwa Mungu na Baba yake.

Ili Kufuata Mufano wa Yesu, Ukuwe . . .

Mara nyingi katika maisha yake, Yesu alionyesha sifa munane.

Endekse ya Maandiko

Tumia endekse hii ili kujua ni wapi katika kitabu maandiko yenye kuwa katika vitabu vya Injili yanazungumuziwa.

Endekse ya Mifano

Tafuta sura katika kitabu hiki yenye inazungumuzia kila mufano.

Unabii Fulani Kuhusu Masiya

Patanisha matukio fulani katika maisha ya Yesu na unabii mbalimbali wa Biblia wenye kuonyesha kuwa yeye ni Masiya; na upatanishe sura za kitabu hiki kwenye unabii huo unazungumuziwa.

Maeneo Kwenye Yesu Aliishi na Kufundisha

Karte hii inaonyesha mahali kwenye Yesu alifanya utumishi wake.